Ngorongoro Heroes uso kwa uso na Gambia

Ngorongoro Heroes uso kwa uso na Gambia

Shadida Salum

Journalist at JamiiForums
Joined
Sep 11, 2020
Posts
69
Reaction score
105
20210218_123142.jpg
Baada ya kupoteza katika mchezo wa ufunguzi wa mashindano ya Afcon U20 Juma lililopita, Timu ya Taifa Tanzania ya vijana chini ya miaka 20, almaarufu Ngorongoro heroes hapo kesho wanatupa tena karata yao kuvaana na Gambia katika Dimba la Stade Municipal de Nouadhibou huko Mauritania.

Ngorongoro Heroes ambayo ipo kundi C pamoja na Ghana , Morocco na Gambia, inashika nafasi ya mwisho baada ya kupoteza dhidi ya Ghana goli 4-0 . Nafasi ya tatu inashikwa na Gambia ambaye naye alipoteza dhidi ya Morocco goli 1-0.

Ghana ndiye kinara katika kundi hilo ambaye naye atashuka dimbani hapo kesho kupepetana na Morocco.

Michezo mingine itachezwa hii leo ya kundi B , hili ni kundi ambalo michezo yake miwili ya ufunguzi ilimalizika kwa sare.

Kwahiyo timu zote zina alama 1, Namibia anashika nafasi ya juu akifuatiwa na Jamhuri ya Afrika ya kati hii ni baada ya kutoka sare ya 1-1 na Tunisia anashika nafasi ya 3 akifatiwa na Burkina Faso hii ni baada ya kutoka sare ya bila kufungana.

Katika michezo ya leo Tunisia atakutana na Namibia huku Jamhuri ya Afrika ya kati atakuwa nyumbani kukipiga na Burkina Faso.
 
19 February 2021

Tanzania U-20 vs Gambia U-20​

Full time match results
Tanzania 1 - 1 Gambia


 
Nimeangalia mpira, vijana wamejutahidi sana na wanampira.fulani ivi amazing.. sema hawana exposure hawan confidence.

Kelvin John haja cheza kabisa, naona labda anaogopa kuumia

Ben stakie naye sijui anaogopa nini..

Wafuatao watafute popote wanywe soda nitalipa

1. Golipa leo alikua moto.. Mgore
2. Duchu (kameta kazi yako nzuri sana), nakuombea upate timu ulaya.

3. Dismas: kwangu mimi wewe ndio man of match, lile goli hata neymar hawezi funga... labda juninho .. akili nyingi.

4. Sop kijana wa coast union, upo vizuri sana, unajiamini, umefanya kazi nzuri sana.. nakuombea upate timu ulaya.

5. Rajab , umeingia kipindi cha pili, umebadili mwelekeo kabisa wa mchezo.. big up.

6. Lau beki matata sana.. kazi yako bora sana.

7. Msengi umeomyesha maturity.. big up.. pale kati mipira umeithihiti.

8. Kassimu upo poa sana

9. Msindo, big up, kazi nzuri sana..

10.. kapilima: kazi bora sana

11.. omari umeingia kipindi cha pili, unaweza kufila mbali.

Na wengi wote walio cheza.

Ushauri wa kocha: wale waliocheza dk 20 za mwisho ndio waanze kipindi cha kwanza na morocco.

Tuna amini Ghana na morocco watatoka suluhu au ghana ashinde, ili nafasi yetu ibakie kumfunga morocco.
19 February 2021

Tanzania U-20 vs Gambia U-20​

Full time match results
Tanzania 1 - 1 Gambia



Source : kamer Traveler
 
Back
Top Bottom