Ni kitu gani ulijifunza utotoni baadaye ukagundua ulipotoshwa na wazazi/walezi?

Ni kitu gani ulijifunza utotoni baadaye ukagundua ulipotoshwa na wazazi/walezi?

music mimi

JF-Expert Member
Joined
Jun 16, 2013
Posts
485
Reaction score
876
Ebu shea na sisi pengine wale wanaorithi kila kitu toka kwa wazazi watakiepuka kwenye malezi ya watoto zao.

Mimi nilikuwa nakatazwa sana kucheza kwenye majumba ya majirani. Wazazi wangu muda wote walitaka wanione nyumbani tena nikiwa mtulivu. Niliamini kutembea kwenye nyumba za jirani ni vibaya.

Hii imenifanya nimekuwa sio mtu wa kujichanganya na muoga wa watu. Moja kati ya mitihani yangu mikubwa ni kuanzisha ushikaji na watu naokutana nao kwa mara ya kwanza. Naamini ni kwa sababu udogoni nilinyimwa skills za kucommunicate na wenzangu.

Kingine mimi nilipokuwa mdogo nilikuwa napenda sana kuchezea cherehani ya mama. Ñilikuwa napenda kushona nguo. Lakini bi mkubwa alikuwa ananiweka mbali na nilishachapwa mara nyingi sababu ya cherehani. Mwisho nikaacha.

Kuna wakati nikiwa mkubwa nilikuja kufanya connection ya mapenzi yangu kwa cherehani na fashion.

Napenda sana kuvaa nguo nzuri. Uhenda ningekomaa na cherehani ningekuwa designer mzuri wa mavazi. Of course nimesoma mpaka chuo kikuu na nna ajira lakini sina tena nguvu ya kusema niwe nna factory yangu kuzalisha maybe suti au magauni. Bado nna uoga uleee wa cherehani.

Ebu shea experience yako na wewe.
 
Watoto wananunuliwa uongo mtupu .
 
Mi kuna vitu naweza kusema nilifundishwa vizuri utotoni na wala sikupotoshwa...

Nilipokuwa mdogo Dodoma tulikuwa na mchezo unaitwa SIMBI, kiufupi ni kama kamari. Sasa ilikuwa baba akinikuta nacheza ananipa kipigo mbele ya wenzangu, na hata kuna muda tukiwa tunacheza kamari za karata akinikuta ni kichapo tu.

Hali ile ilinifanya nikaacha hiyo michezo na hadi sasa ambapo najitegemea sina kabisa mazoea ya kucheza kamari ya namna yoyote ile nikiwa na Imani kwamba unapocheza kamari ukiwa na lengo la kujipatia pesa ni wazi kwamba hata mmiliki wa hiyo kamari naye anaitaka pesa yako ambapo yeye ana nafasi kubwa ya kuichukua yako kuliko wewe kuichukua yake.

Kitu kingine ilikuwa nikitukana tu na baba akasikia au hata asipokuwepo akipewa taarifa tu kwamba nikitukana alikuwa ananichapa sana hiyo imenijenga hadi sasa sina kabisa ujasiri wa kutukana hata kwenye mitandao ambapo kumejaa kutukanana ovyo.
 
Back
Top Bottom