Ni aibu kwa wanafunzi wa elimu ya juu kuipongeza hotuba ya Jakaya Kikwete

Mnasihi

JF-Expert Member
Joined
Oct 9, 2013
Posts
7,762
Reaction score
7,100
Source gazeti la uhuru tarehe 26-12-2014. Nimeanza na chanzo ili kupunguza maswali.

Binafsi nimeshindwa kuwaelew hawa wasomi wetu juu ya uwezo wao wa kuchambua mambo ili kuja na suluhisho.

Kuipongeza hotuba ya JK juu ya escrow ni kutokumsaidia na kutowasaidia wananchi kuujua ukweli. Mnaiungaje mkono wakati wenzao hawakupata mkopo kutokana na kukosekana kwa fedha? Hivi zile sh. 21bn zilizoachwa kulipwa tra zingeweza kufanya mangapi katika jamii?.
Hebu mje mtuambie mmempongeza kwa lipi?.
 

wale ni wapumbavu flani ambao kabla kutoa tamko wananyweshwa viroba na kupewa buku tano tano halafu wanakuja na tamko.

naimani mzazi ukiona mwanao anakuwa sehemu ya wale ujue una hasara kwamba umepeleka ng'ombe shule usiendelee kuharibu fedha zako tena maana hata kuwa na msaada katika jamii tena na wewe pia hawezi kukusaidia.
 
Na mfumo wenyewe wa elimu kama wanasoma kwa kushindana tu nani atakuwa wa kwanza tusitegemee maajabu. Mbona hata maprofessa wanushangaza umma pia wanafunzi itakuwaje.
 
Wale wasomi uchwara,wanaishi kwa kujikomba na kushabikia kila kitu ili wapate mkate wao.Ni hasara kwa taifa kuwa na wasomi ambao hawana faida na hawajakombolewa kifikra.
 
Hoja hapa ni kuwa, kwanini wasomi wa elimu ya juu wamegeuka wasaliti na wapotoshaji wa kiwango cha juu kuhusu masuala nyeti hasa ya wizi wa fedha na rasilimali za umma kwa umma ili hali ukweli wanaujua? Ni nani sasa atasaidia kuuelimisha na kuuambia umma ukweli hasa wale waliokosa elimu?

Tumewashuhudia kina Dr. Bana & co wanavyojipa airtime kuupotosha ukweli. Ni nini maana ya wao kuitwa wasomi? Na sasa wanachuo nao wameamua kujiingiza kichwakichwa kuusaidia utawala wa mafisadi kuiba.

Hivi hawajajua kuwa ile benki ya standardchater ya hongkong kuna siku watakuja kuidai pesa yao baada ya kushinda kesi na tutakiwa kuilipa kama tulivyoilipa dowans. Tutafakri kwa usomi wetu jinsi ya kuiokoa nchi kutoka katika mikono ya mafisadi na sio kuungaunga mkono masuala yaliyowazi kabisa ambayo hata wale waliojiita wazee wa dar waliushtukia mchezo mchafu wa kulindana.

Jifunzeni kuisoma lugha ya mwili (body language). Usomi wetu uwe na maana ya kujikomboa kifikra na siyo kujikomba kwa fikra za wengine.
 
jamani naichukia sana serikali yetu baada ya wanafunzi wa vyuo vikuu kukosa mkopo kumbe pesa zipo wanazigawa tu
chuchuemu nyinyi ngojeni tu ipo siku.
 
Miaka hii hakuna wanafunzi vyuo vikuu..kuna wavaa milegezo na wauza mbunye tu
 
Kama ishu ni kodi ya bilioni 21 kwa nini mnamchafua Rugemalila aliyelipa kodi yake bilioni 38?
 

Tatizo lenu ni kulazimisha mawazo yenu yaonekane ni sahihi hata pale mnapopewa facts mnaona mnadanganywa.
 
Tatizo lenu ni kulazimisha mawazo yenu yaonekane ni sahihi hata pale mnapopewa facts mnaona mnadanganywa.

Ndugu maboso, wapo watu kwao usomi au uungwana au uhalisia au jambo lisilo dhambi lazima liwe kama wanavyotaka wao. Si hoja wala logic inatumika bali wanachoamini wao ndicho wanachotaka kila mtu aamini na wanakuambia hiyo ndiyo demokrasia.
 

Absolutely true !!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…