New administration under Samia Suluhu gives hope after 5 years of hopelessness

THE APPOINTMENT OF PROFESSOR MKUMBO TO THE CABINET SIGNALS MADAM PRESIDENT IS DIGGING IN FOR A FIGHT OF HER CAREER!


Prof. Mkumbo is one of the ardent supporters of the DP WORLD IGA that has doled out prime assets to the Dubai sheikhs for a song.


We deem his appointment to the cabinet not only a scurrilous affront to an amicable resolution of not only the auctioning off of our sovereignty to the lowest bidder but also Madam President is preparing to push back on any attempt to derail her from her objectives which perspire to disowning Tanganyikans from their God given blessing [emoji119].

As she is mapping out her career survival which is looking grim by every passing second, she has figured out she needs a bulldog at the planning ministry but the learned Don is bereft of ideas, notorious for deceit and has little influence to flip the narratives


No matter what Madam President does, her case is open and shut, not only here but also in heaven, says the Lord God of Israel.

That the scripture may be fulfilled:

WHOEVER COVERS HER SIN SHALL NOT PROSPER BUT WHO CONFESSES AND FORSAKE IT SHALL HAVE MERCY. - Proverbs 28:13.


Rewarding mediocrity to cover her tracks is equivalent to pouring petrol to inflame an already conflagration.


It is in humility not justifying the unjustifiable we know God lives in our hearts

For God abhors the proud but exalts the humble. - James 4:6
 
THE CREATION OF A NEW MINISTRY OF PLANNING REWARDS CRONIES BUT ALSO IS A CLOSET ACKNOWLEDGEMENT THE DP WORLD SELLOUT IS A HUGE MESS!

As Madam President fights for her political lifeline, which now hangs in a cliffhanger, she has opted to burden taxpayers with more mouths to feed in the cabinet!

As her political fortunes dwindle, she is confining herself in her "comfort zone" which is to burgeoning the cabinet with minions who will tell her what she wants to hear: our titanic ship is the safest ship in the world until it capsizes. These are signatures of a very insecure, troubled, and low self esteemed individual who is now clinging to a facade of loyalty to hang onto power.

Apart from that, we read Madam President has unambiguously conceded the whole DP WORLD is a quagmire that may bring down her government if not handled properly.

The alacrity with which she has carried out this minor reshuffle is another red flag that she is ferreting her way out of that scandal ridden DP WORLD heist sooner than later. But she has run out of options except to grandstanding in a forlorn hope adrenaline sapping fatigue shall wear us down, and she will prevail against all odds!


Politics being a game of perception to garner numbers, we wonder whether she is really that super chess grandmaster we once thought she was.


An appointment of Professor Mkumbo, whose deceptive views on the DP WORLD nightmares are passim, we know he does not care about us but his own belly. Always, a bellyworshipper flees to nowhere, but in a dungeon lest no man bails him out, says the Lord, God of Jacob. - Proverbs 27:18.


The learned Don always trumpets anything the regime says so the question we need to ponder is this the right moment to surround herself with the "yea men" or discard them and put a team which will tell her the gospel truth no matter how bitter it is?


History is replete with regimes, which are arrogant, proud, and recalcitrant whose end was terrible. We also read the same scripted clichés unfolding here.

We thought it was time to part ways with the inept Mwigulu Nchemba, but when the tyres are falling off from the hurtling bus she is driving, she retains him albeit with clipped wings, but for what?

Well, as we have expounded before, this is a Titanic ship as the original one was that the sailors and their dawdling captain are totally oblivious of, that the ship has already hit an iceberg festooned with very whetted icicles.

The marauding waters pouring in will ultimately sink her titanic ship, and whatever she does now seemly to hasten her own downfall, and the clock keeps chiming the seconds away from her fateful denouement


What she needs is fresh blood emboldened with new ideas amounting to thinking out of the box. She has made her choices abundantly crystal clear: she is not going to lift the stylus from a defective recording that keeps playing the same old tune again and again in her pawned gramophone!

Fatigue and dethroning of our own constitution she had sworn to uphold are now aligning booby traps to blow up her political gamble that has already backfired before our very own eyes that the scripture may be fulfilled that says:-

ONLY WITH OUR EYES SHALL WE BEHOLD AND WITNESS THE REWARD OF THE WICKED. Psalm 91: 8-12.



 



We project NDC, TIB and NAFCO will soon be privatized with Dubai sheikhs very much on the thick and thin of procuring them for a song!

The biggest disadvantage of privatization is neocolonialism that impoverish the majority regressing all the gigantic steps we took to gain our independence.

Any serious leader will seek public debate on how to deal with problems of misnamagement in our public sector but rewinding Nyerere nationalisation policies that are widely accredited for the peace and tranquility in this country is colossal error of judgment.


