mi nadhani hata kuwemo kwenye hiyo kumi bora tumependelewa, sawa tunazo kumbi nzuri za kisasa na nyingine zinajengwa lakini kuna zaidi ya hilo, generosity ya watu wake hali ya hewa, usafi wa miji yetu, si mnakumbuka Michael jacton alikuja Dar akafikia Kilimanjalo Hotel akaondoka anasema Nchi inanuka shombo yote ya ufukowa bahari harufu ya samaki zinazochomwa magogoni kidogo vingenyofoa pua yake.
Nenda Kigali anzia tu air pot unajihisi pumziko furani na utulivu wa akili hawana kumbi nyingi wala zi nzuri kuliko zetu, hayo mengine ninayoyataja yanamfanya mshiriki ajihisi pumziko. kwetu sasa mtu anashuka airport kwanza ni joto lililochamana na harufu mbayambaya mtaani anapishana na marundo ya taka kama vile magari ya kuzoa taka hayakuwahi kununuliwa, mifuko ya plastick iliyokuwa imepotea awamu ya 5 imezagaa utafikiri Nchi haina mwenyewe wakati yupo, barabara zimejaa michanga utafikiri lami haikuwahi kujengwa na viongozi wapo. akitakaaende kaliakoo kwa sifa ya soko kubwa anaondoka huko ameugua kichwa hapa kuna spika hapa generator pale mpiga debe wakati sheria za kudhibiti sauti zipo lakini hazifuatwi hao maafisa mazingira wa ninisasa?
Rwanda mitaa inasafishwa na wanamtaa, imefikia hatua hata barabara zenye lami au mawe zinajenge na wenye mtaa wanachanga na serikali inafanya kwa yale ambayo wannchi hawawezi, sisi huku hata fedha inayotolewa na serikali viongozi wanakula. Eeee wanakula si waliambiwa wale kwa urefu wa kamba yao.
kwa ujumla bado tuko mbali sana ktk masuala ya kuithamini Nchi yetu.