Ngwair alikuwa na kipi cha pekee kwa watu kumsifia sana, au ni kufunika kifo chake cha aibu?

Wakazi mwenzako anateseka twitter huko. Sijajua umri wako ila kwangu Ngwair yupo kwenye top 5 yangu ya mda wote na kwa upande wa freestyle kwa kifupi hajapatikana wakuvaa kiatu chake,Ngwair ana uwezo wa kuflow hata kwenye biti ya mdundiko na akatoa hits.Ana uwezo wa kuimba nyimbo zote zenye ujumbe na za bata.
 
Jamaa kawa inspired na tweets za Wakazi inaonekana ni shabiki wa talentless Wakazi 😂😂😂
 
Jamaa kawa inspired na tweets za Wakazi inaonekana ni shabiki wa talentless Wakazi 😂😂😂
Wanachomfanya huko twitter hadi huruma kuna clip yake moja alikuwa yupo times fm mtangazaji anamwekea biti halafu anamwambia tupe freestyle Wakazi anadai "leo sijajiandaa kwa freestyle.........." 😂😂😂😂

Mimi wakazi hata uniwekee mil 1,uniambie nikutajie nyimbo yake hata moja sijui ana trend tu kwa kujiona anajua sana kisa kakaa US ila ni mweupe kishenzi.
 
A.K.A MIMI hiyo ni album bora ya muda wote ya Albert mangwea kulikuwa na hit songs zilizobamba kipindi iko
1-ghetto langu
2-skiliza jide ft fa
3-she got gwan
4-weekend
5-mikasi
6-bado nimo ft TID
7-kimya kimya

Najua ipo siku utakuja kumlinganisha p funk majani/master j na akina s2kizzy/laizer
 
Kuna mdude wa aka Mimi,Speed 120 ,CNN halafu kuna moja kati ya verse yangu bora sana kwenye wimbo wa Msela ya KR Mulla ft Ngwair,Nature,ile verse ndio alinyonga kabisa halafu kwa Mujibu wa KR wakati akihojiwa na Jabir wa EFM ile verse ali freestyle.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…