NHIF mnatuchanganya

NHIF mnatuchanganya

DidYouKnow

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2019
Posts
1,229
Reaction score
1,950
Nimempeleka bimkubwa katika mojawapo ya hospitali ya serikali hapa jijini Dar.

Ana shida ya mgongo, vidonda vya tumbo, na presha. Leo alipaswa aonwe na madaktari watatu, daktari wa moyo, mifupa na utumbo.

Kwa sababu hospitali hii ina daktari bingwa wa mifupa na daktari bobezi wa moyo, nilitegemea tukionwa na daktari wa mifupa, tutaruhusiwa kuonwa na mbobezi wa moyo.

Ajabu tulipotoka kwa daktari bingwa wa mifupa, tumezuiwa kumwona daktari mbobezi wa moyo, ati kuanzia sasa ukitoka kwa daktari bingwa idara moja huruhusiwi kuonwa na daktari mbobezi wa idara nyingine isipokuwa huyo daktari naye awe level moja na yule aliyekuona mwanzo, na vice versa is true.

Wametuambia kama tunamtaka sana daktari wa moyo basi tuje siku ya pili. Sijaelewa hii mantiki.

Mbona NHIF mnafanya maisha kuwa magumu sana?
 
MAMBO Ni Magumu Sana Hii Mifuko Kama Huu NHIF Imepatwa Na Nini
 
Sasa hapo NHIF inahusikaje? Dirisha la mapokezi la bima walikataa? Kama wao waliona bibi yako anapaswa kuonwa na daktari bingwa wa level moja na huyo wa kwanza je kuna maelekezo mengine ya ziada walikupa? Je ulihoji kwann? Je kulikua na dharura yoyote ya kufanyiwa chekup ya mattzo yote kwa pamoja? Hio hospital ulioenda inaitwaje na bima hio ya NHIF je INACOVER hilo tatizo katika hio hospitali?
 
Pole sana Mkuu. Hao NHIF nahisi hawapo sawa kifedha. Naamanisha pesa waliyonayo ni ndogo kuliko madeni wanayodaiwa na Hospitali zinazitibu kwa Bima. Hivyo wanafanya Kila mbinu kupunguza gharama za matibabu kwa wahitaji hivyo kuleta usumbufu .
 
Back
Top Bottom