Elections 2010 Ni kweli Asilima 51i ya wanafunzi waliomaliza shule za kata wamefaulu kwenda form 5?

analysti

JF-Expert Member
Joined
Aug 24, 2009
Posts
731
Reaction score
614
Nimemsikia Raisi wetu akiwaeleza wananchi ktk moja ya kampeni zake leo kuwa asilimia 51 ya wahitimu wa kidato cha nne shule za kata wamepata nafasi kwenda kidato cha tano. Mimi binafsi nina mashaka sana na hii kauli nikizingatia hali halisi ya hizi shule za kata. Sijui mnasemaje wana JF, Isijeikawa ni muendelezo wa mlolongo wa porojo katika kampeni.
 
Jamani ni uongo mtupu,hawafiki hata asilimia 20, hivi huyu Bwana anapata wapi ujasili wa kusema uongo namna hiyo mbele ya hadhara ya watu. Kweli kikwete ameshatuona watanzania mabwege kweli. Au anatuona wote hatujawahi kwenda shule? Huyu bwana juzi juzi alihaidi bajaj 400 ambazo pia alihaidi 2005.Hakutekeleza, ameahaidi tena mwaka huu!! Mwaka huu hatudanganyiki
 
Hebu tuweke sawa wamefaulu au wamepata nafasi maana unaweza kufaulu na usipate nafasi, heading inasema wamefaulu kwenye maelezo yako umesema wamepata nafasi, wakati unatuweka sawa ngoja nizame kwenye makabrasha yangu.

Elewa kufaulu kwa Tanzania hata una Div.4 unahesabika umefaulu sidhani kama unaweza kupata nafasi kwenda Form5 hata Makongo siku hizi hawachukui Div.4.
 

Ndo maana na mimi nikashtushwa, amesema wamepata nafasi kkwenda kidato cha tano, maana yake hawa wanafunzi wamepata > or = to div 3. Whis is quite imposible!!. Believe me, amesema wamepata nafasi kwenda kidato cha tano!! Huu ni uongo uliokithiri!!!
 

Watanzania Open your eyes ooooohhh!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…