Ni kweli ufugaji wa kuku wa nyama unalipa?

Sanitaiza

Member
Joined
May 19, 2020
Posts
30
Reaction score
21
Wakuu habarini za wakati, wanaboard.

Moja kwa moja nijikite kwenye mada. Nimefuga kuku kwa miaka takribani 6 sasa. Nimefuga kuku wa mayai (layers) na kuku wa nyama (broilers). Katika ufugaji wangu nimezingatia kanuni zote pamoja na ushauri wa wataalam.

Nimekuwa nikipata matokeo chanya katika miradi yangu. Kwa kweli ni jambo la kumshukuru Mungu.

Sasa wakuu, changamoto inakuja kwenye soko. Kuna wale jamaa wanakuja kununua kuku wa nyama usiku usiku mida ya sa 9 au sa 10 alfajiri. Kwa jina maarufu wanaitwa watu wa matenga. Hawa jamaa wanaweza nunua kuku hata 200 wa nyama na wanakupa hela yako vizuri. Kimbembe sasa njo asubuhi hesabu kuku waliobaki, utakuta wamebaki kuku wachache sana. Wengine wamekupiga.

Wakati mnauziana huwa hawapakizi mpaka na wewe uone ndio uruhus wapakize. Kwa kifupi mnahesabiana vizur tu. Ila ambacho sielew huwa wakija kununua kuku lazima waje na kuku wao wachache kama 10 hivi wako kwenye kirikuu.

Sasa sielewi huu uchawi au mazingaumbwe.

Ni kweli tutatoka kwa hii style au ndio tunapoteza muda.

Kwenu wadau, naombeni ushauri, nifanyeje ili niwadhibit hawa jamaa kwenye biashara yangu.

Asanteni wakulu
 
Kila Sehemu kuna changamoto Mkuu

Upo mkoa gani
 
Nakumbuka mda sana,nauza kuku wa bi mkubwa,kuja kuhesabu baadae nakuta pungufu sana.

Kwa kifupi jamaa wengi ni wapigaji,wanabeba pale pale mnapokuwa wote.
 
Ukisikia kuwa hakuna biashara bongo bila kizizi maana yake ndiyo hii sasa!

Niliacha biashara nikaingia kwenye kilimo nako ni balaa, wachawi vigogo wapo huko!

Heeee! Na kwenye ufugaji tena? 😳
 
Pambana uangalie jinsi gani utakabiliana nao, kila mahali kuna changamoto zake. Hakuna pesa rahisi.
 
Basi na wewe tumia kizizi muende sawa! If you can't fight join them!
 
Anachosema ni kweli hawa watu wanawaibia sana wafuga kuku kimazingaombwe, na pia wengi wao wakishakuzoea wanachukua kuku kulipa ni shida sana.
 
Mkuu pole, kilimo ni balaa, unapigwa mbaya wakati unavuna, dah hii dunia ni shida
Ukisikia kuwa hakuna biashara bongo bila kizizi maana yake ndiyo hii sasa!

Niliacha biashara nikaingia kwenye kilimo nako ni balaa, wachawi vigogo wapo huko!

Heeee! Na kwenye ufugaji tena? [emoji15]
 
Anachosema ni kweli hawa watu wanawaibia sana wafuga kuku kimazingaombwe, na pia wengi wao wakishakuzoea wanachukua kuku kulipa ni shida sana.
Fact mkuu, ni wakopaji balaa. Anakulipa mara ya kwanza, ya pili, then anasepa na mzigo na deni kubwa
 
Hapa ndipo mchezo upo.

Ila ambacho sielew huwa wakija kununua kuku lazima waje na kuku wao wachache kama 10 hivi wako kwenye kirikuu
 
Alafu anataka aingie bandani achague mwenyewe kuwa makini anavyobeba anaweza kukuambia mkononi kabeba kuku 10 kila mkono watano kumbe kabeba 7 wnakuwa very sharp akishachanganya kwenye tenga imekula kwako
 
Alafu anataka aingie bandani achague mwenyewe kuwa makini anavyobeba anaweza kukuambia mkononi kabeba kuku 10 kila mkono watano kumbe kabeba 7 wnakuwa very sharp akishachanganya kwenye tenga imekula kwako
Ndio mchezo wao mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…