Mzee wa Code
Member
- Sep 23, 2024
- 61
- 91
Mimi ni Mkulima kutoka Mbinga mkoani Ruvuma, nimekuja mbele yenu nikiwa na changamoto ambayo kwa imani yangu najua kupitia nyie naweza kupata msaada ambao kimsingi sio tu utanisaidia pekee yangu bali sisi sote wenye hii changamoto.
Naomba sauti hii ifike kwa Wizara ya Kilimo na ngazi ya juu ya Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA).
Kumekuwa na tabia ya ucheleweshwaji wa malipo ya mahindi ambayo tunauza kwa NFRA, jamani imepita miezi miwili sasa, tumeuza Mahindi yetu lakini mpaka leo imepita miezi miwili malipo bado changamoto.
Jambo la kusikitisha zaidi ni kuwa msimu mpya wa kulima umeanza tukiwa hatuna mitaji ya kueleweka kwa kuwa mitaji yetu yote tumeipeleka kule NFRA, tukiamini kama pindi tutakapolipwa basi tunarudi tena shamba na shughuli zingine kuendelea.
Wengi wetu tunategemea kilimo kitutoe katika Maisha lakini NRFA wapo kimya kila tukienda tunapigwa kalenda bila majibu ya msingi.
Kwa kawaida NRFA huwa wanafunga vituo pindi muda wa mauzo unapomalizika, sasa hivi wamefunga kituo cha huku kwetu, tukiwapigia simu hawapokei, tukienda kuuliza kwenye kurasa zao za Mitandao ya Kijamii napo hakuna majibu sahihi.
Kuna tetesi kuwa wanataka kuwalipa kwanza Wakulima wanaodai malipo kidogo, wale tunaodai malipo kuanzia Sh milioni 10 tuendelee kukaa benchi, kama ni hivyo tutatoboa kweli kimaisha kwa staili hiyo?
Naomba sauti hii ifike kwa Wizara ya Kilimo na ngazi ya juu ya Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA).
Kumekuwa na tabia ya ucheleweshwaji wa malipo ya mahindi ambayo tunauza kwa NFRA, jamani imepita miezi miwili sasa, tumeuza Mahindi yetu lakini mpaka leo imepita miezi miwili malipo bado changamoto.
Jambo la kusikitisha zaidi ni kuwa msimu mpya wa kulima umeanza tukiwa hatuna mitaji ya kueleweka kwa kuwa mitaji yetu yote tumeipeleka kule NFRA, tukiamini kama pindi tutakapolipwa basi tunarudi tena shamba na shughuli zingine kuendelea.
Wengi wetu tunategemea kilimo kitutoe katika Maisha lakini NRFA wapo kimya kila tukienda tunapigwa kalenda bila majibu ya msingi.
Kwa kawaida NRFA huwa wanafunga vituo pindi muda wa mauzo unapomalizika, sasa hivi wamefunga kituo cha huku kwetu, tukiwapigia simu hawapokei, tukienda kuuliza kwenye kurasa zao za Mitandao ya Kijamii napo hakuna majibu sahihi.
Kuna tetesi kuwa wanataka kuwalipa kwanza Wakulima wanaodai malipo kidogo, wale tunaodai malipo kuanzia Sh milioni 10 tuendelee kukaa benchi, kama ni hivyo tutatoboa kweli kimaisha kwa staili hiyo?