New Mzalendo Style.

New Mzalendo Style.

Malila

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2007
Posts
5,329
Reaction score
5,024
Ukisoma uzi wa ufugaji kuku aliotoa Mzalendo unaweza kucheka, kwa sababu alisema ukweli kwamba alianza na kuku mmoja tena jogoo,baadae alimla. Hii style ni nzuri kwa sababu, kwanza inakuondoa kwenye nadharia na kukupeleka kwenye vitendo. Imebidi nii-copy na kui-paste kwangu. Nimenunua ng`ombe mmoja tu chotara aliyepandishwa. Kwa wale wanaopenda kufuga ng`ombe basi tuwasiliane hapa hapa jamvini. Mzee aliyeniuzia mimi ana ng`ombe wengi wazuri na bei yake ni nzuri.
 
Malila uliyoyanena ni ya kweli kabisa

kuna sector ambazo serekali ingekuwa imeweka msukumo naamini ingewatoa watanganyika wengi,,kila siku nafikiria UVUVI, UFUGAJI HUSUSANI UZALISHAJI WA MAZIWA, ASALI, MBUZI=KONDOO wanasoko kubwa sana Arabuni mayai. Tatizo watawala wetu wamekosa dira tu hakuna lingine

kaka naomba utupe taarifa zaidi hawa mifugo wanapatikana wapi na kwa bei gani? Ukimwgaga taarifa hapa utakuwa umesaidia wengi saana,,,mie nilikuwa nataka ngombe kama wawili waliopandwa nitakushukuru ukini PM

Ubarikiwe saana
 
Malila uliyoyanena ni ya kweli kabisa

kuna sector ambazo serekali ingekuwa imeweka msukumo naamini ingewatoa watanganyika wengi,,kila siku nafikiria UVUVI, UFUGAJI HUSUSANI UZALISHAJI WA MAZIWA, ASALI, MBUZI=KONDOO wanasoko kubwa sana Arabuni mayai. Tatizo watawala wetu wamekosa dira tu hakuna lingine

kaka naomba utupe taarifa zaidi hawa mifugo wanapatikana wapi na kwa bei gani? Ukimwgaga taarifa hapa utakuwa umesaidia wengi saana,,,mie nilikuwa nataka ngombe kama wawili waliopandwa nitakushukuru ukini PM

Ubarikiwe saana

Hawa ng`ombe wako Mkuranga, bei yake ni laki sita tu bila dalali. Ukitaka wa kienyeji ndama mdogo andaa laki tatu,lakini chotara ndama mdogo andaa laki nne tu.
 
Kaka nashukuru saana
hawa ngombe ni aina gani mkuu
naweza pata Borani ambao wamechanganyika?
 
Kaka nashukuru saana
hawa ngombe ni aina gani mkuu
naweza pata Borani ambao wamechanganyika?

Huyu mfugaji aliniambia ni crossbreed ya Mafia. Sasa na mimi nikasahau kutafuta hii breed ya Mafia ni ipi/inafanana na ipi. Tutapata majibu japo kwa kuchelewa kidogo.
 
Ukisoma uzi wa ufugaji kuku aliotoa Mzalendo unaweza kucheka, kwa sababu alisema ukweli kwamba alianza na kuku mmoja tena jogoo,baadae alimla. Hii style ni nzuri kwa sababu, kwanza inakuondoa kwenye nadharia na kukupeleka kwenye vitendo. Imebidi nii-copy na kui-paste kwangu. Nimenunua ng`ombe mmoja tu chotara aliyepandishwa. Kwa wale wanaopenda kufuga ng`ombe basi tuwasiliane hapa hapa jamvini. Mzee aliyeniuzia mimi ana ng`ombe wengi wazuri na bei yake ni nzuri.

ndo maana napenda hapa jukwaani!!
 
Kaka nashukuru saana
hawa ngombe ni aina gani mkuu
naweza pata Borani ambao wamechanganyika?

Kuna rafiki yangu mmoja kapata Boran toka sehemu fulani baada ya kushindwa kupata frisien (spelling sijui), nitamuuliza kama Boran bado wapo.
 
Hawa ng`ombe wako Mkuranga, bei yake ni laki sita tu bila dalali. Ukitaka wa kienyeji ndama mdogo andaa laki tatu,lakini chotara ndama mdogo andaa laki nne tu.
Safi sana mkuu,sasa mkuranga kubwa lakini naomba maelekezo zaidi niko mbioni soon ntamaliza ujenzi wa banda langu nipate japo mmoja wa kuanzia aka newmzalendo style tuko wengi ,...
 
Safi sana mkuu,sasa mkuranga kubwa lakini naomba maelekezo zaidi niko mbioni soon ntamaliza ujenzi wa banda langu nipate japo mmoja wa kuanzia aka newmzalendo style tuko wengi ,...

Mkuranga mjini kabisa pale pale, nitakupa simu yangu kwa njia ya PM ili nikuelekeze vizuri.
 
Just out of curiosity Mkuu Malila. Hivi hao ng'ombe wa Mkuranga wanatoa maziwa takribani lita ngapi kwa siku?
 
Just out of curiosity Mkuu Malila. Hivi hao ng'ombe wa Mkuranga wanatoa maziwa takribani lita ngapi kwa siku?

