Ng'ombe aliyemuua mwenye ng'ombe

Ng'ombe aliyemuua mwenye ng'ombe

Mtondoli

Member
Joined
Nov 9, 2021
Posts
70
Reaction score
174
Watu wa Kaya hii wana utaratibu wao, mpangaji hana sauti kwa mwenye nyumba katu, hawezi hata kupiga mluzi nje ya nyumba mbele ya mwenye nyumba, kwanini asione aibu kumpigia kelele mwenye nyumba?

Alipotia nia mwendazake aliwaomba wenye nyumba wampangishe kwa miaka kumi kisha atawarudishia nyumba kwa makubaliano ya kuiboresha zaidi, mwenye nyumba akashauriana na wanafamilia wakamwamini wakampa, loooh na kumbe mpangaji ni mbogo maji alipohamia tu kaanza kuwatimua kuanzia mwenye nyumba na watoto wake

Kila aliyejitambulisha kwamba yeye ni sehemu ya familia ya mmiliki wa nyumba alitimuliwa, mpangaji kwa kujihami akaleta watu wake, wengine kawakodisha kutoka nje wengine kawachukua jeshini, yarabi Mungu kaamua kuichukua roho ya mpangaji Sasa wenye nyumba na familia wameonekana kila sehemu wengine wamebeba magodoro, wanaelekea kwenye nyumba yao,na sasa wamejiapiza kuirudisha nyumba mikononi mwao

Kila watakaemkuta watamtolea dirishani, ndio maana NAPE kamwambia Polepole kina wenyewe shekhe! Polepole na wenzake hawaamini kama wanatakiwa kuwapisha wenye mji, mwendazake aliwapiga makufuli mpaka waasisi,mzee Makamba Kama hakuwepo, Kinana Kama hakuwepo,wengine ilibidi tu watangulie ili kumuondolea bugudha mpangaji 😂😂
 
Nchi inajengwa kwa misingi bora na katiba. Haya mambo ya wenyewe na waasisi ndiyo yalimkera Hitler, yalileta mapinduzi ya Ufaransa na yalifanya matajiri wengi kukimbilia USA na kupanga katiba inayowaongoza kwa misingi ya Demokrasia.
 
wanagombania nyumba ya ukoo, ndio maana mtoto wa kwanza na uzao wake walitimuliwa na mwana ukoo mmoja aliyekuwa jeuri, sasa jeuri huyu ametoweka na mtoto wa kwanza ametamalaki kila kona ya nyumba na kujinasibu kuwa nyumba ina wenyewe huku akisahau kuwa yeye naye ni msimamizi tu wa nyumba ya ukoo.

bahati mbaya wana ukoo hawajui wafanye nini ili nyumba ifaidishe ukoo mzima na sio kundi fulani tu,

Amini amini nakuambia siku wana ukoo wakiitaka nyumba yao tamaa zitawatokea puani wanandugu wanaojiona wana kila haki ya kufaidi mazuri ya nyumba peke yao.

kacnia
 
Polepole mwenyewe amesema haondoki labda wenye nguvu wamtolee dirishani mpere mpera!
 
Kuna mahali unaeza ukaenda na Sheria wao wakatumia mikuki
 
Mwamba Rais Magufuli alijua kuwanyoooooosha kweli kweli ATAKUMBUKWA DAIMA.
 
Back
Top Bottom