Nguzo 7 za Mafanikio Kupitia Manifestation, Nguzo Kwanza ni Kuijua Asili ya Manifestation, Kuwa na Ndoto, Kutia Nia, Kuamini, Kuthubutu, na Kutenda

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi,
Nipashe ya Leo 16/06/2024


NGUZO 7 ZA MANISTATION
Hili ni bandiko mwendelezo wa wiki iliyopita. Kama hukulisoma bandiko la kwanza, anzia hapa Siri ya Mafanikio Kupitia Manifestation -1: Manifestation ni Nini?

Kwa wasomaji wapya, wiki iliyopita niliintruduce topic ya kitu kinachoitwa manifestation, kwa lugha rahisi ni kuweka nia na kudhamiria kwa dhati kufanikiwa, kwa kutumia nguvu za nia, zilizomo ndani yako. Nikataja manifestations ina nguzo kuu 7.
  1. Foundation: Msingi wa Manifestation
  2. Laws: Sheria za Manifestation
  3. Vibrations:Mitetemo ya Manifestation
  4. Intention: Kuweka Nia
  5. Visualization: Kuona kwa jicho la ndani
  6. Affirmations: Kutumia Imani Chanya ya Kufanikiwa
  7. Process: Utekelezaji wa Manifestation.
Nguzo kuu ya kwanza ni Foundation: Msingi mkuu wa Manifestation ni nia na imani ya kufanikiwa.

Kuna makundi makuu 5 ya watu waliofanikiwa.

1. The Inheritors: hawa ni watu waliozaliwa kwenye familia tajiri, wafalme na matajiri, na viongozi, mtoto wa familia hii anazaliwa na kujikuta amerithi utajiri, hata kama kichwani ni zero, huyu atahesabika amefanikiwa.

2. The Best Brains: Hawa ni watu wenye akili nzuri, wasomi, wataajiriwa kazi nzuri, na kulipwa mishahara, hivyo kupata maisha ya mafanikio, kundi hili ni la waajiriwa.

3. The Best Talent: Hili ni kundi la watu wenye vipaji, wanamuziki, wasanii, waigizaji, wacheza mpira, au watu wenye vipaji vyovyote vinavyowaletea maisha mazuri, wakiwemo waandishi wa habari, watangazaji, etc. Mwanamuziki Michael Jackson, hakusoma hata darasa moja!, huyu Daimond Platnum wetu, Hamonise ni darasa la saba tuu lakini wamefanikiwa kutokana na vipaji.

4. The Hard Workers: Wafanyakazi kwa bidii, hawa ni working class, ukifanyakazi kwa bidii, utafanikiwa, hili ni kundi la wanaofanikiwa kwa kutumia nguvu zao, “mtaji wa masikini ni nguvu zake”.

5. Fixers: Hili ni kundi la mwisho la wapiga domo!, humu ndio kuna wanasiasa, wanaweza wasiwe best brains, hawana talent yoyote, sio hard workers, lakini wanafanikiwa kwa kupiga deals, fix na kupiga domo.

Makundi yote hayo yanafanikiwa kwa kufanya manifestation kwa kujua au bila kujua.

Lugha nyingine ya manifestation is “making your dream come true”, kufanya ndoto yako kuwa kweli.

Msingi mkuu wa manifestation ni nia na imani ya kujiamini kuwa wewe una powers ndani yako na una uwezo wa kufanikiwa, kwa kutumia mawazo yako kutia nia ya kuzifungulia hizo powers zilizomo ndani yako zikuletee mafanikio ya kupata kitu unachokitaka

Manifestation ni kutumia the power of mind, through positive thinking to open the energy stored in your subconscious mind, ikupe chochote unachokitaka. Watu wote wenye mafanikio wanatumia manifestation kwa kujua au kutokujua, ila siri kuu ya kwanza ya mafanikio, ni kuwa na ndoto, wazo, nia, kisha kuifanyia kazi hiyo ndoto.

