Filipo Lubua
JF-Expert Member
- Nov 18, 2011
- 339
- 578
NENO GANI?
Malenga nawaamsha, asubuhi na mapema
Ndoto imenigutusha, mimi sikulala jama
Malaika wa kutisha, ndotoni kanitutuma
Kanifumba fumbo gumu, sikweza kulitanzua
Kaniambia Lubua, hima unipe jawabu
Jibule sikulijua, nikalia kwa aibu
Nambyeni kama mwajua, neno moja ndo jawabu
Neno tata neno gani, laleta tabu dunyani
Malenga nifumbueni, mwenzenu raha sipati
Neno hili neno gani, lasababisha mauti
Neno hili litajeni, msipoteze wakati
Neno hili neno gani, liletalo tafurani
Neno la herufi saba, mtaani lasulubu
Limewatesa wababa, halijaacha mababu
Ya kale yake nasaba, watu wengi lawaadhibu
Neno hili neno gani, liletalo tafurani
Nilipokuwa mdogo, mamangu alinusia
Ni kali kama mbogo, watu wengi limeua
Limekuwa ni mtego, lanasa wasojijua
Neno hili neno gani, tegueni nifahamu
Bado mnajiuliza, tegueni tendawili
Ni hatari nawajuza, ili mwende kwa akili
Laleta mauzauza, si refu kama ukili
Neno hili neno gani, nambieni nifahamu
Silabi zake ni tatu, latesa hasa vijana
Rafiki yake ni chatu, ameza baba na wana
Msiseme kwa ubutu, fafanueni bayana
Neno hili neno gani, litujazalo majonzi
Rafikiye kisirani, nisemacho si uzushi
Atakweka majonzini, akumalize ubishi
Akutupe kaburini, uwe mwisho wa kuishi
Neno hili neno gani, tegueni mnijuvye
Hili neno la zamani, tangu enzi za wahenga
Kwa wivu limeshekheni, naweleza bila chenga
Lawatia wazimuni, laleta mengi matanga
Neno hili neno gani, tegweni kitendawili
Sielezei zaidi, wa busara tegueni
Mkisubiri zaidi, mwenzenu ntakufeni
Malaika kaniradidi, jibule ni shartini
Neno hili neno gani, kitendawili tegweni
© Filipo Lubua, 24 Novemba 2013
Malenga nawaamsha, asubuhi na mapema
Ndoto imenigutusha, mimi sikulala jama
Malaika wa kutisha, ndotoni kanitutuma
Kanifumba fumbo gumu, sikweza kulitanzua
Kaniambia Lubua, hima unipe jawabu
Jibule sikulijua, nikalia kwa aibu
Nambyeni kama mwajua, neno moja ndo jawabu
Neno tata neno gani, laleta tabu dunyani
Malenga nifumbueni, mwenzenu raha sipati
Neno hili neno gani, lasababisha mauti
Neno hili litajeni, msipoteze wakati
Neno hili neno gani, liletalo tafurani
Neno la herufi saba, mtaani lasulubu
Limewatesa wababa, halijaacha mababu
Ya kale yake nasaba, watu wengi lawaadhibu
Neno hili neno gani, liletalo tafurani
Nilipokuwa mdogo, mamangu alinusia
Ni kali kama mbogo, watu wengi limeua
Limekuwa ni mtego, lanasa wasojijua
Neno hili neno gani, tegueni nifahamu
Bado mnajiuliza, tegueni tendawili
Ni hatari nawajuza, ili mwende kwa akili
Laleta mauzauza, si refu kama ukili
Neno hili neno gani, nambieni nifahamu
Silabi zake ni tatu, latesa hasa vijana
Rafiki yake ni chatu, ameza baba na wana
Msiseme kwa ubutu, fafanueni bayana
Neno hili neno gani, litujazalo majonzi
Rafikiye kisirani, nisemacho si uzushi
Atakweka majonzini, akumalize ubishi
Akutupe kaburini, uwe mwisho wa kuishi
Neno hili neno gani, tegueni mnijuvye
Hili neno la zamani, tangu enzi za wahenga
Kwa wivu limeshekheni, naweleza bila chenga
Lawatia wazimuni, laleta mengi matanga
Neno hili neno gani, tegweni kitendawili
Sielezei zaidi, wa busara tegueni
Mkisubiri zaidi, mwenzenu ntakufeni
Malaika kaniradidi, jibule ni shartini
Neno hili neno gani, kitendawili tegweni
© Filipo Lubua, 24 Novemba 2013