The real reason to seek our independence was self governance with major means of economy very much in our hands.

Turning back the clock, and declaring sixty years or so of independence we have failed, and now to relinquish our bread to aliens will come at astronomical costs to national security.

Handing over major means of the economy will lead to social unrest, and increased crime.
 
Kama waislamu wa Somaliland na Djibouti wamewakataa waislamu wenzao DUBAI PORTS WORLD sisi tunakhoja gani ya kuwakumbatia?

Hata Somaliland na umasikini wao wa kutupwa wamesema haitaki ujinga hivi huu upumbavu wa kuingia mikataba ya kipuuzi na kiuhaini namna hii hamjui ni malipo ya wizi uliokithiri wa kura wa 2020


Kuhani wenu mkuu alipigwa chini sasa zamu yenu imewadia.


Mnafikiri Mwenyezi Mungu kasahu la hasha Aliwapa muda wa kutosha mjutie dhambi zenu za wizi wa kura mkagoma sasa imekula kwenu.


Nawahakikishia kwa Jina la Yesu Kristu Mungu wangu pekee Aliyehai siku za CCM kuwa madarakani zimehesabiwa mbinguni na kuonekana hazitoshi na nguvu ya wananchi itawaondoa madarakani.


Hakikisheni mmenunua nyumba Dubai maana Tanganyika hamtaruhusiwa na Mwenyezi Mungu kuwa na makaazi asema BWANA wa Majeshi

 
Ufunuo niloupata sasa hivi huu ni mpango wa Mwenyezi Mungu kuwaondoa CCM madarakani

BYE BYE CCM


Laana ya kuiba kura inawatafuna haponi mtu nyote mnakwenda asema BWANA wa Majeshi

Shukrani sana Yesu Kristu Mungu wangu pekee Aliyehai kwa uaminifu wako na haki Yako yote kwa wale wote wanaokusujudia, kukuabudu na kukutumikia wewe tu ndiye Mwenyezi Mungu na wengineo ni viumbe vyako. Asema BWANA wa Majeshi [emoji120] [emoji120] [emoji120]
 
Malkia wenu Athalia kumekuchaaaaa


Game over! Tulisema kwa Mwendazake sasa tunasema tena game over asema BWANA wa Majeshi.





 
Huwezi eti mimi ni Rais nani alikuchagua?

Ulipata kura ngapi?

Ni nani alizohesabu hizo kura?

Vituo vingapi mawakala wa upinzani walikuwepo na kusaini fomu husika?

Huna uhalali wowote wa kuongoza nchi hii na ndiyo maana umebakia kujimilikisha njia kuu za uchumi wa watanganyika.

Nina kuhakikisha kwa Jina la Yesu Kristu Mungu wangu pekee Aliyehai hutoboi na hao waarabu wako.

JK unayemwabudu atakutangulia kwenye mlango wa hukumu ukisikia kalazwa hospitalini ujue hilo gonjwa halitamwacha salama


Hakikisha unamuaga maana ni wewe umepewa kazi ya kutujuza ratiba ya mazishi yake


Hii nchi ina Mwenyezi Mungu ni nchi takatifu na hata Nyerere mwasisi wa hili taifa anaomba nyote muangamie. Tubu achana na tamaa ridhika na Mwenyezi Mungu alichokupa utaheshimiwa vizazi na vizazi vijavyo.

Hela ni mazingaombwe tu hazikupeleki mahali bali zitakuletea laana kwako na uzao wako uupendao
 
WEZI WA KURA HAWANA UWEZO WA KUSIMAMIA UCHUMI WA NCHI HII!

Tatizo la bandari na maeneo yote ya uchumi yanathibitisha walioshindwa kuusimamia uchumi wetu ni zao la kuiba kura siyo sisi watanzania tulioshindwa.

Mfumo uliomo kwenye katiba na sheria zetu ndiyo umekwama sasa badala ya kuliona hilo wezi wa kura wanakimbilia kumtafuta mchawi.


Sokoine alikuwa akiongea nchi inatetemeka kwa sababu Mungu alikuwa na yeye. Huwezi ukawa mwizi wa kura khalafu ujitutumue kuzuia wizi ulioshamiri sekta ya umma nchi nzima.

Ni nani serikalini akiongea kuna mtu atamsikiliza? Hakuna! Kwa nini? Kwa sababu huwezi kuhimiza maadili mema unapoona inalipa kwako na kuyasigina pale unaona yatakuachia maumivu makali.

Inabidi uyathamini maadili mema nyakati zote ndipo utakuwa mfano wa kuigwa.

Kutatua matatizo ya kiuchumi ya nchi lazima tuanze na kukiri watanzania hatushindwi lolote bali mfumo huu tuliothiri kutoka kwa wakoloni ndiyo umeshindwa kuhimili mahitaji mapya na matarajio ya jamii.

