Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 2,203
- 5,610
Habarini wakuu!
Mimi nimekuwa si mnazi sana wa mchezo wa ndondi; nimejikita zaidi katika kufuatilia mchezo wa soka. Aidha, katika kufuatilia soka katika kurasa mbalimbali za michezo nimekuwa nikikutana na habari za mabondia kufariki ulingoni mara kwa mara.
Zaidi ya hilo, kupitia kurasa mbalimbali za michezo wanaweka bayana kuwa katika kipindi cha miezi sita ndani ya mwaka huu (2019), kuna mabondia sita ambao tayari wamefariki ulingoni kutokana na kupata majeraha kichwani (yaliyosababisha damu kuingia kwenye ubongo). Kimsingi, binafsi nimekuwa sifurahishwi na habari hii na naona kuwa jambo hili lina athari kubwa kwani linaweza kuwakatisha tamaa watu wenye ndoto za kuwa mabondia nguli baadaye.
Hivyo, kutokana na hali hiyo kukithiri, ni jambo gani tunafikiri Shirikisho la Ndondi Duniani (W.B.O) linapaswa kufanya ili kulinda usalama wa mabondia dhidi ya madhara hayo?
Naombeni mchango wenu wadau.
Mimi nimekuwa si mnazi sana wa mchezo wa ndondi; nimejikita zaidi katika kufuatilia mchezo wa soka. Aidha, katika kufuatilia soka katika kurasa mbalimbali za michezo nimekuwa nikikutana na habari za mabondia kufariki ulingoni mara kwa mara.
Zaidi ya hilo, kupitia kurasa mbalimbali za michezo wanaweka bayana kuwa katika kipindi cha miezi sita ndani ya mwaka huu (2019), kuna mabondia sita ambao tayari wamefariki ulingoni kutokana na kupata majeraha kichwani (yaliyosababisha damu kuingia kwenye ubongo). Kimsingi, binafsi nimekuwa sifurahishwi na habari hii na naona kuwa jambo hili lina athari kubwa kwani linaweza kuwakatisha tamaa watu wenye ndoto za kuwa mabondia nguli baadaye.
Hivyo, kutokana na hali hiyo kukithiri, ni jambo gani tunafikiri Shirikisho la Ndondi Duniani (W.B.O) linapaswa kufanya ili kulinda usalama wa mabondia dhidi ya madhara hayo?
Naombeni mchango wenu wadau.