Ni ipi nafasi ya mama na mke katika maisha ya mume

Ni ipi nafasi ya mama na mke katika maisha ya mume

Etugrul Bey

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2020
Posts
6,514
Reaction score
15,247
Hakika hawa wanawake wawili ni watu muhimu sana katika maisha ya mume, lakini kila mmoja mara nyingi huwa anahitaji kuwa chaguo la kwanza, na hapo ndipo shida inapoanzia.

Nadhani mara nyingi tumeshawahi shuhudia ima kwa majirani au kwa ndugu zetu,jinsi wanawake hawa muhimu wanavyo chachafya ndoa nyingi.

Na wakati mwingine tumeshawahi kuona katika clip au video mbali mbali,jinsi wakati mwingine wanawake hawa ambao ni vipenzi kwa mume, wakigombea kukaa sita ya mbele kwenye gari. Inaweza isiwe hivyo katika picha halisi, lakini inaonyesha jinsi wanawake hawa wanavyoweza kuwa paka na panya katika maisha ya mwanaume.

Maana mama anaona anastahili kupata mema ya mwanae kama mzazi,na huku mke anaona anastahili kupata mema kama kipenzi na tamu ya mume.

Sasa mwanaume hapa unatakiwa uwe na busara na hekima kubwa sana,hutakiwi kuwaonyesha mbele yao,nani ana hadhi kubwa kuliko mwingine, ila ukiwa na mmoja wao kwa wakati wake muonyeshe yeye ndio kila kitu kwako.

Yaani unatakiwa uwe na akili kubwa ya kudili na hawa wanawake muhimu katika maisha yako,natambua mama ndio kila kitu,lakini kumbuka hata mkeo nae ana nafasi yake, sikwambii kwamba umpe kipaumbele mke kuliko mama laa! Ila usimfanye akaona wazi kuwa yeye hana thamani kwako.

Lingine hili lipo kidini zaidi,usimnyanyase mke kwa ajili ya mama yako, yaani iko hivi, majukumu ya mama yako ni yako na si ya mke, yaani isifike kipindi mke akaona kero kwa kuwa unamshinikiza sana amjali mama yako,ingawa kihekima na busara huyo ni mama yake pia,lakini kiuhalisia ana mama yake huko kwao

Na wakwe najua kuna baadhi yenu mko humu,sio busara kuingilia ndoa za watoto wenu kisa tu wewe ndio ulimzaa huyo mtoto wa kiume ambaye ni mume wa mkweo, maana kuna ile kauli "je nisingemzaa ungempata huyo?" Wewe ulishamzaa basi inatosha, waache wengine wamtumie.

Na wake nanyi, sio kwasababu huyo mume ndio tamu yako,basi ukajisahau na kuona huyo mumeo hana mama, tambua kama unavyo mthamini mama yako, mumeo nae anamthamini mama yake vile vile, kwahiyo msitake kuchukua nafasi ya mama yake, hamtaweza abadani.

Nawaaibia siri ila msimwambie mtu! Jipendekeze kwa mama wa mumeo hata kinafiki,kwanza mama atakupenda, na mume pia atakupenda.

Ni hayo tu!
 
UKiona mtu anamshindanisha mama na mke wake nani ana hadhi kubwa basi ujue huyo mtu ni mbwa tu hana akili,

Kila mtu ana majukumu yake, ana nafasi yake ambae haiingiliani na mwenzake, ila wote wana umuhimu sawa kwenye maisha ya mtu,

Ni sawa na useme kati ya kipa na striker uwanjani nani wa muhimu zaidi?


Ni machizi tu ndio wanaweza uliza swali kama hilo,
 
UKiona mtu anamshindanisha mama na mke wake nani ana hadhi kubwa basi ujue huyo mtu ni mbwa tu hana akili,

Kila mtu ana majukumu yake, ana nafasi yake ambae haiingiliani na mwenzake, ila wote wana umuhimu sawa kwenye maisha ya mtu,

Ni sawa na useme kati ya kipa na striker uwanjani nani wa muhimu zaidi?


Ni machizi tu ndio wanaweza uliza swali kama hilo,
Mada iishie hapa au Mleta Mada Una lolote la kusema?
 
Hakika hawa wanawake wawili ni watu muhimu sana katika maisha ya mume, lakini kila mmoja mara nyingi huwa anahitaji kuwa chaguo la kwanza, na hapo ndipo shida inapoanzia.

Nadhani mara nyingi tumeshawahi shuhudia ima kwa majirani au kwa ndugu zetu,jinsi wanawake hawa muhimu wanavyo chachafya ndoa nyingi.

Na wakati mwingine tumeshawahi kuona katika clip au video mbali mbali,jinsi wakati mwingine wanawake hawa ambao ni vipenzi kwa mume, wakigombea kukaa sita ya mbele kwenye gari. Inaweza isiwe hivyo katika picha halisi, lakini inaonyesha jinsi wanawake hawa wanavyoweza kuwa paka na panya katika maisha ya mwanaume.