Nchi hii itatawaliwa na watanzania wenyewe na kujitawala kunaanza na kuzisimamia njia kuu za uchumi hakuna namna nyingine tutajitawala kama wageni tutawakabidhi njia za uchumi. Huko ni kupalilia machafuko na lazima yatatutembelea tu.

Tujiulize ni wapi tumegota?

Hilo ndilo swali la msingi kabisa la kuanza nalo.

Katiba mbovu huzaa watawala dhaifu na hivyo kupelekea usimamizi duni wa uchumi. Na hili ndilo tatizo letu tangu tupate uhuru.

Mchumi Enos Bukuku aliwahi kuandika kitabu kinachoitwa "Tanzania Economy is Being Managed by Incompetent Minds" wangapi wamekisoma? Nauliza tena wangapi? Kitafuteni mkakisome.

Kikubwa kwenye hicho kitabu ni kuwa mfumo mbovu tulionao umezaa uongozi duni. Lakini siyo yeye tu hata Nyerere aliliona hilo pale aliposema ili kuendelea tunahitaji vitu vinne: watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora. Alisema vyote tunavyo lakini tunachokosa ni uongozi bora.

Sasa tatizo letu siyo watanzania tumeshindwa kujiamulia mambo yetu wenyewe la hasha bali mfumo tulionao umeshindwa kuzalisha viongozi bora na kinachoendelea ni bora uongozi badala ya uongozi bora.

Kwenye mfumo wa uwajibikaji hii serikali haina sifa ya kuongoza nchi hii. Hawana maadili maana ni zao la wizi wa kura. Na bila maadili huwezi kuhimiza maadili au kuwa mbunifu wa kuunda mifumo ya kuibua vipaji vya uongozi bora.


Kwa hiyo, viongozi tulionao ni tunda la wizi wa kura halina sifa la kuusimamia uchumi wa nchi hii.

Matatizo ya uendeshaji na usimamizi wa rasimali wa nchi hii haupo salama hadi pale tutakapokubali kuachana na mfumo unaozalisha uwakilishi haramu.

Huwezi ukaiba kura ukaapa kiapo cha uongo halafu ukatoka hapo ukakemea maovu kwenye jamii hakuna atakayekusikiliza. Unaowakemea wanajua undani wako sasa utawaambia nini.


Tunachosema inabidi sisi tukiri tubadilishe mfumo unaozaa uwakilishi haramu tuwe na viongozi waliotokana na nguvu ya umma halafu tujadiliane nini cha kufanya kuiokoa sekta ya umma ambayo sasa inatafunwa usiku na mchana.

Kwa mfano, swali la kujiuliza katika hii karne ya 21 tuna sababu yoyote ile ya Bodi za wakurugenzi na wenyeviti wa Bodi kuteuliwa na Rais au Waziri? Kuna uhaja kweli wa waziri au mtendaji wa taasisi yoyote ile ya umma kuteua Bodi za zabuni?

Wako wapi wadau wa sekta hizo? Kwa mfano mifuko ya pensheni Rais na Waziri wake wanayo sababu ya kuteua mtendaji mkuu na bodi za wakurugenzi wakati wao siyo wanachama wa hiyo mifuko? Wana uchungu gani hata wa kuilinda hiyo mifuko ili iwanufaishe wafanyakazi waliokuwa wakiichangia?

Wako wapi wanachama wa mifuko hiyo katika kusimamia michango yao kwenye Bodi za wakurugenzi na uteuzi wa menejimenti ya usimamizi wa mifuko? Huu ni mjadala tunaohitaji nchi hii.

Ukiangalia bandari tatizo ni mamlaka makubwa ya Rais na Waziri wa uchukuzi katika uteuzi wa menejimenti na Bodi ya wakurugenzi ndiko tatizo lilipo. Wadau wakuu wanaoathirika na utendaji mzima wa bandari hawapo kwenye nafasi za maamuzi na ndiyo maana wasiyo na sifa wamefurika katika mamlaka ya usimamizi wa bandari zetu.


Kwa hiyo, badala ya kumleta mwarabu na kusababisha machafuko nchini tujiulize wadau wakuu wa bandari ni akina nani? Maakuli, mawakala, walaji, wafanyakazi, wanasheria, wahandisi, wahasibu n.k

Kazi ya kwanza ni kuwatambua wadau na kuwapa mamlaka ya kuwachagua wawakilishi wao kwenye hizo Bodi za wakurugenzi wakasimamie ajira na nidhamu za watendaji wote wa taasisi hizo halafu tuone tunaelekea wapi.