Huyu Mkulima alisema mzao wa kwanza unaweza kupata lita tano asubuhi na jioni pia kama unamlisha vizuri. Mkulima huyu yy hakumui maziwa kwa biashara, ni yake na watoto wake. Nilichojifunza ni kwamba mpango wa maziwa hana,hata pale home kwake hata maji ya kunywa mifugo yake hana. Ila ana ng`ombe wengi sana na wazuri kiafya.
 
Huyu Mkulima alisema mzao wa kwanza unaweza kupata lita tano asubuhi na jioni pia kama unamlisha vizuri. Mkulima huyu yy hakumui maziwa kwa biashara, ni yake na watoto wake. Nilichojifunza ni kwamba mpango wa maziwa hana,hata pale home kwake hata maji ya kunywa mifugo yake hana. Ila ana ng`ombe wengi sana na wazuri kiafya.
Shukrani Mkuu, huyu Ngombe anaweza akawa msaada mkubwa sana kwenye kulea familia hapa mjini, lakini naona kama hajakaa vizuri sana kibiashara. Kuna ndugu yangu yeye aliagiza Friesian Cow mmoja kutoka Kenya akampeleka Moshi, anatoa 35 ltrs per day. naona wazee wake hawamsumbui tena na hela ya kujikimu. Naona kama aina hii imekaa vizuri kibiashara, kama una eneo zuri na unakaa sehemu isiyo na Joto kama Dsm
 

Attachments

  • friesian Cow.jpg
    friesian Cow.jpg
    37.7 KB · Views: 107
Shukrani Mkuu, huyu Ngombe anaweza akawa msaada mkubwa sana kwenye kulea familia hapa mjini, lakini naona kama hajakaa vizuri sana kibiashara. Kuna ndugu yangu yeye aliagiza Friesian Cow mmoja kutoka Kenya akampeleka Moshi, anatoa 35 ltrs per day. naona wazee wake hawamsumbui tena na hela ya kujikimu. Naona kama aina hii imekaa vizuri kibiashara, kama una eneo zuri na unakaa sehemu isiyo na Joto kama Dsm

Friesian nina wajua walipo, nina uwezo wa kuwachukua, lakini ni delicate sana kwa mazingira ya pwani. Pili, sasa hivi nafanya in-house training kwa vijana wangu ili wajue kukaa na ng`ombe wa maziwa,tatu nataka huyu Chotara awe ndio mlipa mshahara kwao. Sasa nikiona wamemudu vizuri kumtunza huyu Chotara, naleta aina nzuri toka Ruvu, kisha tunagawana. Maziwa ya Chotara yao na huyu mpya yangu. Chotara akizaa mtoto wa kwanza wangu, wa pili wa kijana wangu. Hii ndio plan yangu.
 
Friesian nina wajua walipo, nina uwezo wa kuwachukua, lakini ni delicate sana kwa mazingira ya pwani. Pili, sasa hivi nafanya in-house training kwa vijana wangu ili wajue kukaa na ng`ombe wa maziwa,tatu nataka huyu Chotara awe ndio mlipa mshahara kwao. Sasa nikiona wamemudu vizuri kumtunza huyu Chotara, naleta aina nzuri toka Ruvu, kisha tunagawana. Maziwa ya Chotara yao na huyu mpya yangu. Chotara akizaa mtoto wa kwanza wangu, wa pili wa kijana wangu. Hii ndio plan yangu.

I salute you, your Honour.Kwa ridhaa yako, naomba nireplicate hii model sehemu fulani, lakini kabla ya kufika huko nitakuwa nimeshakutafuta ili nijifunze kitu fulani hata kama ni kwa kugharamia. Aksante
 
mkuu Malila; i salute you man, sasa mimi nitakutafuta kuanzia tarehe 25 ili tubadilishane mawazo...
Nina ndoto ya kua mjasiriamali
 
I salute you, your Honour.Kwa ridhaa yako, naomba nireplicate hii model sehemu fulani, lakini kabla ya kufika huko nitakuwa nimeshakutafuta ili nijifunze kitu fulani hata kama ni kwa kugharamia. Aksante

Kama uko Bongo, basi mimi nitakuwepo kuanzia 28 february mpaka 27 march, ktk kipindi hicho naweza kukutana na wewe bila shida. Ktk mambo haya ya kupeana uzoefu, gharama hazitakiwi kuwepo kabisa. Naamini tutaonana. Hiyo itumie tu ndugu, mafanikio yako ndio mafanikio yangu na jamii kwa ujumla.
 
mkuu Malila; i salute you man, sasa mimi nitakutafuta kuanzia tarehe 25 ili tubadilishane mawazo...
Nina ndoto ya kua mjasiriamali

Hata mimi pia nitafurahi tukionana ili na mimi nipate kutoka kwako. Nitaingia Dar february mwishoni, Mungu ni mwema atatupa muda na afya.
 
Kama uko Bongo, basi mimi nitakuwepo kuanzia 28 february mpaka 27 march, ktk kipindi hicho naweza kukutana na wewe bila shida. Ktk mambo haya ya kupeana uzoefu, gharama hazitakiwi kuwepo kabisa. Naamini tutaonana. Hiyo itumie tu ndugu, mafanikio yako ndio mafanikio yangu na jamii kwa ujumla.

Noted. Nimeshaiingiza schedule yako kwenye Kalenda yangu, nadhani tutakuwa na mengi ya kujifunza Mkuu. Aksante na Kila la heri pia
 
Back
Top Bottom