Bongo movie wana dhambi ya ubaguzi na uzinzi, yaani waanawaacha watu wenye vipaji halisi vya kuigiza wanawachukua malaya na ndio maana bongo movie nyingi hazina creativity, hasa upande wa waigizaji. Hatuna uwezo wa kuwa na vifaa vya kisasa kwa ajili ya kuandaa movie, lkn waigizaji wenye vipaji halisi tunao basi tuwatumie. Bongo movie soko lenu litakuwa siku mkiacha kuchagua waigizaji kwa kuangalia mahips, sura na matako kama kigezo cha ugizaji upande wa wanawake na upande wa wanaume sifa ya kuwa muigizaji uwe shombe shombe na kuuma uma lips, mnajiharibia. We movies inafanyika bush akina kaka nywele zina super black na ukija kwa akina dada kuanzia mwanzo mpaka mwisho kajifunika kitambaa kichwani, anaogopa nywele kuchafuka. Msizilaumu movie za nje, kwani zilikuwepo tokea tunazaliwa na Kuna kipindi movies zenu zilizipita hizo movie za nje kwa sababu ubunifu ulikuwa mkubwa. Ila hilo mnalolidai la ulinzi wa kazi zenu, kweli ni haki yenu lkn hilo la Kuzuia movie za nje mmechemka, boresheni kazi zenu kwa kuwatumia waigizaji wenye vipaji halisi na si hawa wauma lips na watikisa matako.