Ni aibu sana kwa wanafunzi wa vyuo vikuu kutokupiga kura

Ni aibu sana kwa wanafunzi wa vyuo vikuu kutokupiga kura

oneblood

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2011
Posts
244
Reaction score
51
Nasema ni aibu kwa wasomi wetu wa kada mbalimbali hapa nchini ambao wanategemewa na jamii kubwa ya watanzania katika kuleta mabadiliko na kuchochea maendeleo katika jamii watokazo,ni kama wiki moja sasa imepita tangu nilete uzi humu jamvini kuhusu kilichokuwa kinaendelea katka harakati za uchaguzi wa nafasi ya urais chuoni hapo na jinsi mizengwe mbalimbali ilivyokuwa inaendelea baada ya kila mgombea kubeba taswira ya uchama baina ya CDM na CCM chuoni hapo,bt me kama kijana msomi nimesikitishwa na kuumizwa baada ya kupokea taarifa ya jumla kamili ya wanachuo wa SAUT waliojitokeza kupiga kura katika uchaguzi huo ,ambapo kati ya wanafunzi 13500 waliopo chuoni hapo ni jumla ya wanafunzi elfu 3000 na....ndio waliojitokeza kupiga kura ya kuwachagua wabunge na kumchagua rais wa chuo hicho,ambapo Donavankamwene Mcheshi anaedaiwa kuwa kamanda wa CDM kumshinda mpinzani wake anaedaiwa pia kuwa kada wa CCM bwana Peter Bega katika uchaguzi uliofanyika jana chuoni hapo,kwakweli ni aibu kwa kuwa siku yote ya jana pindi uchaguzi unaendelea na vipindi vilikuwa vikiendelea madarasani bt wanafunzi walikuwa wanatoka darasani na kuvipita vituo vya kupigia kura na kuondoka bila kupiga kura,kwakweli hii ni changamoto kwa wasomi wa Tanzania,itakuwaje kama wataenda huko makwao,watawashauri nini ndugu zao,kaka ,dada na rafiki zao ambao si tu kwamba hawajaenda shule bali hata IQ yao ni ndogo na ya kawaida sana,itakuwaje hapo 2015?vijana na wasomi tuone umuhimu wa kushiriki katika michakato ya kidemokrasia ya kuchagua na kuchaguliwa la sivyo tutabaki kulalamika kuwa tunaibiwa kura.
 
Hakuna ukombozi wa kweli tz,ni watu na matumbo yao na familia zao! Hata mimi sitapiga kura maishani mwangu mpaka tumwazime kagame awe prezzo wa tz,hawa wengine ni ovyo tu,si ccm wala chadema ,ni yale yale tu! Njaa tatizo
 
Wasomi wengi wa tz huwa hawashiriki kwenye zoezi la kupiga kura,si SAUT tu,kila chuo uchaguzi ukifika wanadhani kama wanamfaidisha mgombea! Bt hao hao ndo walalamikaji wengi wenye kutengeneza kila aina ya tusi kwa watawala wakati nafasi za kuwakataa walikuwa nazo. Pls vijana wenzangu wasomi kura yako ni ajira,elimu,maji,barabara,mshahara nk kura yako ni maisha yako,ndugu yako,jirani nk TUBADILIKE.
 
Kumbuka jana wakati wa kupiga kura mvua kubwa ilianza kunyesha na kumbuka ilikuwa bado mapema nafolen zilikuwa ndefu at the same time wapiga kura walikuwa wanamiminika kwa kasi....baada tu ya ile mvua kuanza wanafunzi wengi walikimbia vituoni....na pale mvua ilipo malizika kulikuwa na hali ambayo haimvutii mtu kutoka nje.....but all in all these are assumptions!! Mimi pia nakuunga mkono..
 
Kwan huko chuon wameenda kusoma au kupiga kura?
 
Kumbuka jana wakati wa kupiga kura mvua kubwa ilianza kunyesha na kumbuka ilikuwa bado mapema nafolen zilikuwa ndefu at the same time wapiga kura walikuwa wanamiminika kwa kasi....baada tu ya ile mvua kuanza wanafunzi wengi walikimbia vituoni....na pale mvua ilipo malizika kulikuwa na hali ambayo haimvutii mtu kutoka nje.....but all in all these are assumptions!! Mimi pia nakuunga mkono..

Kama msomi anaweza kuona kutoka nje hakumvutii na akakubali kupoteza haki yake ni aina ya wasomi wa aibu tunaozalisha!!! Mvua ndiyo ikusababishe usipige kura!!!

Je siku mkiambiwa muandamane kwenye mvua itakuwaje kudai haki zenu???
 
Kwa structure ya Chuo hicho Uongozi wa SAUTISO ni pambo wala hauna mandate yoyote ya kuleta mabadiliko yenye tija kwenye matatizo ya wanachuo. Hilo nimeliexperience kwa kipindi nilichosoma hapo. Mara nyingi viongozi hujinadi kwa kutoa ahadi kedekede kwa wanachuo lakini mwisho wa siku ukiingia madarakani unaishia kutoka na kashfa tu.
 
Back
Top Bottom