Ni kwanini Viongozi Serikalini wakilazwa Mzena Hospital huwa tunafichwa, ila wakifa tu tunaambiwa Walilazwa hapo Mzena Hospital?

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2015
Posts
8,018
Reaction score
16,802
Sasa kwanini tu kwakuwa mmeamua Kutuficha Watanzania kuhusu Kulazwa Kwao hapo Mzena Hospital basi hata Wakifa ( Wakifariki ) msiendelee pia Kutuficha kwa Kutotujajia hiyo Hospitali na badala yake muendelee tu na Ratiba zenu za Maziko nyie nyie kama nyie pamoja na Wauguzi wa Mzena Hospital na wale Walinzi Wanoko wenye Maswali ya Kukomoa pale Getini Makumbusho? Tumeivumilia hii tabia tumechoka na badilikeni!
 
Hivi hiyo hospital ni kwa ajili ya kina nani??
Viongozi na viongozi wakubwa wakiumwa hutibiwa hapo mbona kitambo sana tu.

Nashangaa sahivi watu wanaona big deal

"Ila watu wajitahidi wawe na connection na kujuana na watu fulani mambo kama haya huwezi kukosa jua"

Ova

Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobile app
 
Ina maana hata yule mzee wetu wa kutuita marofa alikuwa anatibiwa pale?
 
Asante mkuu umenipa elimu nilikuwa silifahamu hili kabisa,
 
Kwani mkuu unaumia na nini juu ya Mzena? Wakilazwa hapo wagonjwa unatesekea nini? Ulisikia pale ni ya kila mtu ndo uende ende?

Ila unashangaza sana mtanzania mwenzangu. Ulienda kwa kufata protocol inavyopaswa ama ukienda na mziki wako mkubwa masifa sifa etc?

Na aliyekuambia ninkila kiongozi anatibiwa hapo ni nani? Na mbona ni hispitali ya siku nyingi sana hiyo ndo mnaijua leo ama?
 
Nashangaa wakati watu wanaijua kitambo sanaa
Ipo tu

Ova

Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobile app
 
Mzena ni hospitali ya mashushu na askari kanzu.
 
Nafikiri kwa suala la usalama wa viongozi kulingana na majukumu yao ya kazi, kivipi? mfano kiongozi ametatua mgogoro wa mtu maskini na tajiri, na tajiri akawa ameshindwa kesi lakini hajafurahisha na adui yake hapo namba moja ni huyo kiongozi msuluhishaji. Sasa tajiri anao uwezo wa kumdhuru kiongozi kwa njia tofauti, hivyo usalama elekezi ni muhimu kwa viongozi hasa wa afya zao.

Nachakata tu...
 

Yaani uliruhusiwa kumuona baba wa mshikaji wako???🤣🤣🤣
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…