Just Distinctions
JF-Expert Member
- May 5, 2016
- 3,230
- 6,742
Daluga ni njumu
Duh huyu cheche ana undugu na popobawa nini?[emoji1]Chitola - chuma ulete
Matamba- ugali wa muhogo
Songola - bania chenji chenji baada ya kutumwa,au ombea kitu pate kwa bei ya chini alafu ile iliyobaki unaiweka takoni hiyo ndo tunaita songola.
Cheche- mwanaume anaekula wanaume au wanawake kwa njia ya miujiza,usiku au mchana.
Hizi ni terminologues za LINDI HUKO.
Dah hili neno chimbuko lake hata sijui ila linamaanisha...alama ya mshangao tu kama vile "asalalee"kudadeki
Ngori = ndialala = lonzero = taabu = kali. Haya maneno hutumiwa Kenya jinsi Tanzania wanavyotumia neno shida ama sheeda.Kutokana na lugha kuzidi kukua na ndivyo misamiati inavyozidi kuongezeka, hivyo utajikuta kuna baadhi ya maneno huelewi kabisa japo yanatamkwa na wazungumzaji wa kiswahili, hii ni kwa wakenya je ni neno gani la "kibongo" unalisikia tu ama kwenye nyimbo au kuliona kwenye mitandao ila hulielewi? Post hapa wabongo wakufafanulie
Mimi kwa upande wa kenya, kuna baadhi ya maneno siyaelewi mf. Ngori, nduthi...yafafanueni tafadhali....
Sent using Jamii Forums mobile app
Lugha inatakiwa iwaunganishe watu lakini kwa EA ni tofauti.Ni vigumu sana kuratibu Kiswahili ukanda wote wa EAC, kwa mfano kule Pemba na hata Unguja nilkutana na misamiati ambayo sijaisikia Dar wala Nairobi, halafu pia kuna kisiwa kinaitwa Tumbatu, huko tulienda na Watanzania wa kutokea Dar ambao waliishia kushangaa shangaa misamiati iliyokua inatumika, hao watu wa Tumbatu walikua kila wakiongea wenyewe kwa wenyewe tunaishia kutoelewa chochote japo wanazungumza Kiswahili.
Wao wanaita lahaja ya Kitumbatu, halafu wale hawaruhusu dada zao kuolewa nje ya hicho kisiwa. Na pia hawaruhusu mtu asiye wa asili ya pale kununua kiwanja humo hata kama una pesa ngapi, hamna klabu wala pombe inayoruhusiwa pale, na zaidi hairuhusiwi dini nyingine yoyote nje ya uislamu. Wao wapo na maisha yao wanavyotaka yaendeshwe japo wanajiita Wanzazibari au Watanzania lakini hawatengamani
Kila mgeni ukiingia hicho kisiwa lazima upokelewe na sheha yaani mkuu wa shehia, ifahamike ulichokusudia kufanya na kwa muda gani na utageuza saa ngapi na lazima iwe hiyo hiyo siku uliyofikia, maana hamna gesti, haziruhusiwi, pia hawaruhusu watalii, kilichotupeleka kule kilikua mradi wa asasi ya huduma za kijamii na tuligeuza jioni moja kwa moja.
Matamshi huathiriwa na mahali mtu amezaliwa.mimi hushangaa vile waBongo hutamka L karibu kama R
Chibudi chibudeChitola - chuma ulete
Matamba- ugali wa muhogo
Songola - bania chenji chenji baada ya kutumwa,au ombea kitu pate kwa bei ya chini alafu ile iliyobaki unaiweka takoni hiyo ndo tunaita songola.
Cheche- mwanaume anaekula wanaume au wanawake kwa njia ya miujiza,usiku au mchana.
Hizi ni terminologues za LINDI HUKO.
Lugha inatakiwa iwaunganishe watu lakini kwa EA ni tofauti.
Nilikua naangalia Churchill Show, kuna mwanamke hua kama mwalimu mara nyingi segment yake nilikua siwezi elewa kitu na nilikua na uhakika pale ni anazungumza kiswahili.
Usiwaze, yaweke hapa wajuzi wakusaidieManeno mengi ya kibongo huwa yananipiga chenga kuandika na kuzungumza.