Ni kwanini Viongozi Serikalini wakilazwa Mzena Hospital huwa tunafichwa, ila wakifa tu tunaambiwa Walilazwa hapo Mzena Hospital?

Mrangi mpuuzi sana yani kuwa na rafiki wa makumbusho na alivyopata nafasi ya kuingia huko ndani amejiona yuko tofouti na watanzania wengine, leo nimeamini jamaa mshamba sana.
Ilhali baani anakaa nao anakunywa nao bia sema utofauti ni kwamba baani hawafahamu.
 
Mzena ni hospitali ya watu fulani tu na ipo kwa sababu fulani wakati we ukilalamika wapo watanzania hata akiugua kidole harusiwi kwenda pengine ila pale, tena ni wenzetu na tunaishi nao mitaani na ikitokea akitibiwa pengine likatokea tatizo anawajibika kujibu kwann alienda huko na sio mzena.... kwa ufupi sio kila mtanzania anaruhusiwa kuingia pale na hata hivyo sasa naona inaanza kujulikana kwa watu ambapo pia ni kosa la kiufundi.
 
Mbona bado kuna Viongozi wengi tu wanasafirishwa kwenda huko Nje na huwa wanaonekana mno tu pale JNIA kupitia kule VIP Lounge au hujui?
 
Rose naye alikuwa kiongozi?
Kuna mahala katika Uzi wangu umeona popote pale katajwa kuwa ni Kiongozi? Kama nimeandika hivyo tafadhali naomba uweke hapa Ushahidi.
 
Hospital hii inamilikiwa na TISS so wengi wao wanaohudumiwa pale ni Usalama au Viongozi waandamizi wa Serikali ambao wanaona Hospital nyingne sio salama kwao
Zamani sana miaka ya themanini niliwahi kuwa reporter wa Anti-Corruption Squad (kabla ya Takukuru). Ile hoteli ya Palm Beach ilikuwa ni yao, na ingawa kila mtu alikuwa anaruhusiwa kuingia ndani ya hoteli ile, kuna sehemu ndani ya baa hiyo akina kapuku kama mimi na wewe tulikuwa haruhusiwi kufika na hakuna aliyelalamika. Nchi hii imegeuka kuwa nchi ya walalamikaji sana siku hizi.
 
Nafikili mtoa mada alimanisha wananchi kupewa tahalifa tu kwamba kiongonzi flani anaumwa kalazwa,hospitali flani basi but aina ya ugonjwa sio lazima kuitoa public bila consert ya mgonjwa, na kweli ugonjwa bado unabaki siri ya mgonjwa na mtoaji huduma wake
Vinginevyo kwa kuzitoa tahalifa bila ruhusa ya mhusika sio tu inakiuka mahadili ya kitabibu bali pia ya mgonjwa husika, labda tu Kama ugonjwa una vihatarishi katika jamii waweza kutoa tahalifa ili jamii kujikinga
 
Kawadanganye Wapumbavu katika hili Ndugu na ni vyema kama pengine unakuwa ama hujui au huna uhakika na Jambo lolote basi ukanyamaza.
Kumbe wewe popoma na kujiita charismatic na game changer huna lolote unalojua ni maneno matupu tu?

Niambie uliona nani amekwenda pale kutibiwa akatimuliwa, kama sio tu hisia zako na maneno yenu ya mtaani huko na vijiweni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…