Ni kichapo gani ulichokipokea kutoka kwa wazazi enzi za utoto wako ambacho hautokisahau?

NIN MATUKIO AMBAYO NIKIKUMBUKA NACHEKA NA KUHUZUNIKA.

1.Nakukumbuka kipindi cha nyuma Nilikuwa mtu wa misuli misuli , kujisomea somea na kusolve pepa na watu walionizidi darasa, maana wengi ndio nilikuwa nao na kucheza nao.

Hasa siku hiyo narudi usiku like saa moja hivi, na kabegi kangu, watu kimyaaaa home.

Kumbe kuna nanga alienda rum kwa wazee akapanda na matope kitandani ili achukue hela kabtini juu.

Maza kurudi kakuta tope, kauliza kimyaaa, kagawa kipigo nyumba nzima hadi atajwe muhsika.

Baada ya kipigo kuzidi, wakaona wanitoe kafara mie nisiekuwepo. Sasa hapo ndo nikawa nasubiriwa hamu na morale zote.

Tangazo likatolewa mm ndio most wanted,kufika naambiw unaitwa na maza chumbani kwake. Nikakaribshwa kwa upendo wote, kilicho faata naona maza anafunga mlango kama HELL IN A CELL, MITHILI YA POLISI MNAA NA MAABUSU MPYA.

Kamchezo kakaanza, kimbizana rum hapa na pale kwa kipigo sijui kosa langu, nilikuwa napenya kweny kochi la ndani, mara nyuma ya kabati mara nipo uvunguni sijui nilibugi wapi mie nikadkwa pigwa loba na miguuu, kichapo kitamuuu sana ( hiki lazima nilipe nikidaka mwizi) nilichomoka kama Jerry kwenye mikono
ya Tom, fungua mlango, fungua geti ndukiii
Maza nae mnaaa hajaniacha huyu mkuku, nikasema hapa nawasha turbo asome namba za viatu

Watu wakaaniungia siunajua life la zaman, ukifanya kosa kwa mzazi unakuwa adui wa mtaaa mzima lakin wapi sijadakwa.

Ishu ikawa kurudi home.
 
2. Dingi yeye alikuwa sio mtu wa kutoa kipigo daily, anakuhesabia tu. Ila siku akikudaka ni msala.

Kuna siku ilikuwa usiku tulipewa task mimi na dogo tujaze maji kwenye tenki kubwa, likijaaa tufunge bomba ili maji yaache kupanda. Then mwingine aoshe madumu akinge ya mifugo then mwingine ashikilie mpira ( Yalikuwa madumu mengi)

Sasa mim nikasema poaa, nawahi kutoa madumu njee , nikayaosha, nikatoa mpira chomeka bombani , dogo akija ashikilie akimaliza achomoe mpira akunje arudishe.

Hasa kuosha madumu hataki maji ya baridi. Nikafanya vyote, ila yeye anataka kushika mpira tu, yakijaaa tena mm nikunje na kuingiza mpira.( ambayo sio fea hata)

Basi nikapga kaz weka madumu mpira hupo dogo hataki kazi.

Dingi kakadiria muda kuja kucheki hakun kinacho fanyika.

Hapo juz tu, nilivaa buti yake aliyo bull vzuri ili aendee kazini nkaenda nayo kuuzia sula aka mute sasa akaungasha hapa.

Dogo alikuwa karibu na mlango, alipewa banzi la kichwa hadi akishika matako badala ya kichwa kwa maumivu, mimi nikafatwa nduki, fungua geti, omba msamaha kwa dingi kuwa tutaweka sawa.

Yeye anasema nendeni ndani nakinga mimi.
Nikagoma nikasema dingi mim nikienda ndan utaenda kutuvunja,
( Sasa upigwe kipigo cha usiku, cha mjeda, kesho asubuhi umevimba shuleni utakuwa maarufu kama YANGA ZARI ACHUKULIWE NA MSAGA SUMU)

Nika yeya mwanaume, dingi kaliunganisha, kanilibia kanipiga banzi la mgongo lakini haikuwa KO so nikabilingita nikasimama .

Nikasema baba unazjua sound waves zinavyo safiri?? Ushawahi kuona spidi ya Electron njooo ufanye observation, toka nduki ya hatari .

Dingi akarudi toa kipigo kwa dogo mim nikasolv bila kubondwa nilivyo usiku sana
 
Dah! Nakumbuka nikiwa kati ya darasa la tatu au nne hivi nilikuwa naishi kwenye geto langu kwenye geto hilo nilikuwa naishi na rafki zangu watatu hao jamaa walinizidi umri na wao walikuwa hawasomi shule ,sasa ikafika mahali wenzangu nawaona na wanawake halafu mbaya zaidi walikuwa wanawagongea kwenye hilo geto dah! Roho ikawa inaniuma sana , sasa ikatokea na mm nilitokea kumpenda bint mmoja alikuwa anaitwa lucy ikawa kumtongoza nashindwa sijui namna ya kutongoza , sasa nikawaambia wenzangu niliokuwa naishi nao wakanishauri nimwendee kwa mganga ili anipe dawa ya mapenzi , nilienda kwa huyo mganga akanitafutia dawa ila akanambia gharama yake itakuwa shilingi elfumbili.

