Neymar Jr aitwa kikosi cha Brazil baada ya miaka miwili! Antony na Endrick watemwa

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Nyota wa Soka Neymar Jr amerejea katika kikosi cha timu ya taifa ya Brazil kwa michezo ya Machi, ikiwa ni mara yake ya kwanza kuitwa baada ya takriban miaka miwili.

Hata hivyo, Antony na Endrick wameachwa nje ya kikosi kwa mara nyingine tena.

Kikosi Kamili:

Makipa:
Alisson, Bento, Ederson.

Mabeki: Danilo, Gabriel Magalhães, Léo Ortiz, Marquinhos, Murillo, Guilherme Arana, Vanderson, Wesley.

Viungo: André, Bruno Guimarães, Gerson, Joelinton, Matheus Cunha.

Washambuliaji: Neymar, Estêvão, João Pedro, Raphinha, Rodrygo, Savinho, Vinicius Jr.
 
Antony hana kiwango cha kuichezea Brazil kwa sasa, hajiamini kabisa, anapoteza sana mipira,
 
Sioni brazil ikienda kushinda hizo game mbili za Argentina na Colombia, Ukiangalia mchezaji mmoja mmoia, wana uwezo mkubwa, ila ukiwaangalia kama team unaona kabisa hawana uelekeo
 
mashabiki wa brazili tulikuwa tuna imani ingekuja siku moja tukawa na akina ronaldo,rivaldo ,cafu,ronaldinho ,romario, carlos,dunga n.k wapya
ila kiukweli hii ni ndoto
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…