Ni benki gani inayotoa mkopo kwa masharti nafuu?

Mbwa dume

JF-Expert Member
Joined
Jan 15, 2014
Posts
5,934
Reaction score
10,206
poleni na kazi za mchana kutwa,
Mimi kama mfanya biashara/mjasiriamali mdogo nahitaji mkopo kwa ajili ya kukuzia biashara yangu kiasi cha kuanzia milioni 2
kuna mtu alinishauri niende NMB kisha nifungue account ya mfanyabiashara ambayo inatakiwa iwe na kiasi kisichopungua laki moja muda wote,
then nitumie account hiyo kwa miezi kuanzia 3 kisha niombe mkopo huo ninaotaka eti NMB ndio wana riba ndogo.
lakini pia kuna mtu kanishauri niende AZANIA BANK au CRDB
hivyo najua humu kuna baadhi ya watu wana experience na mambo ya mikopo midogo naomba kuelewa kidogo.
NB; Mimi ni mjasiriamali mdogo na nimesajiri ofisi yangu nna leseni ya biashara na TIN no
na mkopo ninaotaka ni 2 milion basi.!
lakini sina nyumba wala kiwanja eneo hili.
 
Huna chochote cha kuweka dhamana? Jaribu FINCA, dhamana kwa mabenki yetu ndio sifa kuu,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…