Neno RAHISI la kiswahili linalosumbua watu wengi.

tpaul

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
24,225
Reaction score
22,632
Mnazijua PEMBE ZA NDOVU? Ndovu (tembo) hana PEMBE kama watu wengi wanavyodhani. Majangili huwinda tembo kwa ajili ya kupata vipusa ambavyo huviuza, hasa ktk nchi za mashariki ya mbali. Vipusa hivi ndivyo huitwa MENO YA NDOVU. Hizi sio PEMBE kama watu wengi wanavyodhani. Haya ni MENO (canine teeth); na hata ukimuangalia vizuri tembo utaona kwamba meno yale huchomoza kutoka mashavuni mwake--sio kichwani--ambako pembe huota.
Habari ndiyo hiyo.
 
umetisha, safi sana kutupiamo mara moja moja kama hivi...
 

Inaonekana wewe ni mjuzi wa Kiswahili. Kuna hii phrase naisikia watu wakiitamka lakini sijui kama ni Kiswahili ama lugha nyingine
"TUKITU TUDOGO TUDOGO".
Naomba unihabarishe.
 



Hayo ya mdomoni mwa tembo utayaitaje?
 
Inaonekana wewe ni mjuzi wa Kiswahili. Kuna hii phrase naisikia watu wakiitamka lakini sijui kama ni Kiswahili ama lugha nyingine
"TUKITU TUDOGO TUDOGO".
Naomba unihabarishe.

mkuu hicho ni kiswahili cha mtaani--sio rasmi wala sanifu.
 
Kwa maelezo hayo...ni sahihi kabisa kuziita PEMBE za Ndovu na si meno ya Ndovu...na Vipusa vya Kifaru
 
Zile ni pembe sio meno
Meno ya ndovu (tembo) yamo mdomoni na ndio anayotafunia
 
yale sio meno ya kutafunia bali ni meno ya pembeni (canine teeth) ambayo hutumika kwa kuchania au kupasulia chakula (teeth for tearing and/or crushing food)
 
From wildlife point of view
Yale ni meno ya tembo/ndovu

Bazazi
 
Nadhani huu ufunuo uliupata aidha baada ya kupiga msuba au kiroba kwa mkupuo. Ingelikuwa sio Sheriff Arpaio ulikuwa tayari umeshanichanganya akili aisee!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…