Rais na waziri wazuiwe kuteua watendaji wa taasisi zote za kiuchumi za nchi hii na waziri akomeshwe kuteua wajumbe wa Bodi na kazi hiyo ifanywe na wawakilishi wa wadau ambao nao ni mjadala wa kisekta kwa sekta.

Lazima wadau wa kila sekta wakubaliane juu ya ni nani ni wadau wa shirika la umma husika na sheria zibadilishwe kuwapa mamlaka kamili wadau wayasimamie mashirika ya umma.

Tunarudia kilichoshindwa ni mfumo huu wa Rais ndiye anateua kila mtu na kuwajaza makada wa CCM kuusimamia uchumi wa nchi hii wakati hawana maadili, uwezo na hata ujuzi kwenye baadhi ya maeneo.

Mfano, utakuta mtu kaharibu mfuko wa pensheni ya PPF anahamishiwa ATC sasa ana ujuzi gani wa kuwa mtendaji mkuu wa shirika la ndege na yeye hana hata mapenzi na hiyo taaluma ni dhahiri kapelekwa huko akale sasa akila mnasena TUMESHINDWA!!!!!


Aliyeshindwa ni yule anayetegemea wizi wa kura kubaki madarakani huyo ndiye kashindwa na ni vyema sasa akajipima kabla jamii haijampima akaachia ngazi na kutupisha wenye uwezo tuwawezeshe wadau katika kila sekta halafu muone na kuusikilizia muziki wake.
 
UKOLONI UNARUDI TANZANIA?

Na Thadei Ole Mushi.

Miaka 60 ya Uhuru tumeshindwa kabisa kusimamia rasilimali zetu wenyewe.

Migodi tumeitoa kwa Wazungu, Misitu tumeitoa kwa Mwarabu, Posta tumeitoa kwa Mwarabu, Misitu tumeitoa kwa mwarabu, Gesi tumeitoa kwa Mzungu, Uwanja wa ndege wa KIA nao tumeutoa, TPDC tumeitoa, Bandari tumeitoa kwa mwarabu, Loliondo tumeitoa kwa Mwarabu, karibi maeneo yote Muhimu tumeshatoa…. Sisi tumebakia na nini?

Maswali ni Mengi mno….

1. Tulidai Uhuru wa Nini?

2. CCM imeshindwa kuiongoza Nchi? Maana kila eneo tuliloliwekeza tunasema kuna wapigaji hivyo bora tumpe mwekezaji. Je Serikali ni dhaifu imeshindwa kuzuia upigaji?

3. Vyuo Vikuu zaidi ya 31 nchini vimeshindwa kutengeneza wasomi wa kusimamia hizi rasilimali za taifa? Kazi za Graduate wetu kubwa ni kuendesha Bodaboda, kama taifa tunajua tunakoelekea?

4. Tanzania tunaweza jambo gani kubwa hapa nchini? Mambo yote ya muhimu tunaona ni Magumu tunawapa wawekezaji je sisi ni kitu gani tunaweza? Wenzetu wanawezaje sisi tunashindwa? Huu uvivu wa kufikiri tumeutoa wapi?

5. Baada ya Bandari tunaenda kuwekeza rasilimali gani tena? Ukiona wabunge wetu wanavyovaa Suti Pale Bungeni na taifa linapoelekea utatamani kulia. Hawa watu (wabunge) tunawalipa mishahara, tunawanunulia mafuta ya magari, watoto wao tunawasomesha na bado wanatuibia kupitia mikataba hivi nani alituloga tukawa waoga hivi?

6. Tanzania ya watu Milioni 69 plus tumeshindwa kuchaguana miongoni mwetu tupate watu wanaoweza kutuvusha hapa tulipo kwa kuwa taifa linaelekea kutawaliwa kwa mara ya Pili?

7. Wakati Uganda ilipogundua kuwa ni kweli Taifa lao lina mafuta walichukua vijana wao wakakimbiziwa ughaibuni kwenda kujifunza kuhusu Oil Production na asilimia kubwa ya mradi wao wa mafuta ni vijana wanausimamia. Sisi badala ya kuandaa vijana tunatuma kina Steve Nyerere na kina Kitenge kwenda kukagua Bandari za wenzetu hivi nani alituloga?

8. Vijana asilimia 90 sasa hivi hapa nchini bila kujali elimu zao kazi zao kubwa za kujipatia kipato ni Kubet au kuendesha Bodaboda. Huku maeneo muhimu ya rasilimali za taifa lao zikigawanywa kwa wazungu na waarabu kwa jina la kusema ni mwekezaji. Hii ni hatari sana kwa taifa letu…. Tanzania ina wanyamapori kila mahali ila anayekula nyama pori first class kabisa hapa Tanzania ni Mwarabu hii ni aibu…

9. Je tuliwahi kupata Uhuru? Lakini mbona Kina Singapore walipata Uhuru nyuma yetu? Mbona leo ipo mbali sana na wanajisimamia wenyewe?

