Ni huduma gani ya Serikali ambayo ungependa iwe kwa njia ya mtandao?

Ni huduma gani ya Serikali ambayo ungependa iwe kwa njia ya mtandao?

mwananchi01

New Member
Joined
Aug 20, 2022
Posts
1
Reaction score
4
Binafsi nimekaa na kutafakari sana kuhusu Serikali yetu inapambana kuanzisha mifumo ya kielektroniki ili kurahisisha utoaji wa huduma zake. Mimi pia nimenufaika moja kwa moja kwa jitihada hizi maana napata/nalipia huduma za Serikali kwa njia rahisi sana huku nikiwa naendelea na shughuli zangu.

Mambo ya kwenda kwenye taasisi za serikali kupanga foleni ili kulipia huduma mbalimbali kama kodi ya ardhi, umeme, maji, n.k nimeshasahau kabisa. Napata bili zangu kwa USSD (*152*00#) au kwakutumia App ya GePG TANZANIA kirahisi kabisa.

Lakini inaonesha bado kuna taasisi chache ambao huduma wanazozitoa unaweza kuzipata bila kwenda kwenye taasisi hizo lakini kwa utaratibu wao wanalazimisha mpaka ufike ofisini ndiyo upatiwe huduma ambayo kwa mtazamo wangu haijakaa vizuri, maana inakupotezea muda na kukuongezea usumbufu bila sababu.

Taja taasisi ya Serikali ambayo inafaa iboreshe huduma zake ziendane na zama za sasa za Sayansi na Teknolojia.
 
TANAPA na NCAA kwenye mageti makuu hasa wakati wa kutoka, watu wengescan tu permit watoke
Kwa sasa hivi ni hadi watu wapange foleni eti upigiwe muhuri, wasaini out manually na hii ndio inaleta msongamano kwenye mageti hasa Loduare na Nabi
Na mtu akilipia kitu cha ziada mfano crater service; angeweza tu kuscan getini na kupita tofauti na sasa ni hadi mtu aende ofisini kwao; yaani wanatumia system ya Mwalimu Nyerere ambayo ilikuwa inaendana na magari labda 50 kwa siku na sio sasa hivi................. hata sijui wanafaidika na nini kwa hiyo local system
 
Tanapa waweke hotel za chakula za kawaida na wauze nyama poli.

Ndiyo tutaona nia ya kweli ya kuhamamasisha wazawa kwenda kupata huduma pale.
 
Kwanza nikupongeze kwa kuwaza kwa sauti, na niipongeze serikali kwa hatua bora zinapunguza urasimu kwa kiasi kikubwa, binafsi huduma zote zinazohusiana na aridhi(ie kupimiwa, kupata hati mpaka kodi ya aridhi) zingepelekwa kielektroniki ASAP.
 
TRA kama mpo humu, tafadharini sana! Fanyeni utaratibu wa kutoa contol number ya malipo ya kodi kwa njia ya sms kupitia simu za mkononi.

Huu utaratibu wa walipa kodi kuwafuata ofisini kwenu, na kupanga foleni ili kupata hiyo control number ya kwenda kulipia mapato; unakera! Lakini pia ni utaratibu uliopitwa na wakati. Yaani hela ya kwangu, bado mnanitesa kukaa foleni!!

Mnashindwa hata kuwaiga wenzenu wanaohusika na maji! Kwanza wakija kusoma mita, wanakutumia ujumbe na baadaye wanakutumia bill, na control number ya malipo.

Ukichelewa ndani ya miezi 3, wanakukatia maji! Na hapo ni baada ya kukutumia ujumbe wa kutosha kupitia simu yako ya mkononi.
 
TRA makadirio ya kodi na ulipaji wa kodi ufanyike kwa mitandao kuepuka mazingira ya mipigo na vitisho
 
Nikikumbuka mtiti wa kuchukua na kurudisha fomu za kugombea ubunge n udiwani 2020 kwa vyama vya upinzani ,,,da Bora huduma hiyo itolewe kwa njia ya mtandao. Mambo ya kurudisha fomu unakuta mkurugenzi kashasepa kwa makusudi. Upo ushetani ulifanywa na JPM mmoja wapo ndio huo.
 
