Ni dr. gani Tanzania anatoa huduma ya IVF (kuwawekea wanandoa mtoto?)

Ni dr. gani Tanzania anatoa huduma ya IVF (kuwawekea wanandoa mtoto?)

mbalaga

Member
Joined
Aug 19, 2013
Posts
16
Reaction score
4
Nimetafuta mtoto mimi na mume wamgu muda mrefu sasa tumeamua kuwekewa mtoto kitaalamu lakini hatujui huduma hii inapataikana wapi na ni sh ngapi? uwezo wa kwenda India na Ulaya hatuna , mwenye taarifa atujuze tafadhali maana tunapendana na vipimo viko ok kwetu sote wawili
 
Ile Clinic ya Premier Care pale karibu na Best Bite Namanga wako vizuri sana issue ya reproductive health. Labda ungejaribu kuwatembelea kama upo Dar.

Inshallah Mungu awajaalie mtoto.
 
Hospitali ipo

Dar ivf center

Karibu na baraka plaza kwenye ile chochoro

Ila kama ungekuwa na hela heri ukafanyie nairobi aisee

Cost kama sikosei $8,000
 
kwa mbegu zako mwenyewe au anonymous donnor?
 
Mbona nmesikia ni sh 20m kufanya hapa bongo.
 
Jamani kumbe ni ghali hivyo; asante Mungu kwa zawadi ya watoto! Poleni sana Mwenyezi Mungu atawasikia.
Salaam ziwaendee wale wote wanaotoa mimba au kutupa watoto.
 
Mtu huona thamani ya kitu pale tu anapokihitaji »»» mabinti wengi wa zama hizi watakushinikiza mkatoe mimba endapo hali hiyo imejitokeza nje ya mpango lakini kuna wanandoa wengi huhangaika kutafuta watoto hata bila kijali ni kwa gharama gani
Poleni sana mleta uzi naamini wanajf watakusaidia taarifa sahihi kama ndo option yenu ya mwisho
 
Pole kwa muhusika kama hujahusika kwenye kuwa chanzo cha hilo tatizo. Ila kama ulikuwa maarufu wa kuzalia kwenye vyoo vya shule muonee huruma Mungu ana wenye natural disasters wengi mno. Ukipita njia ya mikocheni kutokea msasani beach kuelekea posta kuna bango limeandikwa ivf centre. Sina uhakika kama wanafanya kazi hizo ila kuulizia ni bora zaidi.
 
Nenda dar ivf center wapo mikocheni. Gharama inategemea na tatizo lenu. Maana matatizo yanatofautiana. Wengine tatizo ni la mwAnaume wengine ni wote na wengine ni mwanamke. Cha muhimu ni kwenda pale mwenyewe ili upate maelezo yaliyokamilika
 
Poleni sana, ngoja wataalam wengie wakupe options uamue. Asikuambie mtu, mtoto ni raha ya nyumba, na wakikuwa basi furaha inakuwa mara mia mbili. Amini Mungu anaweza na atawapa mtoto kwa kuwa ameahidi katika neno lake kuwa "hakuna atakayekuwa mgumba kati yenu'. Omba kwa kushika neno hilo na Mungu atafanya.Pia waone watumishi wanaoombea wawaombee ila kama mna imani kuwa inawezekana.
 
nairobi wapo vizuri hiyo ya dar siifahamu.jiandae tu kwa gharama coz unaweza ukarudia ivf several times before ikubali
 
asante sana kwa taarifa hii maana hata mie inanifaa mwaya....mwaka wa 6 huu hatujabahatika na tumepima wote hakuna tatizo...wana jf tuombeane jamani!
Ile Clinic ya Premier Care pale karibu na Best Bite Namanga wako vizuri sana issue ya reproductive health. Labda ungejaribu kuwatembelea kama upo Dar.

Inshallah Mungu awajaalie mtoto.
 
asante sana kwa taarifa hii maana hata mie inanifaa mwaya....mwaka wa 6 huu hatujabahatika na tumepima wote hakuna tatizo...wana jf tuombeane jamani!

pole sana , wish ningekusaidia ila huo muda wa kukaa na wewe kwa karibu kudiscuss nahisi kama umeshaonana na

madaktari wengi zaidi.......

ila kama wote hamna tatizo jaribuni kuchukua likizo kwa pamoja msafiri sehemu kwa mapumziko huku mkijaribu kukutana siku za ovulation.......

usipokuwa umerelax pia ni tatizo besti...........
 
asante sana my dear...tunaweza kudiscuss tu ukatusaida maana nimechoka upweke huu kwa kweli.
pole sana , wish ningekusaidia ila huo muda wa kukaa na wewe kwa karibu kudiscuss nahisi kama umeshaonana na

madaktari wengi zaidi.......

ila kama wote hamna tatizo jaribuni kuchukua likizo kwa pamoja msafiri sehemu kwa mapumziko huku mkijaribu kukutana siku za ovulation.......

usipokuwa umerelax pia ni tatizo besti...........
 
Back
Top Bottom