10. Hata kuzalisha mafuta ya kula ya kutosha kwa taifa zima tumeshindwa tunaagiza nje ya nchi, Ngano tunaagiza, Mbolea tunaagiza, Maziwa ya Unga na hata ya kawaidia tunaagiza, pale Bandarini asilimia 95 ni bidhaa zinaingia nchini badala ya kutoka hivi tunaelekea wapi?

CCM ikubali sasa kutumia watu ambao wapo nje ya familia zenye Connection kwenye Uongozi wa nchi hii. Babu alikuwa kiongozi, mtoto akatafutiwa connection akawa kiongozi, mjukuu naye akawa kiongozi nk …. Hizi DNA kwa mazingira ya Sasa zimechoka au CCM ikubali kuwaachia wengine wajaribu kutusogeza tulipo.

Kuna siku nilisema kama Africa itaheshimu Sanduku la Kura katika kuchaguana tutafika mbali sana. Na kama askari polisi wa Mataifa ya Africa watatimiza wajibu wao kwa mujibu wa Sheria hili bara linapiga hatua kubwa. Askari anamlinda mtu mwenye V8, Mke ana gari, watoto wa huyo Mtu wanachukuliwa na School Bus wanakupita getini unawachekelea kama Zuzu, huku kwako ukiwa unafukuzana na Baba Mwenye nyumba anakudai kodi, kijana wako wa kwanza aliyehitimu Chuo kikuu anashinda vibanda umiza anabet, wanao wanasoma shule za makabwela kabisa huku akiwa hana uniform za kubadilisha lakini bado unaendelea kupiga Salute kwenye mageti ya viongozi.

Vijana kwa Rasilimali zilizopo hapa nchini hampaswi kukesha mkiwa mna Bet na kuendesha Boda boda. Wafanyakazi kwa rasilimali zilizopo Hampaswi kulipwa mishahara mnayolipwa. Hivyo basi watu kama kina Steve Nyerere na kina Maulid Kitenge ni wa kuwatenga kwenye jamii yetu…. Tunatakiwa tuanze kutokomeza hizi chawa kwanza kabla hatujawafikia Viongozi wetu.

Wakati ukoloni ukibisha Hodi Africa ulikuja kwa njia ya Mikataba. Ndiko tunakoelekea…..

Vijana tuliopo ndani ya CCM ni wakati wa kujitafuta sasa tuache kusifia ujinga wakati taifa limekwama. Tuzungumze, tukatae kabisa kuwa Chawa wa mtu, wakati ni sasa….. kila mtu kwenye familia yake atoe elimu ya Uraia.

Tumekwama kama Taifa….. share

Ole Mushi
0712702602
 
KWANINI TUNASEMA PROFESA MBARAWA NI LAGHAI?


Profesa Mbarawa kwa kunuia kabisa aliongopa bungeni kukadiria mapato ya miaka 10 ijayo ambayo anajua ni hewa kwa sababu zifuatazo:-

1) Anajua hatakuwepo kuwajibika kwa kulipotosha bunge na hivyo alichochewa kutamka matrilioni ambayo hakutoa hata kigezo kimoja alifikiaje hiyo tathmini.


2) Hakutofautisha kati ya mapato ya kodi yanayokusanywa na TRA na naksi ya uendeshaji wa shughuli za bandari zetu na hivyo kujipatia mwanya wa kuchanganya vyanzo viwili vya mapato ambavyo viko chini ya mamlaka mbili tofauti na sheria mbili tofauti!.

3) Hakutoa mchango wa mfumuko wa bei (inflation) katika matrilioni aliyoyatamka kwa kila mwaka kwa kipindi cha miaka 10 ijayo.

4) Alipaswa kutoa mchanganuo wa kila mwaka wa mapato serikali itapata kwa shughuli za uendeshaji wa bandari kwa miaka 10 ijayo. Kutotoa takwimu tajwa inakuwa vigumu kuhakiki kila mwaka tangia DP WORLD wanakabidhiwa bandari zetu kama hata wana mwelekeo wa kufikia malengo ya miaka 10.

5) Alikwepa kutoa tathmini ya utendaji wa DP WORLD na hususani kwanini wametimuliwa Somaliland na Djibouti ili atuhakikishie changamoto zilizojitokeza kwenye uendeshaji wa bandari tajwa hazingejitokeza kwetu.

6)Alishindwa kutoa maoni yake kwanini DubaiTainer wanaoendesha bandari ya Wilmington ya jimbo la Delaware anatoka Rais wa Marekani Joe Biden haijawahi kuchangia bajeti ya jimbo hili pamoja na kukabidhiwa kuiendesha bandari tajwa kwa zaidi ya miaka 5 sasa.

