Ni lini Serikali itaanza kuwekeza kwenye viwanja vya michezo vya kisasa

Mtu Kwao

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2019
Posts
394
Reaction score
720
Salaam.

Kwa wale wanaofuatalia AFCON kule Cameroon watakubaliana na mimi kuwa Cameroon wametuacha sana kwenye suala la viwanja vya kisasa.

Viwanja vyao viko vizuri ni level za Ulaya.

Je, sisi tunakwama wapi na naamini hata kwenye suala la maendeleo tupo mbele ya Cameroon.

Kwa kwetu kidogo uwanja una uafadhali ni Uwanja Mkapa pale Dar es Salaam labda na wa uhuru kidogo lakini viwanja vya mikoani ni vina hali mbaya kabisa.

Kwa hali tuliyopo tunapaswa kuwa na viwanja vya kisasa walau hata 4 vya kubeba watu kuanzia elfu 40.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
tuna Ligi Bora kabisa lakin inauma watu wanavyokipiga kwenye tope eti premier league Ccm wamevikumbatia viwanja tuu.

na wanauwezo wa kutengeneza kiwanja kimoja kimoja kila mwaka upuuz tuuu
CCM wanatuchelewesha kwenye mambo mengi sana. Na tukiendelea kuikumbatia, basi siku zote tutabakia tu kuwa kichwa cha mwendawazimu.
 
Serekali iwaweke Simba na Yanga Kati iwakopeshe fungu kiasi wajenge viwanja viwili vyenye hadhi ya kimataifa then timu zirejeshe kidogo kidogo kwa miaka kadhaa huku wakiwa wamesolve tatizo la viwanja
Serikali hii hii ya ccm! Sasa si chama chao kitakosa mapato ya kuwalipa wafanyakazi wao, kupitia mapato yatokanayo na viingilio kwenye viwanja vilivyo jengwa kwa kodi za Watanzania wote! Ila mwisho wa siku wakaamua kujimilikisha kinyemela.

Wasingekuwa na maslahi yao binafsi, basi hili wazo lako lilikuwa ni zuri sana.
 
Serekali iwaweke Simba na Yanga Kati iwakopeshe fungu kiasi wajenge viwanja viwili vyenye hadhi ya kimataifa then timu zirejeshe kidogo kidogo kwa miaka kadhaa huku wakiwa wamesolve tatizo la viwanja
Viwanja vyote vizuri vitajaa Dar sasa hiyo watakuwa wamefanya nini.

Serikali inapaswa kujenga viwanja vizuri mikoani na ccm isalimishe mara moja viwanja vyote walivyotwaa kwani hivyo viwanja sio mali yao ni mali ya nchi.
 
Kweli Cameroon wana viwanja vizuri sana na wala hawapigi navyo kelele, vingejengwa hapa redio na TV zote zingepasuka kwa kusifia rais kwa kujenga viwanda vya kimataifa hadi mikoani.
 
Viwanja vyote vizuri vitajaa Dar sasa hiyo watakuwa wamefanya nini.

Serikali inapaswa kujenga viwanja vizuri mikoani na ccm isalimishe mara moja viwanja vyote walivyotwaa kwani hivyo viwanja sio mali yao ni mali ya nchi.
Nimejaribu kufikiria njia rahisi ya kuweza angalao kuwa na viwanja vitatu vyenye hadhi huwenda hiyo itakuwa njia nyepesi.
 
Cameroon wanacheza sana mpira na ni wapenzi wa muziki pia
Katika riadha na michezo mingi wapo mbele sana

Wapo top
Samuel Eto’o
Roger Milla kwa wanaomkumbuka huyu mwamba
Alex Song
Richard Bona Musician

Francis Ngannou- Mixed Martial arts
Huyu Francis ngumi yake lazima uende chini ni heavyweight wa UFC na mpunga anao

Sisi hata mbio tumeahindwa
Olympic tunawakilisha bendera tu bila watu
 
Nimejaribu kufikiria njia rahisi ya kuweza angalao kuwa na viwanja vitatu vyenye hadhi huwenda hiyo itakuwa njia nyepesi.
Sawa lakini viwanja vijengwe mikoani na waanzie kwenye kanda Mwanza, Arusha, Dodoma na Mbeya kila moja uwe na ujazo wa kuchukua watazamaji 60,000 na waweke kabisa na Floodlights.
 
tuna Ligi Bora kabisa lakin inauma watu wanavyokipiga kwenye tope eti premier league Ccm wamevikumbatia viwanja tuu.

na wanauwezo wa kutengeneza kiwanja kimoja kimoja kila mwaka upuuz tuuu
Unasema kwenye tope la Manungu, wenyewe TFF wakikusikia watakasirika mno..Ule ni uwanja hauna shida yaani kucheza Ligi Kuu
 
Kikubwa hata tuanze kuwa na pitch zenye ubora.

Sisi mashabiki hatuna shida. Inawezekana kabisa kila mkoa ukawa na kiwanja bora kabisa.

Waanzishe hata tozo [emoji23][emoji23][emoji4]
 
kama hatuku-host afcon ilipokuwa inashirikisha timu 16 leo ina timu 24 tusahau. leo gharama za kujenga uwanja wa kawaida wa soka kabisa wenye capacity ya kubeba mashabiki 50,000 na kuendelea ni wastani wa dola milioni 350-600, hapa ni sawa na bilion za kibongo bilion 700+ cha kuishauri serikali, ije na utaratibu kwmba kila raisi aingiaye madarakani kabla hajamaliza muhula wake aache ametuachia uwanja mmoja wenye standard za kimataifa. nasema hvyo kwa kutambua ughali na ugumu kutekeleza miradi hii kwa maramoja huku nchi ikikabiliwa na vipaumbele vingne.. endapo utaratibu ungekuwa rasmi toka awamu ya 3..ina maana leo tungekuwa na viwanja vinne vikubwa (multipurpose)
 
Wakijenga mtalalamika kwamba mnataka pesa mofukoni na sio kuwekeza kwenye burudani
 
Watanzania hatuna desturi kuwekeza kwenye viwanja hata vya makazi.

Mtu yupo radhi atumie milioni 4 kwa mwaka kwenye nyumba za kupanga kuliko kununua kiwanja cha milioni 2 tena kwa mkopo (kulipa kidogo kidogo).

Sasa ukija kwenye viwanja vya michezo anasubiriwa Bakhresa na Moo
 
Uwanja wa sokoine mbeya umechakaa sana nahis ndo umchoka kuliko vyote vya Ccm
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…