Elections 2010 NEC: Wananchi wakae mita 100 kutoka vituo vya kura

Elections 2010 NEC: Wananchi wakae mita 100 kutoka vituo vya kura

Mhabarishaji

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2010
Posts
1,007
Reaction score
600
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imevishauri vyombo vya dola kutowabughudhi wananchi watakaokaa mita 100 kwenye maeneo ya vituo vya kupigia kura baada ya kumaliza kupiga kura.

Ushauri huo ylitolewa jana na Makamu Mwenyekiti wa Tume hiyo, Omari makungu wakati akijibu hoja iliyowasilishwa na Mwenyekiti wa Chadema mkoani kagera, Wilfred Lwakatare kwenye mkutano wa tume na vyama vya siasa jana.

Katika kikao hicho, Lwakatare ambaye pia ni mgombea ubunge wa jimbo la Bukoba mjini alisema kuna tabia ya vyombo vya dola ya kutumia nguvu kuwatawanya wananchi ambao hupenda kukaa kwenye vituo vya kupiga kura baada ya kupiga kura kusubiri matokeo.

Jaji Makungu alisema katika kanuni na sheria zinazoongoza Tume hakina kipengele kinachowazuia wananchi wasikae kwenye vituo vya kupigia kura.

Alisema mwananchi kukaa kwenye kituo cha kupigia kura ni hiari yake.

Makungu alisema anachotakiwa kufanya mwananchi kufanya ni kutofanya vurugu yoyote na kutokaa kwenye makundi yenye lengo la kuleta uvunjifu wa amani.

Pia alisema mgombea yeyote ana haki ya kuingia kwenye chumba cha kupigia kura kwa ajili ya kuangalia usalama wa kura zake.

CHANZO: Gazeti Mtanzania (19.10.2010)
 
Safi sana. Kumbe tuna haki si kulazimisha. werawera, kuhamasishane tuake vituoni mpaka kieleweke. Mhabaishaji unasoma sana magazeti lete manewz, Tuhakikishe hapiti mtu na kura feki. Mwaka huu noma, miaka yote CCM walikuwa wanajificha nyuma ya Picha ya Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, now hakuna kitu hawapati kiti 2010.

Jeykey and Family poleni sana, tafuteni ikulu yenu wenyewe. Safari njema.

SLAA JUU KIKWETE HAFIKI HATA AKIRUKA.
 
amkeni waambie watu wakampuzike si kuwasumbua na jua jisha matokeo yakiwa si mazuri kwao waanze kusababisha uvunjifu wa amani

na pia wapumzike na kujiaandaa waje kufurahia ushindi wakiwa na nguvu sio wachovu kwa kupigwa na jua na njaa


hatuna vyama vyenye akili Tanzania zaidi ya CCM, hivi kila chama kikisema kikae kituoni kulinda kura hapo kituoni patatosha ?


amkeni nyie watani, Mjj mnamuamini sana kuliko yeyote humu keshawatoa wasi wasi na kukupeni elimu ya vp zoezi zima linavyokua
 
safi sanaaaa,hiyo ni haki ya watu kulinda kura zao
 
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imevishauri vyombo vya dola kutowabughudhi wananchi watakaokaa mita 100 kwenye maeneo ya vituo vya kupigia kura baada ya kumaliza kupiga kura.

Thank you NEC............Dalili za uchaguzi wa huru na haki zimeanza sasa..............................
 
amkeni waambie watu wakampuzike si kuwasumbua na jua jisha matokeo yakiwa si mazuri kwao waanze kusababisha uvunjifu wa amani

na pia wapumzike na kujiaandaa waje kufurahia ushindi wakiwa na nguvu sio wachovu kwa kupigwa na jua na njaa


hatuna vyama vyenye akili Tanzania zaidi ya CCM, hivi kila chama kikisema kikae kituoni kulinda kura hapo kituoni patatosha ?


amkeni nyie watani, Mjj mnamuamini sana kuliko yeyote humu keshawatoa wasi wasi na kukupeni elimu ya vp zoezi zima linavyokua

Mtu wa Pwani, leo umekunywa nini? Lakini ni kawaida yako.
CCM na wengi wa wanachama wake (sio wote) ndo wamelala pono! wanaishi dunia ya kufikirika, hamjatambua kuwa Watanzania wamebadilika na sio makondoo mliokuwa mnayafanya mtaji.

Kuhusu MMK, hakuna aliyekubaliana naye, labda wachache kutoka kambi yenu wanaotaka watu walegeze uzi ili muibe kura sawasawa!
Chama kinachotumia wizi wa kura ili kiingie madarakani si hicho ni mufilisi??!!
 
Ndio maana mimi mwenye nimetafuta hili gazeti la mwananchi nikalipata na habari yenyewe nikaiona kama ilivyoandikwa lakini IPO NDANI SANA UKURASA WA TANO CHINI KUSHOTO nadhani hawakutaka watu wajue hili, njama kubwa wanayotumia kubalisha maboksi ya kura ni kutumia kigezo cha kusogeza watu na kukitoa vurugu ndio watuliza ghasia huweka maboksi ya kura zilizochakachuliwa.
TUKAE HAPO HAPO MPAKA KIELEWEKE.
 
Hahahaha walianza na mita 200 kutoka kituoni, sasa wanakuja na mita 100...tunazidi kukaribia ushindi.
Najua polisi pia mmesikia hili, maana wakati mwingine mnajifanya hamnazo nyie.
Tuacheni tusubiri matokeo kwa uhuru na haki!

Tutakapomaliza hamu yetu ya kuona matokeo, na hasa baada ya kupiga picha na madigito kamera yetu ndipo tutakapo sepa.
 
Tanzania Daima la leo limeripoti ya kuwa NEC wamekanusha haki ya wapigakura kuwa mita 100 kutoka vituo vya kupiga kura wakidai siyo ya kisheria.........sababu iliyotolewa na NEC ni kuwa kwa wapigakura kuwa hizo mita mia moja kuna weza kuwa ndiyo chanzo cha vurugu........

Msimamo huu wa NEC sasa unatofautiana na kauli yao ya awali ambayo waliitoa pale walipokuwa wanajibu swali la mgombea ubunge wa Bukoba mjini Mheshimiwa Rwakatare walipomjibu ni rukhsa kwa wapigakura kuwa mita 100 kutoka kwene vituo vyao vya kupiga kura..............Kauli hizi mbili za NEC zinazotofautiana zinaongeza wasiwasi wa kura kuibiwa kwa kuingiza maboksi yenye kura haramu ambayo yamekuwa yakiongelewa kwa siku kadhaa.

Ushauri wangu kwa wapigakura tuwe macho mahali popote pale kumulika vituo vyetu tulivyopiga kura ili kuzuia mchezo mchafu usifanyike kwenye vituo hivyo..
 
Back
Top Bottom