realMamy
JF-Expert Member
- Apr 28, 2024
- 3,925
- 8,853
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amesema serikali inatambua umuhimu wa wakulima nchini katika kuisaidia nchi kuwa na chakula cha kutosha.
Rais Samia ameeleza hayo Jijini Dodoma wakati wa Kilele cha Maonesho ya NaneNane.
Amesema ndio maana serikali imeamua kujenga Viwanda ikiwamo cha kuunganisha Matrekta yatakayosaidia kufanya kilimo kwa urahisi.
Amewataka wakulima na wafugaji kuishi kwa amani na kupunguza migogoro isiyo na ulazima.
Sambamba na hayo amewataka maafisa ugani kuitumia vizuri taaluma yao katika kuwasaidia wakulima kufanya kilimo chenye tija.
Akihitimisha hotuba yake amewataka wananchi kuchagua viongozi madhubuti watakaowasaidia wananchi kupata maendeleo.
Maadhimishi ya Nanenane yamehudhuriwa na Viongozi mbalimbali pamoja na wadau wa maendeleo nchini.
Rais Samia ameeleza hayo Jijini Dodoma wakati wa Kilele cha Maonesho ya NaneNane.
Amesema ndio maana serikali imeamua kujenga Viwanda ikiwamo cha kuunganisha Matrekta yatakayosaidia kufanya kilimo kwa urahisi.
Amewataka wakulima na wafugaji kuishi kwa amani na kupunguza migogoro isiyo na ulazima.
Sambamba na hayo amewataka maafisa ugani kuitumia vizuri taaluma yao katika kuwasaidia wakulima kufanya kilimo chenye tija.
Akihitimisha hotuba yake amewataka wananchi kuchagua viongozi madhubuti watakaowasaidia wananchi kupata maendeleo.
Maadhimishi ya Nanenane yamehudhuriwa na Viongozi mbalimbali pamoja na wadau wa maendeleo nchini.