Maana mama anaona anastahili kupata mema ya mwanae kama mzazi,na huku mke anaona anastahili kupata mema kama kipenzi na tamu ya mume.

Sasa mwanaume hapa unatakiwa uwe na busara na hekima kubwa sana,hutakiwi kuwaonyesha mbele yao,nani ana hadhi kubwa kuliko mwingine, ila ukiwa na mmoja wao kwa wakati wake muonyeshe yeye ndio kila kitu kwako.

Yaani unatakiwa uwe na akili kubwa ya kudili na hawa wanawake muhimu katika maisha yako,natambua mama ndio kila kitu,lakini kumbuka hata mkeo nae ana nafasi yake, sikwambii kwamba umpe kipaumbele mke kuliko mama laa! Ila usimfanye akaona wazi kuwa yeye hana thamani kwako.

Lingine hili lipo kidini zaidi,usimnyanyase mke kwa ajili ya mama yako, yaani iko hivi, majukumu ya mama yako ni yako na si ya mke, yaani isifike kipindi mke akaona kero kwa kuwa unamshinikiza sana amjali mama yako,ingawa kihekima na busara huyo ni mama yake pia,lakini kiuhalisia ana mama yake huko kwao

Na wakwe najua kuna baadhi yenu mko humu,sio busara kuingilia ndoa za watoto wenu kisa tu wewe ndio ulimzaa huyo mtoto wa kiume ambaye ni mume wa mkweo, maana kuna ile kauli "je nisingemzaa ungempata huyo?" Wewe ulishamzaa basi inatosha, waache wengine wamtumie.

Na wake nanyi, sio kwasababu huyo mume ndio tamu yako,basi ukajisahau na kuona huyo mumeo hana mama, tambua kama unavyo mthamini mama yako, mumeo nae anamthamini mama yake vile vile, kwahiyo msitake kuchukua nafasi ya mama yake, hamtaweza abadani.

Nawaaibia siri ila msimwambie mtu! Jipendekeze kwa mama wa mumeo hata kinafiki,kwanza mama atakupenda, na mume pia atakupenda.

Ni hayo tu!
unamlinganisha mama na vitu vya ajabu
 
Mke anapendwa kimahaba na mama anapendwa kama mzazi. Yaani mapenzi ya mke yanaitwa "EROS" na mama yanaitwa "STONGE", hiyo ni kwa mujibu wa wanafalsafa wa Kigiriki waligawa mapenzi katika sehemu kuu 5.
Kuna mijinga miwili ilifukuza wake zao sababu ya akina mama.
1-Huyu alimfukuza mke sababu mama alimwambia mkeo hataki kukaa kupiga stori na mimi hadi anapiga stori na mabinti wa jirani.Mke ameajiriwa kwa hiyo huwa anashinda kazini na huwa anarudi nyumbani saa 11,akifika anakuta mama mkwe kakaa kibarazani na mabinti wa jirani kazi kuongea umbea. Jioni mwanamke anaandaa msosi na muda wa yeye kuwa free ni jumapili tu. Jamaa hakumsikliza mkewe akaamua kumfukuza
2-Jinga lingine lilimfukuza mke kisa mama anasema mkeo amezidisha sana kusali.Mke huwa akiamka asabuhi,cha kwanza maombi,ikfika mchana anatenga muda wa maombi,jioni maombi na huwa wakati mwingine anafunga wiki nzima na kufanya maombi,hapo mama mkwe alikuwa anakereka...kuna wazazi wa kiafrika usipokuwa na misimamo jiandae kuharibu maisha yako
 
Mke anapendwa kimahaba na mama anapendwa kama mzazi. Yaani mapenzi ya mke yanaitwa "EROS" na mama yanaitwa "STONGE", hiyo ni kwa mujibu wa wanafalsafa wa Kigiriki waligawa mapenzi katika sehemu kuu 5.
Kuna mijinga miwili ilifukuza wake zao sababu ya akina mama.
1-Huyu alimfukuza mke sababu mama alimwambia mkeo hataki kukaa kupiga stori na mimi hadi anapiga stori na mabinti wa jirani.Mke ameajiriwa kwa hiyo huwa anashinda kazini na huwa anarudi nyumbani saa 11,akifika anakuta mama mkwe kakaa kibarazani na mabinti wa jirani kazi kuongea umbea. Jioni mwanamke anaandaa msosi na muda wa yeye kuwa free ni jumapili tu. Jamaa hakumsikliza mkewe akaamua kumfukuza
2-Jinga lingine lilimfukuza mke kisa mama anasema mkeo amezidisha sana kusali.Mke huwa akiamka asabuhi,cha kwanza maombi,ikfika mchana anatenga muda wa maombi,jioni maombi na huwa wakati mwingine anafunga wiki nzima na kufanya maombi,hapo mama mkwe alikuwa anakereka...kuna wazazi wa kiafrika usipokuwa na misimamo jiandae kuharibu maisha yako
Nimeipenda hii

Na ndio msingi mzima wa andiko langu

Asante sana
 
Back
Top Bottom