Nikikumbuka mtiti wa kuchukua na kurudisha fomu za kugombea ubunge n udiwani 2020 kwa vyama vya upinzani ,,,da Bora huduma hiyo itolewe kwa njia ya mtandao. Mambo ya kurudisha fomu unakuta mkurugenzi kashasepa kwa makusudi. Upo ushetani ulifanywa na JPM mmoja wapo ndio huo.
Hili jambo ni kweli kbsa , waweke iwe online tu
 
Mada nzuri Sana , majibu mengi wengi wamejibu
Kwenye ardhi,
LAKINI JAMBO AMBALO BINAFSI NAPENDA LIFANIKIWE NI KUNUNUA KWA KUTUMIA MTANDAO
YAAN PAPERLESS MONEY,.
NIKITAKA BATI AU NONDO CEMENT AU CHOCHOTE KILE NA PURCHASE KWA SIM KODI YANGU INAKATWA JUU KWA JUU,

HILI JAMBO NAOMBA MUNGU SIKU ZOTE SIKU MOJA LIWE HALISI
 
TRA kama mpo humu, tafadharini sana! Fanyeni utaratibu wa kutoa contol number ya malipo ya kodi kwa njia ya sms kupitia simu za mkononi.

Huu utaratibu wa walipa kodi kuwafuata ofisini kwenu, na kupanga foleni ili kupata hiyo control number ya kwenda kulipia mapato; unakera! Lakini pia ni utaratibu uliopitwa na wakati. Yaani hela ya kwangu, bado mnanitesa kukaa foleni!!

Mnashindwa hata kuwaiga wenzenu wanaohusika na maji! Kwanza wakija kusoma mita, wanakutumia ujumbe na baadaye wanakutumia bill, na control number ya malipo.

Ukichelewa ndani ya miezi 3, wanakukatia maji! Na hapo ni baada ya kukutumia ujumbe wa kutosha kupitia simu yako ya mkononi.



Mbona imekuwa ikifanyika hivyo kwa miaka mingi ?
 
Mbona imekuwa ikifanyika hivyo kwa miaka mingi ?
Huu mfumo wao unatakiwa ubadilike. Wawe na control number moja tu ya malipo ya serikali. Na mlipa kodi atumiwe kupitia namba yake ya simu wakati ukifika wa kulipa kodi.

Hakuna sababu ya msingi ya kwenda kupanga foleni kila baada ya miezi 3 ili kupewa hiyo Control Number. Idara nyingi za serikali zilishaondoka kwenye huu urasimu.
 
TRA makadirio ya kodi na ulipaji wa kodi ufanyike kwa mitandao kuepuka mazingira ya mipigo na vitisho
Unakuta mtu anatumia EFD machine, records za mauzo yake kwa mwaka uliopita TRA wanayo kwenye systems zao. Ni kiasi cha kukadiria mapato ya mwaka huu, basing on last year sales, then wanakutumia kwenye simu, kama mteja ukitaka kulipa una request control number, unaingiza amount unataka kulipa, unaipata unalipa kwa simu, sms ya risiti una print unatunza.

badala yake kila.mwanzo wa mwaka inabidi uende TRA upoteze muda kibao na on top of that upewe vitisho kibao, utoe rushwa kidogo, ndio ukadiriwe. Ukitaka kulipa, ukapange foleni tena. inakera sana kwakweli.

Maafisa wa kukadiria kodi wanajua kabisa kuwa mwanzo wa mwaka ni muda wao wa kutengeneza hela, kwa rushwa. Wanaudhi sana. utatafutiwa sababu mpaka utanasa tu.
 
Unakuta mtu anatumia EFD machine, records za mauzo yake kwa mwaka uliopita TRA wanayo kwenye systems zao. Ni kiasi cha kukadiria mapato ya mwaka huu, basing on last year sales, then wanakutumia kwenye simu, kama mteja ukitaka kulipa una request control number, unaingiza amount unataka kulipa, unaipata unalipa kwa simu, sms ya risiti una print unatunza.

badala yake kila.mwanzo wa mwaka inabidi uende TRA upoteze muda kibao na on top of that upewe vitisho kibao, utoe rushwa kidogo, ndio ukadiriwe. Ukitaka kulipa, ukapange foleni tena. inakera sana kwakweli.

Maafisa wa kukadiria kodi wanajua kabisa kuwa mwanzo wa mwaka ni muda wao wa kutengeneza hela, kwa rushwa. Wanaudhi sana. utatafutiwa sababu mpaka utanasa tu.
mambo ya hela yakishakua na watu wengi kwenye process lazima upigaji uwepo mwingi
 
Back
Top Bottom