NguvuKazi suluhisho la kuondoa Umasikini na kujenga Uchumi!

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2006
Posts
4,526
Reaction score
1,540

Hivi kucheza Pool kuna athari gani na ubunifu na ufanisi?

Tanzania tunatumia masaa 12 kuzalisha kitu ambacho tunaweza kutumia masaa 4, kisha tunaona kutumia masaa 12 ni ufanisi? Mbona tunaongozwa na watu wenye akili za kiduwanzi na kijima namna hii?

Wastani wa mtu kuwa productive ni chini ya masaa 6, kama huko makazini hakuna anayepima uchapakazi kuna maana gani kuanza misako Rose garden kukamata wale wanaocheza pool na snooker kama si bao, drafti na domino?

Hivi kweli Mrutu anataka kutuambia Tanzania ambayo mhitimu wa UDASA hana kazi, leo itaanzisha sheria ya kusaka wasiofanya kazi? kazi gani? Je ni kulazimisha watu wawe wakulima au vibarua? kama hawataki, inawawasha nini serikali?

Kama serikali na mashirika yanashindwa kujiendesha kwa ufanisi kwa nini wasianze kuangalia miundo yao na uongozi na si kulaumu kina Invisible na Shy kwenda Rose Garden kula mchemsho?

Ikiwa wacheza Pool ni Machinga au waliojiajiri bado watakamatwa na askari wa TAMISEMI na kupelekwa Kibugumo?

Mbona hazungumzii uhujumu, ufisadi na uzembe wa viongozi kudumaza uchumi wa nchi?
 
Rev. Kishoka,
Kama sikosei ile sheria ya nguvu kazi si ndio iliyokuja kukusanya vijana mjini kama wazururaji?.. Je, mnakumbuka adha ya sheria ile au mimi ndo nimechanganya!..Utaweza vipi kurudisha sheria ile ikiwa hakuna ajira, wananchi wenyewe hawawezeshwi ktk kukopeshwa zana za kilimo, iwe ufugaji, uvuvi, ama kilimo chenyewe. Viwanda tupo at the low level ambayo haijawahi kutokea ukilinganisha na Population inayoweza kufanya kazi. Kifupi unemployment is at the highest level sasa hivi kuliko wkati wowote baada ya mashirika mengi kupunguza ama kufukuza watu kazi. Je,
Kuna mbinu gani serikali imejiandaa yenyewe kuhakikisha nafasi za ajira zimeongezwa na muhimu zaidi makosa yale hayatarudiwa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…