A
Anonymous
Guest
Mimi ni mmoja wa watu ambao nimekuwa nikifanya kazi kwa ukaribu na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), sina nafasi hiyo ya juu lakini nipo katika sehemu ambayo NHIF wakitimiza wajibu wao itakuwa ni furaha kwangu.
Lakini ninachokiona ni kuwa Mfuko huo ni kama umepoteza uwezo wa kulipa fedha kwa watoa huduma wake, kwa sasa watoa huduma wengi hawajalipwa madai ya zaidi ya Miezi 5, kutokulipwa kwao kunasababisha pia sisi wengine tuwe na maisha magumu.
Wengi wetu hatujalipwa mishahara na malipo mengine kwa kuwa waajiri wetu wanategemea kulipwa na NHIF ili nao waweze kutulipa, hivyo huo mnyororo unaathiri sana maisha yetu,
Najua Mkataba unawataka NHIF kulipa watoa huduma ndani ya siku 60 tangu walipowasilisha madai, kwa sasa hali ni tofauti kwa watoa huduma kwani wapo wanaodai fedha walizohudumia wanachama wa NHIF tangu mwezi wa 6 Mwaka huu 2023 ambao ni muda wa miezi 5, hiyo ni kinyume na mkataba.
Tumekuwa tukijaribu kuulizia sababu za wao kuchelewesha malipo kwa muda wote huo, sababu wanazotoa ni kuwa hawajapokea fedha kutoka Hazina kwa kuwa wameishiwa fedha.
Kitendo hiki kinavunja mkataba na kuathiri ubora wa utoaji huduma za afya nchini hasa tunapoelekea Afya kwa wote.
Nashauri NHIF ilipe madai yetu sisi watoa huduma kwa mujibu wa mkataba.
====
Pia soma: Hospitali za private (binafsi) zatishia kutohudumia wagonjwa wanaotumia bima ya afya ya NHIF
Lakini ninachokiona ni kuwa Mfuko huo ni kama umepoteza uwezo wa kulipa fedha kwa watoa huduma wake, kwa sasa watoa huduma wengi hawajalipwa madai ya zaidi ya Miezi 5, kutokulipwa kwao kunasababisha pia sisi wengine tuwe na maisha magumu.
Wengi wetu hatujalipwa mishahara na malipo mengine kwa kuwa waajiri wetu wanategemea kulipwa na NHIF ili nao waweze kutulipa, hivyo huo mnyororo unaathiri sana maisha yetu,
Najua Mkataba unawataka NHIF kulipa watoa huduma ndani ya siku 60 tangu walipowasilisha madai, kwa sasa hali ni tofauti kwa watoa huduma kwani wapo wanaodai fedha walizohudumia wanachama wa NHIF tangu mwezi wa 6 Mwaka huu 2023 ambao ni muda wa miezi 5, hiyo ni kinyume na mkataba.
Tumekuwa tukijaribu kuulizia sababu za wao kuchelewesha malipo kwa muda wote huo, sababu wanazotoa ni kuwa hawajapokea fedha kutoka Hazina kwa kuwa wameishiwa fedha.
Kitendo hiki kinavunja mkataba na kuathiri ubora wa utoaji huduma za afya nchini hasa tunapoelekea Afya kwa wote.
Nashauri NHIF ilipe madai yetu sisi watoa huduma kwa mujibu wa mkataba.
====
Pia soma: Hospitali za private (binafsi) zatishia kutohudumia wagonjwa wanaotumia bima ya afya ya NHIF