Elections 2010 NEC wekeni mambo hadharani!

Ilumine

Senior Member
Joined
Dec 27, 2008
Posts
196
Reaction score
4
Nionavyo mimi, ingewezekana kabisa NEC watuwekee link kwenye mtandao wao ili tuweze kuona waziwazi:
1 Majimbo yote ya Uchaguzi katika mikoa yetu,
2. vituo vyote vya kupigia kura vilivyo katika jimbo Fulani la uchaguzi,
3, na kisha tuweze kubofya KITUO, ili orodha ya wapigakura na ID zao zionekane.

Kwa uelewa wangu mdogo wa mambo haya ya IT hii ni kazi ndogo sana kwa sababu Baraza la Mitihani wamekuwa wakiweka hadharani majina yote ya wanafunzi kwa utaratibu mzuri na wa wazi, ambapo, tunaweza kubofya-bofya tukaona kila kitu.

Wakuu hili mnalionaje? Tungeweza kupunguza ‘doubts' ambazo zinaendelea kujitokeza.
Nawasilisha!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…