Ni halali SUA kuwa na TV au kiwanda cha maziwa?


unajidanganya mkubwa hakuna mhitimu wa SUA atakaeathirika tusubiri tuone mashine zipo kwa ajili ya masomo kwa vitendo kama unaona biashara ya maziwa na nyama inalipa ni bora ukawekeza wewe suala la coverage lisikusumbue kwani hata ikionekana katika tarafa moja inatosha hata hiyo TBC haionekani kote siwezi pia kukulazimisha kuwa kuamini kuwa kuna tafiti ambazo matokeo yake yanasambazwa kupitia SUA TV kwa sababu inaonekana hujataka kutafuta ukweli wa hili kabla hujapost nakushauri tembelea hapo SUA tv ukapate ukweli
 

hivyo ndo unavyo ona wewe lakini jaribu kuwa na mtazamo wa mbali kidogo, ukweli ndo huo graduate wa SUA hawawezi ku compite hata kidogo na wenzao wakenya hili ni tatizo na ushahidi upo, wewe kama waona wazo langu halina maana toa wazo mbadala lengo ni taifa letu lisonge mbele,,,,,,,,kwama wewe ni mfuatiliaji mzuri wa mambo VETA walikuwa na wazo la kuanzisha kozi za hoteli na utalii, kabla wamejenga chuo kikubwa na hotel kubwa tu Arusha kwajili ya mafunzo kwa vitendo sasa kuwashauri SUA wewe na kiwanda cha maziwa na nyama unaona wazo finyu sijui wewe unamtizamo gani
 

Wakifanya hizo kazi hakitakuwa tena chuo, chuo ni sehemu ya kutoa knowledge na kusolve matatizo ya viwandani na mashambani ni kwingineko a si ku invest
 

Binafsi ninakushangaa - Prodigal Son - kama kweli wastahili kuwa na jina hilo. Kwa ninavyoelewa mimi, Prodigal Son ni kijana ambaye ana upeo mkubwa wa kuona mbali, jambo ambalo, kama ungetafakari kwa kina ungeelwa SUA wana mtazamo gani kwa kuanzisha hiyo TV. Kwa kuwa sikuwa na taarifa kwamba tayari imeanzishwa, nawapa pongezi kwa kufanya hivyo.

Suala ni, kwa nini SUA wameanzisha TV BADALA YA kiwanda cha maziwa, kama unavyotoa hoja yako.

Ndio, SUA ni chuo kikuu cha kilimo, na iko kwenye mantiki yao kuwa na kiwanda cha maziwa. Je, unafahamu kama kiwanda hicho - hata kama kina uwezo mdogo - kipo au hakipo?

Kuhusu kwa nini SUA wameanzisha kituo cha TV, jibu lake ni rahisi sana. Kama nyote mnavyoelewa, kwanza, wataalam wa ugani (agricultural extension officers) ni wachache sana nchini mwetu, na hata hao wanaosomea fani hiyo, wengi wao hukimbia kwenda mikoani wanapopangiwa, kwa kuwa wanaona kwamba mikoani kuna hali duni ya maisha. Kwa hiyo, wataalam wa SUA wameona kwamba, kituo hicho cha TV kinaweza kutoa mafunzo na/au maelekezo ya ugani, ili kuwafundisha wakulima kilimo cha kisasa, kwa kuwa TV inaweza kuonekana mbali zaidi na kuwafikia watu wengi zaidi, kuliko uwezo mdogo wa maofisa ugani.

Suala la kwamba TV hiyo haionekani kila mahali ni la kisheria zaidi. Kwa mujibu wa sheria ya mawasiliano, inayosimamiwa na TCRA, kila anayeanzisha kituo cha redio na/au TV, anapewa leseni ya muda ya kutangaza kwenye kiwango kinachoitwa District, yaani, ndani ya wilaya yake tu, kwa muda wa mwaka mmoja. Hii inawekwa kwa sababu ya angalizo; je, mtangazaji na uwezo wa kudumu katika soko? Je, vipindi vinavyoandaliwa vina manufaa yoyote yale kwa jamii na havikiuki maadili ya Kitanzania? Haya ni baadhi tu ya mambo ambayo TCRA wanayapima na kuyafuatilia, kwa muda wa mwaka mmoja, kabla ya kukaa kikao na kutoa leseni mpya inatakayomwezesha mtangazaji kufika nchini kote.

