Ni ipi faida ya kuwa Wakala wa Tigopesa

godfrey_avya

Senior Member
Joined
Feb 25, 2014
Posts
131
Reaction score
24
Wakuu ninahitaji kuanza kazi hii hivyo anaye waza kunin'gmulia hili.....

Karibu
 
Kila kitu kina faida na hasara zake, japo siwezi kukupa jibu la swali lako, lakini tambua mjasiriamali lazima awe "RISK TAKER" hivyo we jaribu tu utaona matokeo yake. Jambo la msingi ni kuhakikisha una weka biashara yako mahali penye soko, pia pasiwe penye competition kubwa, na uwe mbunifu zaidi. Utatoka tu ndugu yangu.

Lakini ukisema uulize faida utapewa majibu kulingana na mtu, mwingine kashindwa biashara mwenyewe basi ataponda tu, mwingine hajui lolote ila kwakuwa ana chuki zake na watu wa tigo basi ataponda tu. We tambua biashara ambayo unaona watu wanafanya kila siku hiyo ina faida, ila ni muhimu uwe na ufahamu wa biashara walau kidogo, iwe kwa kusoma darasni, au kwa ufahamu wa kawaida tu, au hata kufundishwa kwa namna yoyote itasaidia zaidi.
 

ushauri huu unatosha nazan mm sina la kuongezea
 
Wakala bado hujajibu sawa sawa swali la mleta mada.
Umetoa maelezo ya jumla jumla sana tena kuhusu suala la biashara, sio specific kwa biashara hii. Mbaya zaidi unamshawishi aamue tu kufanya au kutokufanya lakini imwambii kwanini.

Mleta mada anatamani kufahamu mambo ya msingi na mahususi kuhusu biashara hiyo.
Kwa mfano
1/Msingi wa faida ya biashara ya simu-money(Tigo Pesa, M-Pesa, Airtel money) inapatikana vipi? Ni kiasi gani?
2/Namna gani ninaweza kutengeneza faida zaidi katika hiyo biashara?
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…