Ikumbukwe mzigo unaopitia bandari ta Wilmington ni takribani tani milioni 6. 6 wakati bandari ya Dar-es-Salaam ni takribani tani milioni 14.3 [2016]. Kampuni hiyo binafsi inaendeshwa kwa hasara hata kupewa ruzuku ya dola milioni 6 kila mwaka


7) Kuna uwekezaji wa mkopo wa Benki ya dunia ambao Tanzania iliupata na ulilenga kuongeza ufanisi na mapato chini ya TPA. Profesa Mbarawa hakutoa mchanganuo wa ulinganishi wa kipindi hicho hicho cha miaka 10 TPA mapato yake yangelikuwaje. Kukwepa kuongelea uwekezaji tajwa ambao utaiongezea bandari ya Dar-es-Salaam uwezo wa kushusha magari zaidi ya mara mbili na nusu hivi na kuongeza mapato ya serikali. Mchanganuo wa profesa Mbarawa kwa kutuficha hizi takwimu alilenga kulipotosha bunge ili kuonyesha matrilioni aliyoyataja hayahusiani na upanuzi wa bandari kwa mkopo wa Benki ya dunia wa dola milioni 421 hivi.



8) Kulinganisha TICTS na DP WORLD siyo sahihi kwa sababu TICTS walipewa geti namba 8-11 ambazo hazina mapato wakati DP WORLD wamepewa geti namba 1-7 zenye mapato ya zaidi ya 90% ya mapato yote ya bandari ya Dar-es-Salaam.


9) Mkakati wa serikali ni kuijengea TPA mazingira ife (natural death) kwa kuipora geti namba 1-7 ambazo zinaingiza zaidi ya 90% mapato yote ya bandari.

10) Profesa Mbarawa alilificha bunge ukweli ya kuwa baada ya ujio wa DP WORLD TPA mapato yake yatashuka kwa 90% na hivyo itashindwa kuwalipa mishahara wafanyakazi wake takribani 2, 600. Hivyo, khoja ya profesa Mbarawa ajira zitaongezeka kuwa ni ulaghai usiyo na kifani hasa ukizingatia DP WORLD kwa kufunga mitambo hawatawaajiri wafanyakazi watakaokuwa wameachishwa kazi na TPA kwa sababu haitawahitaji.








 
Lilongwe - Malawi. Nakala ya Kwanza ya Kitabu Kipya Cha Hayati Rais Magufuli Kama kilivyoandikwa na Profesa wa Chuo kikuu Cha Hebron Nchini Malawi Prof Malango Chinthenga kimeuzwa kwa USD 600 sawa na Tsh 1,450,000/= kwa Mwananchi wa Kawaida wa Malawi ambaye alijitokeza katika Uzinduzi wa Kitabu hicho jijini Lilongwe, Kitabu hicho chenye kurasa 461 na Chapter zipatazo 48 kimeanza kuwa Gumzo Kubwa Barani Afrika Kitabu kinaitwa "AFRICA MAGUFULI AND CHANGE" an integrated Approach in abolishing Africa's modern economic Slavery", kwa tafisiri isiyo Rasmi Ni "AFRIKA MAGUFULI NA MABADILIKO" Namna, Njia ya Kutokomeza Utumwa wa Kisasa wa Afrika Kiuchumi" Mgeni Rasmi katika Uzinduzi wa Kitabu Hicho jijini Lilongwe Dr Grace Kumchulesi ambaye Ni Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Mipango ya Maendeleo ya Serikali ya Malawi anasema:[emoji116] "Kutokea Hapa Malawi tutajitahidi kusambaza Kitabu Hiki katika Vyuo vyetu Vyote kwa ajili ya Vijana wetu Kujifunza Nini Maana ya Uongozi na Ukombozi wa Bara la Afrika kutoka katika Ukoloni



 
Ukiona wanaamini nchi imeuzwa hata kama haijauzwa ni vyema kujitoa kwenye huu mkataba kwa sababu huko mbele mabaya yanakuja kwetu sote hakuna atakayekwepa.


Uwekezaji ambao una mapepo kama huu HAUTUFAI. Roho zetu zina thamani kuliko utajiri kulikoni lolote lile.
 
Unapoona sheria za nchi hazitumiki kwenye usimamizi wa mali za umma bali sheria za mkoloni ndizo zinatumika ujue huna sababu ya kuunga mkono labda tu kama tunakiri hatuko tayari kujitawala.

Unapoona mikataba inasainiwa halafu vikao vinafuata kubariki ujue hakuna ushirikishwaji. Swali la kujiuliza kwanini usaini kwanza halafu urudi kuvitumia vikao kupitisha? Kwanini hukuuliza kwanza kabla ya kusaini? Mashinikizo ya kusaini kabla ya ushirikishwaji yanaashiria huu mkataba utakuja kutuumbua.