Kaka, kama ulikuwa huelewi ni kwa nini SUA-TV haionekani kila mahali, ungeuliza, kuliko kukurupuka na kuanza kubwabwaja maneno yasiyo na msingi.

Kuuliza si ujinga. Ficha upumbavu wako, usifiche hekima zako.

./Mwana wa Haki

P.S. SUA wanapaswa kuwa na TV PAMOJA NA kiwanda cha maziwa. Lakini wapo wawekezaji ambao wanaweza kuwekeza kwenye kiwanda. SUA ni wataalam wa kilimo, TV itasaidia kuwafundisha Watanzania kuhusu ukulima wa kisasa! Bila elimu, Kilimo Kwanza HAITAFANIKIWA! Tumaini University, nanyi mmejiandaaje kuwapa wananchi mnachofundisha?
 

naoona wewe ndo umekurupuka tena kabisa,mimi hii hoja ninayo ni zaidi ya miaka mitatu kama sio 4,na kabla sijaiweka hapa nilitafiti vyuo vingine kama SUA wanafanya nini hapa nazungumzia Kenya na Uganda, na kwa bahati nzuri nilishafika nikajionea mwenyewe shughuli mbalimbali za kilimo zinavyotiwa chachu na hivi vyuo specifically na zungumzia Egarton na Makerere shule yao ya kilimo, Uganda kwa ukanda wa kusini wameshafanya mapinduzi ya namna bora za kufuga hata Mh JK ametuma baadhi ya maofisa wa wilaya ya Ngorongoro wakajifunze, je SUA wakowapi??? TV ya SUA ipo hewani zaidi ya miaka 4 sasa hata mkoa wa pwani haionekani,unachozungumza kuhusu TCRA umekosea tena kabisa, Hoja yangu ni kwamba KIPAUMBELE kwa SUA ingekuwa TV au mambo yanayoendana na wanayofundisha??? ku question my credibility kwenye hii hoja yangu unakosea nilitegemea na wewe ungeleta mawazo chanya lengo ni secta ya kilimo iendelee na ichangie pato la taifa, binafsi nimeona kiwand acha maziwa kingetumiwa kama maabara na wanafunzi na kingeamsha ari ya ujasiriamali kwa wanafunzi waliowengi at the some time kuopatia chuo kipato na kuondokana kwa kiasi na utegemezi wa serekali kuu kwa kila kitu, kama SUA walitaka mambo yao yajulikane wanaweza itumia TBC, na ukumbuke SUA hawataweza kuwa na TV itakayoonekana nchi nzima uendeshwaji wake ni hawataweza wangekuwa wanatengeneza vipindi na kurushwa na TBC walau lingeingia akilini,


Ushauri: jubu hoja kwa hoja na ikiwezekana tafiti walau hata kidogo au usome na uelewe mada kabla hujaanza kutuhumu,
 
SUA wanahitaji vyote,kiwanda cha maziwa na TV kama inao uwezo. Hili ni wazo tu,lakini siyo lazima wawe na kiwanda cha maziwa. Mwingine anaweza kusema kwanini wasiwe na shamba la maua,mwingine kwanini wasianzishe shamba la mahindi,mwingine kwanini wasianzishe shamba la kahawa. Mwisho wa siku wataacha kazi yao ya msingi (Utafiti na kufundisha).

LAzima kuwe na mgawanyo wa kazi,SUA watafiti na wafundishe watu wa kwenda kwenye industry. Wapo kufanya practice ya wanachofundisha haitakiwi iwe kwa kiasi kikubwa sana ili kuwafanya waconcentrate na kazi yao ya msingi.
 

