NHIF mmeacha lengo la msingi na kujiingiza kwenye biashara

NHIF mmeacha lengo la msingi na kujiingiza kwenye biashara

Singo Batan

JF-Expert Member
Joined
Apr 24, 2020
Posts
295
Reaction score
198
Mwanzoni wakati mfuko huu unaanzishwa ulikuwa unafanya vizuri sana kwasababu ulikuwa unachangiwa na Watumishi wa umma na kuwahudumia watumishi wa umma. Mfuko ulikuwa stable sana. Tatizo lilianza mlipoingiza tamaa za kuufanya kuwa mfuko wa biashara badala ya huduma.

Haikupaswa taha kidogo kuufanya mfuku huu uhudumie kundi kubwa la watu kabla hamjafanya utafiti wa kutosha kama mnaweza kuwahudumia. Watumishi na wategemezi wa watumishi waliwatosha sana kuwahudumia. Mlichotakiwa kufanya ni kutoa mapendekezo ya kuanzishwa kwa bima ya wananchi wote nje ya watumishi, na mfuko wenu ungekuwa unachangia shirika hilo jipya linalohudumia wananchi wote ambao sio wanufaika wa NHIF.

Madhara ya kujitanua bila utafiti wa kutosha kuhusu gharama za uendeshaji wa shirika ni haya yanayojitokeza sasa, kupunguza huduma na kushindwa kukidhi matarajio ya wateja wenu hasa wale mlioanza nao. Ushauri kwenu kaeni na CHF boresheni models za huduma huko na ifanyeni ikidhi standards za kitaifa kamailivyo NHIF kisha mpunguze idadi kubwa ya wateja wanaoelekea kuwashinda na kuufilisi mfuko wenu.

jikiteni kwenye huduma ya msingi ili msiharibikiwe zaidi. wateja hawategemei kushushiwa au kupunguziwa viwango vya huduma badala yake viwango vinapaswa kuongezeka. Zile ni fedha zao sio hisani mnatoa
 
Sijaelewa ni Kwa nini nyinyi mnaoitwa/ kujiita watumishi wa umma/serikali huwa mnajiona kama ni watu maalum? Nyinyi ni nani kwani?

Bima zipo AAR unatibiwa Agha Khan, unaweza kuchukuliwa na flying doctor popote na matibabu yako kama yanahitaji upelekwe abroad bima ina cover, nenda kakate huko, ipo bima inaitwa Strategies nenda kakate huko, kwani umelazimishwa NHIF?

Sasa wewe Kitu kinaitwa "National" yani cha Taifa unataka kiwe chombo Kwa ajili ya wajinga wachache tu kama wewe?
 
Huna lolote unalojua juu ya biashara/huduma ya bima na ufanyaji kazi wake kwa ujumla. [/I]
 
Mtumishi wa umma kiatu soli imeisha nenda kwa fundi mangi uweke nyingine kwa mkopo, mtumishi wa umma, mtumishi wa umma. Sisi wakulima sio Watanzania?

Sawa na sisi private sector hatutaki watumishi wa umma wake hospital binafsi. Katibiweni hospital za umma
 
Watumishi wa umma ni janga kwenye hii nchi , huwa yanajiona kama yameyapatia maisha , utendaji kazi zero kazi kupanua panua tuu midomo kuomba nyongeza za mishahara , shwain.....
 
Unajua kwa nini NHIF ina neno National?

Jifunze kwanza maana ya neno national kisha ndipo uwakosoe NHIF?

Unajua chanzo cha pesa zilizoanzisha hiyo NHIF ama ruzuku inazopata NHIF ni hela za kodi zinazolipwa na hao ambao wewe hutaki NHIF iwahudumie kisa sio watumishi wa uma.

Pesa za walipa kodi unazitaka ila kuhudumia walipa kodi hutaki sababu sio watumishi wa uma
 
Huu ni ubinafsi, kwa hiyo sisi ambao sio watumishi wa umma tuondolewe NHIF kwani hatuchangii pesa?
 
Daah jobless huu uzi wako tumeusoma kwa uchungu sana ..


Niseme tu watumishi muendelee kudidimizwa na kunyonywa mpka kiama
 
Back
Top Bottom