Nyankurungu2020
JF-Expert Member
- Oct 2, 2020
- 4,170
- 6,757
Ibara ya 54(2) imetanabaisha wazi kuwa baraza la mawaziri ndio kitakuwa chombo kikuu cha kutoa ushauri kwa rais ili aweze kutekeleza majukumu yake.
Hata kabla ya kumaliza maombolezo tangu afariki hayati Dkt. John Pombe Magufuli tunasikia kauli za kushangaza toka kwa baadhi ya waliokuwa mawaziri chini ya utawala aliouongoza. Na hawa mawaziri walikuwa ni wajumbe wa baraza la mawaziri. Mfano ni Nape Nnauye anadiliki kusema kulikuwa na mapungufu juu ya kusimamia haki za binadamu. Huku mwingine akidai kuwa kama mtaalamu wa tiba kujifukiza hakusaidii kuzuia Covid 19.
Mbali na hayo pia suala la kutumia mitutu ya bunduki kukusanya kodi kupitia task force pia linatia doa awamu iliyopita na sasa tunaona kama limezuiwa mapema kabisa.
Hivyo tunapata picha kabisa kumbe baadhi ya mawaziri waliotumikia awamu ya tano walikuwa wanaona dosari nyingi zikifanyika ila kwa kuona kuwa watawala hawashauriki basi waliamua kukaa kimya japokuwa kwa kinafiki ili mkate upatikane.
N.B Makamu wa rais pia ni mjumbe wa baraza la Mawaziri.
Hata kabla ya kumaliza maombolezo tangu afariki hayati Dkt. John Pombe Magufuli tunasikia kauli za kushangaza toka kwa baadhi ya waliokuwa mawaziri chini ya utawala aliouongoza. Na hawa mawaziri walikuwa ni wajumbe wa baraza la mawaziri. Mfano ni Nape Nnauye anadiliki kusema kulikuwa na mapungufu juu ya kusimamia haki za binadamu. Huku mwingine akidai kuwa kama mtaalamu wa tiba kujifukiza hakusaidii kuzuia Covid 19.
Mbali na hayo pia suala la kutumia mitutu ya bunduki kukusanya kodi kupitia task force pia linatia doa awamu iliyopita na sasa tunaona kama limezuiwa mapema kabisa.
Hivyo tunapata picha kabisa kumbe baadhi ya mawaziri waliotumikia awamu ya tano walikuwa wanaona dosari nyingi zikifanyika ila kwa kuona kuwa watawala hawashauriki basi waliamua kukaa kimya japokuwa kwa kinafiki ili mkate upatikane.
N.B Makamu wa rais pia ni mjumbe wa baraza la Mawaziri.