Prodigal Son,

Hoja zako zinaweza kuwa nzuri sana ila jinsi ulivyoziwasilisha ndo kuna tatizo. Pia kuna ombwe katika ufahamu wako wa SUA. Kwa hiyo labda ungeleta hoja zako kama unayetaka kuelimishwa ili wadau wenye uelewa wakusaidie.

1. SUA TV ilianzishwa mapema kwenye miaka ya 1990 (kitu kama 1994) baada ya kuwekewa Satellite Dish na wafadhili na wakati huo walikuwa wanatumia channels za MNET na Supersport (bure). TV ililenga kutoa burudani na elimu kwa wanajimii wa SUA. Hata hivyo wakazi wanaoishi jirani waliweza kufaidika nayo. Baada ya Abood kufungua TV mwishoni wa miaka ya 90 (nadhani ilikuwa 1997) kulizuka ushindani kwani Abood alitaka kutumia channels za MNET na Supersport kwa hiyo SUA wakapoteza hiyo nafasi. Pia nadhani na masharti ya kisheria yalibanwa ikabidi waombe leseni ya kuendesha TV rasmi. Kwa hiyo walianza kuandaa vipindi vyao na kurusha. Na kama walitaka taarifa iende bali walishirikiana na vituo vingine nje ya Morogoro. Kwa hiyo unaweza kuona nini kilikuwa chanzo za SUA kuanzisha TV. Na kwa vile hiki chuo kinalo jukumu kubwa la kutoa elimu, sioni kama ni kosa kumiliki TV.
2. Kuwa na viwanda au la siyo kazi yao na wala haimo kwenye majukumu yao (SUA's mandates). Kwa hiyo wanapohitaji kufundisha kwa vitendo wanajua nini wafanye.
3. Mambo ya kuwa na mashamba ya Ng'ombe au mimea ya mfano nadhani hujui unachokisema. Kabla ya Utandawazi SUA ilikuwa na mashamba mazuri sana. Lakini ng'ombe wazuri wate walichukuliwa na viongozi wa serikali na chama (CCM) kila walipopata nafasi ya kutembelea chuo. Kwa sasa hayo mashamba ni magofu.
4. Ungekuwa karibu na vyuo usingesema hayo unayoyasema. Huwezi kuamini kwamba kwa sasa vyuo vikuu ikiwemo SUA wanapewa bajeti ambayo hata haitoshi kununua karatasi achia mbali vifaa vya maabara n.k. Sina hakika kama wanapewa hata senti moja na serikali kwa ajili ya utafiti. Hali ni mbaya sana. Kuna taasisi moja ilikuwa inapewa Ths 3bn za utafiti kwa mwaka hadi 2005 ila kwasasa wanapata sifuri (zero or 0).

Naomba tusiwe wepesi wa kulalamika na kulaumu bila kujua ukweli wa mambo. Hata ng'ombe hawezi kutoa maziwa bila kulishwa kwanza.
 
Si chuo tu muzee, kama kawaida yetu........ WIZARA NYINGI ZIMESHAWAHI KUONGOZWA NA MAWAZILI HAMBAO HATA TAALUMA RASMI YA WIZARA HIYO HANA........
 

Mimi sioni tatizo lolote SUA kuwa na huduma ya TV, labda tatizo ni kwamba kama mradi huo hauko kwa manufaa ya kuwaelimisha watanzania hapo ndipo naweza kuwa na wasiwasi na kujiuliza kwa nini wasingekuwa na mradi mwingine tofauti na huo. Suala la TV ya SUA kutoonyeshwa sehemu zote za Morogoro inaweza ikawa ni kwa sababu ya masuala ya kisheria kwamba hayo maeneo inapoonekana tu ndiyo yanaruhusiwa kisheria, lakini pia inawezekana ni kwa sababu ya kukosa umakini wa watendaji wanaohusika na uendeshaji wa TV hiyo.

Hivyo, kama ni kukosa umakini kwa watendaji, basi hata wangekuwa na kiwanda kisingeweza kuleta matokeo yaliyokusudiwa. Suala ninaloliona kwetu sisi watanzania, wengi wetu hatuka makini kusimamia vitu tunavyojipangia kuvifanya. Hatuna uzalendo, tunatanguliza ubinafsi zaidi kuliko manufaa ya umma. Hadi hapo tutakapoachana na tabia hiyo mbaya na adui wa maendeleo ya wengi, hatuwezi kufika popote hata kama ni kuwekeza katika viwenda kama ulivyotolea mfano vya maziwa na nyama.