Wanaosema hili swala limfeikia tamati wawe na akiba ya maneno. Mahakama zetu bado zinalifanyia kazi tusubiri wataafiki na huu utaratibu uliotumika?

Misingi ya usawa, ushirikishwaji, nini nafasi ya sheria zetu katika kusimamia rasimali zetu n.k tusubiri mahakama zitoe msimamo.
 
TUONAVYO KUHUSU UUZWAJI WA BANDARI ZA NCHI HII.


1) Hatuhitaji uwekezaji kwenye eneo hili kwa sababu mtaji wake ni mdogo mno na upo ndani ya uwezo wetu.

Mtaji wa dola 600 milioni ni kichekesho kuwa ndiyo sababu ya kuwaita wawekezaji kutoka nje. Tunahitaji maelezo kwanini sisi wenyewe tusiwekeze hizo dola milioni 600 hasa ukizingatia tayari tumechukua mkopo wa dola milioni 420 wa benki ya dunia? Hata hatujaona matunda ya huo mkopo tuna kiherehere ya kusaka mwekezaji ili afaidike na huo mkopo kwa gharama yetu. Huu ni uzandiki kwa taifa hili.

Leo ukiwaambia watanzania unarudisha tozo ya miamala ili kupata mtaji wa kuwekeza kwenye bandari zetu chini ya taasisi ya umma tutaiunga mkono serikali kwa [emoji817] bila zengwe hata chembe.


2) Bandari za Tanzania lazima ziendelee kuwa mashirika ya umma na kusimamiwa na watanzania


3) Hoja za ufanisi na tija za kuhalalisha kuuza pande za nchi ni makosa ya jinai ya kiuhaini. Huu ni usaliti dhidi ya wananchi wa Tanzania.


Haiwezekani wewe mwanasiasa uwe na sifa ya kuwaongoza watanzania lakini watanzania hawana sifa ya kusimamia njia kuu za uchumi wa nchi.

Tutakapofika huko na hatutafika huko itabidi turudi UN tuseme tumeshindwa kujitawala.

Kama raia hatuna uwezo wa kuendesha kitu kidogo kama bandari sasa hapa duniani tunafanya nini?

Ni aibu kwa nchi yenye dhima ya kujitegemea inajisalimisha kwa mamluki kwa vipande thelathini vya fedha

4) Pamoja na mikataba kusainiwa na Bunge kupitisha maazimio ya kifisadi tunawahakikishia bandari zetu mwarabu kamwe hataziendesha.

Mtendaji Mkuu wa bandari zetu atakuwa raia wa Tanzania awe mwaminifu awe fisadi sisi hatujali lakini lazima awe raia na hao wakuja hawataruhusiwa kugusa bandari zetu.


Menejimenti ya Bandari zetu lazima [emoji817] iundwe na watanzania hata mgeni mmoja hataruhusiwa kuweka pua yake.


Tupo tayari kujadili maboresho ya miundombinu na uendeshaji wa bandari ili kuongeza ufanisi na tija chini ya taasisi hiyo kuwa [emoji817] mikononi mwa watanzania.

5) Kiongozi yoyote yule anayejidanganya ya kuwa nchi hii ni mali yake na anaweza kutuuza ili ale yeye na wapambe wake ajiandae kuachama kinywa kwa mshangao.


6) Urais siyo fursa ya kupora rasimali za nchi bali ni fursa ya kuwawezesha raia waliokupa dhamana waweze kusimamia urithi wa vizazi vijavyo.

7) Jiulizeni Nyerere angelikuwa mlafi kama hawa viwavi jeshi wangapi leo wangelikuwapo hapo walipo?


8) Tunaamini bila shaka yoyote kila ubinafsishaji uliofanyika hapa nchini ni wanasiasa wetu uchwara ambao wanapora mali ya umma kupitia mgongo wa wawekezaji kutoka nje.

Leo ukiwaambia watupe takwimu ya kila mwekezaji anatoa mchango gani kwenye bajeti ya kila mwaka ya serikali tutaanza kutafutana. Mchango wa wawekezaji wote waliopo na wanaokuja wanaiona nchi hii ni shamba la bibi lakini wanasiasa wamepofuliwa na ulafi wao hata kuwaona raia ndiyo tatizo la maendeleo ya nchi yao!!!!!!!

9) Hadi leo serikali imeshindwa kujibu hata hoja moja ni kwanini vinchi vibogoyo kama Djibouti na Somaliland wamevunja mikataba na DP WORLD na bado wao wanawakumbatia hawa wezi wa mali ya umma?