Kuna wengi wana mawazo mazuri tuu ya maendeleo, na kusema nikiwa mkubwa nataka kuwa pilot, daktari, polisi, tajiri, lakini wazo hilo linaishia hewani, kwasababu haulifanyii kazi. Ili uweze kufanikiwa, ni lazima ufanyie kazi ndoto yako. Kuota tuu ndoto ya unataka kuwa tajiri, halafu hauifanyii kazi hiyo ndoto, inaitwa ni “day dreaming”, yaani yaani kuota ndoto ya mchana, kama ile hadithi ya ndoto ya Alinacha kwenye hadithi za Alfu Lela Ulela.

Kwenye Nguzo 7 za Manifestation, Nguzo ya kwanza ni Asili ya Manifestation
Kuna wengi wanadhani manifestations ni jambo jipya, hapana, manifestation ni jambo la enzi na enzi toka enzi za Masiha, alifundisha “ombeni mtapewa", "tafuteni mtapata", "bisheni hodi, mtafunguliwa”, na akasema “hata ukiwa na imani ndogo kama chembe ya haradali, unaweza kuiambia milima iondoke na milima ikahama”.

Kitu kinachoitwa meditation, tafakuri jadidi au tahajudi, ni manifestation. Wakati wa mwezi Mtukufu wa Ramadhani, Waislamu, wanatakiwa kunuizia kufunga kila siku kuwa kesho nitafunga. Kitendo cha kunuizia ni manifestation. Wakatoliki hufanya sala za novena ni manifestation. Sala za kujirudia rudia kama rozari ni manifestation, sala za tasbihi ni manifestations.

Mara nyingi enzi za ujana maji ya moto, mvulana akimuona msichana, akampenda, akadhamiria kumpata, hufanya juhudi mbalimbali, ili kumpata, hivyo kutumia manifestation bila kujijua, ila mwisho wa siku, hufanikiwa.

Ili kupata mafanikio kwenye jambo lolote, lazima kwanza, uwe na ndoto ya kufanikiwa, ndoto hiyo ni kuwa na mawazo chanya, kwa kizungu, “positive thinking”. Mawazo chanya haya yanakuwa yana nguvu ndani yake, inayoitwa “the power of positive thinking”. Kisha uweke nia thabiti na ya dhati ya kufanikiwa, tatu ufanye juhudi na bidii kulifanikisha hilo jambo lako. Ile power au nguvu iliyomo ndani yako, itafungua milango ya mafanikio, na utafanikiwa.

Kuna watu wanadhani kuna watu wana bahati tuu ya kufanikiwa na wengine wana laana ya umasikini, hapana!, Mungu alituumba binadamu wote tufanikiwe, ila kuna kanuni za mafanikio, ukizifuata na kuzipatia, ni lazima utafanikiwa.

Wiki itajayo nitakuletea nguzo ya pili ya manifestation yenye sheria 12 za mafanikio kupitia manifestation ambazo ukizifuata kikamilifu, utafanikiwa.

Paskali
 
hayo ulioandika yanalipa kwenye Christian western societies au jamii zinazofwata western philosophy i.e meritocracy, tanzagiza haifwati meritocracy hivyo hard work haiwi rewarded na hailipi wanaoafanikiwa (karibia)wote ni wezi, walaghai na wababaishaji btw rostamu is 8 billion dollars worth, how is that possible kwenye nchi masikini kabisa duniani kama tanzagiza?
 
Mimi binafsi siwezi kupinga ukiteuliwa, na hakuna atakayepinga kwasababu hawaulizwi kukubali au kupinga. Mi naona ni uchoyo au wivu kuchukia au kumsema vibaya mwenzio aliyeteuliwa. Ni jambo jema kuitumikia nchi yako ukipata fursa, na kazi hizi huwa zinamipaka na miiko yake. Usijinyime fulsa kwa kutuogopa wananchi.

Naamini utakuwa kiongozi mzuri sana, hilo sina shaka nalo, na kelele huwa haziishi, tunamsema Makonda na viongozi wengine humu kila siku lakini majukumu yao ni makubwa na mengi sana, sidhani kama wanaweza kumaliza shida na changamoto zetu. Ila ni ubinadamu wetu kulalamika na kusema tunachoona na kuamini.

Hata wewe tutakulalamikia kwa sababu hiyo ni hulka ya binadamu wote duniani.

Ukipata nafasi, chukua kazi ukatuonyeshe mfano wa kiongozi mzuri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…