dah!
pole sweetheart na hii christmas
The Boss bado anayeyusha kukupeleka pariiiiiiii ulimfanyia mtimanyongo semeki yangu
Mkirua bure kabisa!sa hoz ungekuwa wapi sijui ah!
well hebu turudi jikoni
mi this x mas nna mpango wa kupika
-
NYAMA YA MBUZI YA KUCHOMA hii italiwa jioni hiv kama saa kumi na keuendelea mpka bujhee manake nna kina mangi kama saba hiv watakuja!
ntaipika hiviii
-marination ya kitunguu swaumu, maziwa mtindi,chumvi,limao,pilipili na tangawizi,ntaifanya mapemaaaa ili mpka mida ya saa saba hv naiweka kwenye waya then will do the geuzaring bisness mpka iive!thn ntaisip kwenye whisky thn nairudisha tena jikoni kukiwa na moto mdogo kabisa!tayari kwa kuliwa pilipili ya haya itahusika hapa nitamdesa
amu na ile chachandu yake
.
-LUNCH itakuwa ya ndizi mnyenyere kwa nyama pia
will menya ndizi,chemsaha nyama,andaa tui la nazi,karoti,na kitunguu maji
ndizi ntazikata pieces ndogo sio sana thn karoti ni kubwa kubwa na kitunguu majia pia kinakuwa size ya kati!
ntaanza kukaanga nyama,itunguu thn ntaweka ndizi ntaziacha zijichanganye thn ntaweka supu!
halafu ntachuja matui matatu ya nazi!lakwanza litakuwa zito kwa kweli! maji kidogoooooo,la pili maji kidogo kiasi
la tatu maji mengi kiasi ,after 10 misn zile ndizi jikoni zitakuwa ziko tayari kuwekwa tui la tatu!kisha nazifunika
zichemke,dk 10 zingine zitafanya ziwe poa kuwekwa tui la pili hili sitafunika wala kutoa mwiko!
nitaendele kupitisha mwiko mpka nione ndizi zimeiva kabisa na kiasi cha mchuzi hakitakuwa kiiingi!
halafu nitaweka tui la kwanza,sitatoa mwiko mpaka tui liechemke!thn taipua ndizi!tayri hizo
upande wa desert ntakuwa na smoothie ya tikiti maji maembe na maziwa fresh!itabidi tu iwe ya baridi aseee!
juice kwa wale wasiosukuma kilauri kama mie itakuwepo ila hapa bado sijaamua ntafanya ya matunda gani ila lazima iwe mixeeer
upande wa kisukumizio cha mbuzi choma ahahahha watahusika wenyewe wakija pesa angu hainunui beer mimi!lol!
KUSEMA UKWELI NATAMANI NINGEKUBEBA UJE!