Hivyo, TV SUA si kosa kuwa nayo, lakini pia miradi wa viwanda vya maziwa na nyama inakaribishwa kwa lengo moja tu la kubadilisha maisha ya watanzania kiuchumi na kijamii. Watanzania wanahitaji kuhabarishwa kuhusiana na masuala ya kitaalamu ya kilimo. Viwanda kama vya maziwa na nyama navyo ni vyema kuwa navyo pale kwa nia njema tu ya kutoa elimu zaidi na hata kuongeza kipato cha chuo na lishe nchini. Hata hivyo inategemea na upatikanaji wa soko la bidhaa zinazotarajiwa kupatikana kutokana na viwanda hivyo. Kwa mfano, ni watanzania wangapi waonao uwezo na utashi wa kula nyama kwa siku? Maziwa ya kopo na pakiti yananywewa kwa kiwango gani nchini mwetu? Soko hilo liko wapi (mikoa gani hasa)? Hivyo, kwa kutoa mfano wa Kenya inaweza kuwa ni upotoshaji kwa maana tu ya kibiashara maana ni nchi tofauti zenye watu wenye tamaduni tofauti hasa katika ulaji na kipato pia!!!
 
ukienda site ya TCRA utapata habari zaidi kama ni halali au la.kwa wenzetu unakuta kuna TV za manispaa (hapa ipo ya Iringa tu) ma timu ya mpira wa miguu ,kikapu nk wanakuwa na TV zao.hata ulianzisha hii mada waweza fungua ya kwako ukifata masharti
 

ndio ni halali
 
ukienda site ya TCRA utapata habari zaidi kama ni halali au la.kwa wenzetu unakuta kuna TV za manispaa (hapa ipo ya Iringa tu) ma timu ya mpira wa miguu ,kikapu nk wanakuwa na TV zao.hata ulianzisha hii mada waweza fungua ya kwako ukifata masharti

Tungejaribu kulifikiria in terms of vipaumbele nadhani tungekuwa na conclusion nzuri,sishangai hata jiji la DSM na wao wako mwishoni kuwa na TV yao lakini nachojiuliza kila siku nini kipewe kipaumbele kwanza hili linatokana na yanayofanyika vyuo vingine ambavyo vinatoa mafunzo yanayofanana na yanayotolewa na SUA.
 

Mkubwa Prodigal Son
Hatuko sote mkubwa kwa hili japo naheshimu mawazo yako. SUA kuanzisha kituo cha TV kwa mawazo yangu bado wako sawa kabisa, kama kituo hicho kitatumika kama njia mojawapo ya kuwafikia wadau wake kwa haraka na mapana! Pile kama chuo kinatakiwa kiwe na njia za kujiingizia mapato na kwa kutumia TV wanaweza kuuza matangazo yao kwa makampuni mbali mbali na waki-ingiza pesa ya kuendesha chuo chao, linaweza lisionekane hili leo lakini kesho kutwa likawa jambo zuri, la maana hapa ni kwamba wamejiandaaje katika siku zijazo? Kuna vyuo vingi vyenje radio,magazeti, tv , tovuti na njia mbadala za mawasiliano si geni hili. Fikiria ni kiasi gani cha pesa kinaenda kuendesha SUA kwa mwaka, na kama wao SUA wataweza kupungunza utegemezi kwa serikali japo kwa asilimia 50, hizi pesa zitaweza kupunguza umasikini kwa kiwango gani?
Kuhusu viwanda vya maziwa na vinginevyo bado wapo sahihi kabisa kama wataanzisha, kwa chuo kilicho makini hakipimwi kwa idadi ya machachipo (publications) tu bali kwa product wanazotengeza kusadia kuinua khali ya wananchi wao. Kwa maana hii leo hii wakianza kuuza mayayi au njiwa ili kuinua lishe ya watanzania walio wengi nakwa upande mwingine kuongeza kipato chao tunatakiwa tuwape hongera.
 


