Nadhani kama hujui huwa wanaangalia nini basi hukupashwa kusema kuwa ni ' aibu ' kwa wana Arusha. Halafu wala haiitaji akili kubwa sana kutaka kujua ni kwanini TFF imeweka Kiingilio kidogo kama hicho katika hiyo Fainali ya ASFC. Kumbuka Mkoa wa Arusha kwa muda mrefu sasa hauna Timu yoyote VPL hivyo wakazi wa Arusha ni kama vile mwamko wao katika Kupenda mchezo wa Soka umeshuka kama siyo kupungua sana na njia pekee ya kurudisha ' hamasa ' na ' kuwavutia ' Watu warudishe mapenzi yao katika mchezo Kwanza ni kuwapelekea mechi muhimu kama ile halafu unawakea Kiingilio kidogo sawa na bure ili kuwatia moyo kisha na Wao sasa wajitahidi kuzipigania Timu zao ili basi ziweze kufanya vyema katika Ligi mbalimbali na zipande Ligi Kuu ya VPL na Mkoa uwe na Timu. Kama kuna Mkoa ambao ni dhambi sana kwa wenyewe kutokuwa na Timu VPL basi ni wa Arusha hasa kutokana na umuhimu wake ' strategically ' na ' economically '.
Kila la kheri.