Ni lini sherehe za sikukuu za kitaifa zisizo za kidini ziligeuka na kuwa maonyesho ya kijeshi?

Ni lini sherehe za sikukuu za kitaifa zisizo za kidini ziligeuka na kuwa maonyesho ya kijeshi?

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
94,296
Reaction score
122,540
Wajuzi na wajuvi, ni lini hizi sherehe za sikukuu za kitaifa zisizo za kidini ziligeuka na kuwa fursa ya wanajeshi kufanya maonyesho ya kazi zao?

Maana sikumbuki kabisa kuona mambo kama haya miaka ya nyuma enzi za Mkapa, Mwinyi, na kwa kiasi hata Nyerere.

Pengine labda nimesahau. Kama ni hivyo, basi naomba kukumbushwa kama hata huko nyuma yalikuwepo haya maonyesho ya aina hii.

Na lengo lake ni lipi hasa? Kutisha waleta chokochoko?

Hii ni leo katika kusherehekea siku ya muungano.


View: https://youtu.be/AcYex2b3448?si=qi7Ve1LeMO5VcnvB
 
Back
Top Bottom