binafsi nataka kuwapa changamoto kwani garama za kuendesha TV ni kubwa na hawana uwezo wa kuifanya hiyo TV ionekane TZ nzima na wadau wa SUA ni watanzania wote, na isitoshe hiyo tv haihusiani na kinachofundishwa SUA, wangejaribu kufikiria kwa kwenda mbali kidogo kuwa na mradi ambao mbali na kuwaingizia kipato wanafunzi wangepata sehemu ya kujifunzia kwa vitendo,

Hili linawezekana kwani SUA wanaweza wakaingia ubia na mtu binafsi au hata kampuni ilikuanzisha project zinazoendana na masomo wanyofundisha, hili linawezekana kwa kenya na uganda wameweza kufanikiwa saana na kupunguza utegemezi kutoka serekalini
 
SUA kuwa na Tv ni jambo jema, kwani utafiti wanaoufanya wanaweza kutumia TV yao kufundisha wakulima, wafugaji na wananchi kwa ujumla mambo mema waliyotafiti yanayofaa kwa Tanzania
 
Kwa wanaoijua vyema SUA, kuna ranch ya mfano ya ng'ombe na mbuzi wa kisasa wa maziwa (MAGADU FARM). Pia dept ya animal science kuna mradi mdogo wa kusindika maziwa. Wanafunzi huwa wanatumia hiyo ranch kujifunza mengi. Sidhani kama kuna umuhimu wa kuwa na kiwanda cha kusindika nyama/maziwa ilhali kuna Magadu farm ambako wanafunzi wanaweza kujifunza kwa vitendo pia. SUATV inaweza kuwa imezingatia kipaumbele cha kuelimisha na kufikia wakulima kwa wingi. Vinginevyo,je unazungumzia vyuo vikuu kujikita zaidi katika uwekezaji kulingana na fani wanayofundisha..?
 

wonderfull observation, you have my big thank you.
 
Watanzania, by our majority, ni watu wasio na ubunifu mkubwa. Prodigal Son just proves my point!

Kwa nini SUA wasiwe na TV? Kilimo Kwanza itatekelezwa vipi bila ya wakulima - ambao ndio walengwa - kufahamu nini maana ya ukulima wa kisasa? Hakuna Extensions Officers wa kutosha, SUA watatumia TV kuwafundisha wakulima. That is just ONE justification for the TV!

Let's start thinking outside of the box, people!

Happy New Year!
 


Kaka ubunifu gani kwa mtizamo wako wakulima wa tanzania wanaishi sehemu ya morogoro tu, kumbuka tv yenyewe hata morogoro yote haionekani, mulima wa mawese kigoma atanufaika na SUA TV kivipi???then kumbuka kuifanya hiyo tv ionekane tz nzima ni garama saana kitu ambacho SUA hawana uwezo,na Extensions Officers unaowazungumzia kama wapo maeneo yote je wana hizo TV na umeme UPO???? huko wanakoishi???? watu kwa kukurupuka hamjambo,,, kama ni kuelimisha wanaweza kushirikiana na TBC abayo inaonekana TZ nzima na kutengeneza vipindi vya kuelimisha hao wakulima unaowazungumzuia wewe. my concern ni jinsi wa tz tulio wengi tunashindwa kuwa na vipaumbele

kama wewe ni mtu unayependa kudodosa mambo ungejaribu kuangalia How Makerere University agriculture school yao walivyosaidia kufanya mordenisation ya ufugaji na kilimo maeneo ya Toro kingdom, kasese, mbarara nk. Also unaweza ukajifunza also chuo kikuu cha kilimo cha Egarton cha kenya wamefanya nini kuhusu kilimo, from there ndo u conclude kwamba hii mada yangu sio ya kibunifu,,

binafsi changamoto nayoipa SUA wabadilike waingie mikataba na private individuals au kampuni wawe na miradi itakayo waingizia kipato na kupunguza Utegemezi wa serekali kuu,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…