HPAUL
JF-Expert Member
- Jan 18, 2011
- 410
- 567
Tangu uongozi wa TFF chini ya Karia uingie madarakani Agosti 2017, kumekuwa na kawimbi ka mafanikio kiasi katika soka la Tanzania angalau kwa kiwango fulani kulinganisha na TFF za Malinzi na Tenga au hata FAT huko nyuma.
Mafanikio
1. Kuimarika kwa team ya under 17 ya akina Kelvin ambapo iliweza ku-qualify kushiriki fainali ya mwaka 2019.
2. Tanzania kwa mara ya kwanza iliweza kundaa fainali michezo Africa Under 17 mwaka 2019.
3. Baada ya miaka 37 Tanzania iliweza ku qualify fainali ya AFCON mwaka 2019 iliyofanyika Misri.
4, Kwa mara ya kwanza Tanzania katika ngazi ya klabu iliweza kuvuka hatua ya makundi ya Klabu Bingwa Afrika na kuingia robo fainali 2019 (wengi watasema hayo ni mafanikio ya juhudi binafsi za klabu ya Simba, lakini huko nje wanajua ni mafanikio ya Tanzania).
5. Tumeweza kuunda timu ya Under 20 imara Ngorongoro Heroes na kufanikiwa kuchukuwa kombe la Afrika Mashariki na ya kati ugenini 2019.
6. Baada ya miaka 10 Tanzania imefanikiwa tena ku-qualify kwa mashindano ya CHAN itakayofanyika Kameruni 2020.
Je, hayo ni mafanikio ya TFF ya Karia au ni upepo tu wa bahati? Na kama ni mafanikio, je kuna dalili yatakuwa endelevu? Naomba maoni yenu.
Mafanikio
1. Kuimarika kwa team ya under 17 ya akina Kelvin ambapo iliweza ku-qualify kushiriki fainali ya mwaka 2019.
2. Tanzania kwa mara ya kwanza iliweza kundaa fainali michezo Africa Under 17 mwaka 2019.
3. Baada ya miaka 37 Tanzania iliweza ku qualify fainali ya AFCON mwaka 2019 iliyofanyika Misri.
4, Kwa mara ya kwanza Tanzania katika ngazi ya klabu iliweza kuvuka hatua ya makundi ya Klabu Bingwa Afrika na kuingia robo fainali 2019 (wengi watasema hayo ni mafanikio ya juhudi binafsi za klabu ya Simba, lakini huko nje wanajua ni mafanikio ya Tanzania).
5. Tumeweza kuunda timu ya Under 20 imara Ngorongoro Heroes na kufanikiwa kuchukuwa kombe la Afrika Mashariki na ya kati ugenini 2019.
6. Baada ya miaka 10 Tanzania imefanikiwa tena ku-qualify kwa mashindano ya CHAN itakayofanyika Kameruni 2020.
Je, hayo ni mafanikio ya TFF ya Karia au ni upepo tu wa bahati? Na kama ni mafanikio, je kuna dalili yatakuwa endelevu? Naomba maoni yenu.