Sasa hyo elfu mbili nikawa sina ikabidi niende nyumban nikamdanganya baba kuwa nmepoteza kitabu shulen, naye akanipa hela nikaipeleka kwa mganga baadae sjui baba alifikiria nn akaenda shulen kuulizia kama kweli nmepoteza hcho kitabu mwalm alikataa mzee karudi kwangu akanibana kuwa hela ilikuwa ya nn?

Baada ya kuona amenibana na maswali nilisema ukweli kuwa nmeipeleka kwa mganga ili anipe dawa ya mapenzi dah! Aisee nilikula kibano hicho mpaka sasa nina alama ya kovu kwasababu ya kipigo hicho. Utoto una raha yake
 
Hahahaha mkuu aisee mi mwenyewe nilikuwaga na hako kamtindo ka kwenda kuogelea almanusura nife maji mpaka leo naogopa kuogelea.
Hahahahaha Kumbe tupo wengi mkuu maana watu huwa wananicheka nikienda beach hata maji sigusi
 
Mi vichapo bi mkubwa kanitembezea vingi saana nikieleza hapa nitajaza kurasa.... ila moja ya vichapo heavy kuwahi tokea ni siku alinigonga stik zaid ya 100 daah kwakweli hua sisahau na hua namuoji kwanin alinichapa vile? Kosa ni kukaa chimbo tu et miezi 2
 
dodoma??
 
dah! Sitosahau b maza alivyonirushia TV ya inch 6
 
Aiseee katika malezi Wa Mama wanapiga bwana asikwambie mtu
 
Kila weekend nilikuwa na kazi ya kufagia banda la kuku nikimaliza napika chai.Mi zile kazi nlikuwa naona kama naonewa kwasababu mdogo wangu wa kike yeye alikuwa hafanyi chochote anaamka na kunywa chai tu hajafanya chochote.Tulikuwa tunamtindo wa kutaniana bas siku hiyo nimemaliza kufagia nikapika chai ila nlikuwa nimeamka na kisirani Wakati tunakunywa chai akaanza kunitania halafu nlikuwa nimekasirika namwambia sitaki uchokozi hasikiaa.Asa wakati anaendelea kakangu akanambia kama in mimi ningemwagia chai.Si nikamwagia ile chai mdogo wangu hata sijui nlikuwa nafkiria nini dogo akapiga kelele anakimbia analia mzee akaja akauliza.Aisee nilichezea kichapo mpaka nikasema bro ndo kanishauri.Tulichapwa mimi na bro sitakaa nisahau.
 
Tulilelewa na dingi kwa kuwa mama alienda zake abroad kusoma tangu mimi na mdogo wangu tukiwa wadogo kabisa, kwahiyo dingi alilazimika kuwa mpole tu nafikiri alikuwa anatuonea huruma.

Sasa mimi nikajua dingi ni mshkaji tu hamaindi chochote. Kila siku alikuwa anarudi saa mbili usiku ndio mimi naenda kuoga nae. Siku hiyo namsubiri nipo sebuleni nakula mziki wa Alfa Blondi, dingi akatia timu kama kawa, akaenda moja kwa moja kwenye redio akaroa tape yangu akaweka mabolingo yake

Mimi kuona hivyo nikajifanya Tundu Lisu nikamuambia "hivi baba wewe ni mjinga sanaee, kwanini umezima nyimbo yangu?" dingi aligeuka na sura fulani hivi nikajua tu hapa nimekinukisha. Wadada wa kazi walikuwa jikoni wakaona tumekatiza hapo jikoni kama Tom na Jerry ikabidi wamtulize mshua kwamba usiku ule isingekuwa poa maana nyumba ilikuwa na fensi ila haina geti

Usiku ule nililala na wale wadada maana dingi alikuwa na nia ya kunifanya kitu mbaya

Kulipokucha nikasahau msala wa jana usiku nikamfuata kama kawa anapojiandaa nakuwa naye, kumbe yeye bado ana fundo aisee, nilikula kipondo kitakatifu na hapo watu hawanisaidii wala nini. Hadi leo wadogo zangu ambao walikuwa hawajazaliwa kipindi hicho wananitania na stori hiyo ys kumuita baba mjinga
 
Hahahaha duh mkuu aisee angekuwa ni baba yangu ndo nimemwambia hivyo sijui kama leo hii ningekuwa salama.. Manake hasira za mahabusu zote zingeishia kwangu.
 
Hahahahaha kama ndo mimi nimepigwa na mzee kisa dogo akae muda wote mbali na mimi mzee akitoka tu namalizana nae kimya kimya.
 
Ndugu nilipigwa acha tu,nilipigwa mpaka nikaiva mwili wote, nilibaki na alama nyeusi za fimbo mwili mzima, halafu dogo mwenyewe kwa sasa ana nyodo balaa.
Patience123 nimeipenda sana story...huyo mdogo wako wa me/ me, maana nimesikitika tu pale uliposema ana nyodo sasa hivi
 
Nakumbuka nikiwa darasa la saba mwaka 2000 mama alinipa hela ya tuition....mie nikaenda zangu kununua mitumba kipindi hicho manzese wanauza sana mitumba.......

Nikawa siingii tuition kumbe kuna mwalimu ana namba ya mama akamuuliza mbona haujamlipia mwanao tuition na unajua ana mitihani.....eh akasema hela nimempa....kuja kuuliza sina majibu......alooo nilichezea bakora za mpera mpaka nikajikojolea........
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…