Djibouti na Somaliland wanasema hakuna uwekezaji uliofanyika kwa takribani miaka 5 na zaidi ya uwekezaji, hakuna ufanisi, mapato yameshuka sana na mbaya zaidi usalama wa mataifa yao umeporomoka. Wanajiona hawajui nini kinaingia na kutoka kwenye bandari zao.

10) Ukiona Rais mzima kiguu kwa njia na kwenda Dubai na kusaini mikataba inayodhalilisha utu wa mtanzania ambao msingi wake mkuu ni HAKI YA KUJITAWALA na Rais huyo anatengua misingi ya kikatiba ya usawa, ushindani na ushirikishwaji kwenye mchakato mzima wa kumpata mwekezaji basi ujue humo hakuna masilahi ya taifa bali ni masilahi binafsi ya Rais mhusika.

Masilahi ya taifa yatapatikana na kulindwa kwa kuheshimu katiba na sheria za nchi hii siyo kujisalimisha kwa sheria za mkoloni wa uingereza. Mwekezaji ambaye hana imani na sheria zetu hana sifa ya kuwekeza hapa nchini.


Kuna masilahi gani kuua shirika la umma kwa kiduchu cha dola milioni 600 wakati hata mkopo wa Benki ya dunia wa dola 420 milioni hatujaona matunda yake? Kwa lugha nyingine tumekopa siyo kwa manufaa yetu bali kwa manufaa ya mwekezaji feki. Mkopo tuulipe sisi lakini mgeni ale. Hii siyo maana ya mgeni njoo mwenyeji apone.

Hivi, wakati hawa wezi wa mali ya umma wanatulaghai ajira za TPA zitalindwa hawatuelezi ni kwa mapato yapi wakati 90% ya mapato yao wanampa askari wa mamluki. Hivi, TPA bila kuachisha kazi maelfu kwa maelfu ya wafanyakazi wake watatoa wapi hela ya kuwalipa wakati vyanzo vyao vya mapato wameporwa na hawa mafisadi wa CCM?

Ukiisha wapora TPA malango 1 hadi 7 ambako mizigo ya konteina hushuka na ndiyo inalipa na unawaachia TPA lango 8 hadi 11 asimamie boti za Azam kweli lengo si ni kulifuta shirika la umma lililokuwa linaendeshwa kwa faida?


Tunahitimisha kwa yafuatayo


1) Bandari zetu zitaendelea kusimamiwa na watanzania [emoji817] wawe waaminifu au wawe siyo waaminifu


2) Hoja za tija, ufanisi na uwekezaji zinazopigiwa upatu zinawezekana kufikiwa na taasisi ya umma kama tutaheshimu sheria zetu. Nje ya sheria zetu ni wizi na ubadhirifu ulioshamiri

3) Historia ya mwekezaji DP WORLD ni kuhonga viongozi kusaini mikataba ya kifisadi ambayo inawapa haki lukuki bila wajibu wowote ule kwa malengo ya kuibua migogoro ili kushinda kesi za mabilioni ya dola. Hawana mtazamo wa muda mrefu.


4) Uwakilishi haramu ndiyo umetufikisha hapa tulipo.


5) Wanasiasa wameshindwa kuusimamia uchumi wetu badala ya kukiri hawana ujuzi wala maarifa zaidi ya kukwapua kura na kujitangaza washindi wanakimbilia majibu mepesi kwa maswali magumu.

6) Hata wakifanikiwa kutudhalilisha utu wetu na kudai tumeshindwa hata kusimamia kitu kidogo kama bandari ndani ya miaka 2 baada ya hawa DP WORLD kuanza kazi ya uporaji wa maliasili zetu hawa hawa wanasiasa watauvunja huu mkataba na malengo yao ya kuhakikisha tunawalipa wawekezaji feki mabilioni ya dola yatakuwa yametimia ili wao wakatiwe mgao wao.


7) Chini ya CCM, wizi na ubadhirifu umechachamaa katika kila sekta ikimaanisha kama tukiongozwa na hoja zao za kukomesha nchi hii kuwa ni shamba la bibi basi itabidi maeneo yote wabinafsishe. Hii haitaishia mashirika ya umma bali pia serikali kuu na ya mitaa maana nako ni shamba la bibi.


Ikulu yenyewe ina tuhuma tosha za ufisadi sasa kama kigezo sisi tumeigeuza bandari kuwa shamba la bibi na mwekezaji ndiyo mwarobaini mbona hoja hizo hizo zinatosha kuibinafsisha ikulu?

Mbona kigugumizi kikali inapokuja khoja ya kuibinafsisha Ikulu?

Haiwezekani sisi huku mtaani tuonekane hatufai lakini watawala ambao waliapa kutusimamia waonekane wanafaa na wanaowasimamia hawafai. Aidha sote tunafaa au sote hatufai. Huwezi ukamung'unya mung'unya keki yako halafu bado udai iko kiganjani mwako!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…