ryana fan
JF-Expert Member
- Apr 27, 2018
- 2,632
- 3,055
Habari zenu wakuu poleni na miangaiko ya huku na kule kutafuta chochote.
Niende moja kwa moja kwenye Hoja.
Kama ilivyokawaida na kanuni na taratibu bila kusahau katiba yetu inavyosema, baada ya miaka 5 ni uchaguzi mkuu nchini kwetu.
Nimekaa na kuwaza na kutafakari kwa kina sana juu ya uchaguzi huu wa October 2020 na kujiuliza kwann tusimrudishe JPM kwa kishindo katika uchaguzi ujao kwasababu JPM ametufanyia mengi makubwa kwa muda mchache. Nitaelezea machache
1. Afya. Serikali imejenga zahanati 1198, vituo vya afya 487, Hospitali za Wilaya 71, Hospitali za Mikoa 10, Hospitali ya kanda 4 pamoja na Hospitali ya Uhuru inayoendelea kujengwa Dodoma.
2. Madawa ya Kulevya. Tunafahamu fika miaka 5 nyuma jinsi nguvu kazi/vijana walivyokuwa wanaaribikiwa na madawa ya kulevya. Sasa ivi madawa ni ndoto katika nchi yetu. Hapa nampa 100% JPM
3. Umeme wa REA. Ni nani asiyejua nini kinaendelea huko vijijini. Umeme unasambazwa kila kijiji aisee kwa hili nampa JPM 100%. Sasa ivi hakuna tofauti kati ya mjini na kijijini. Tumpe 5 tena amalize vijiji vilivyosalia.
4. Miundombinu. Kipindi hiki cha miaka mitano JPM amejenga zaidi ya kilomita 2000.
5. Madaraja na fly over. Ubungo exchange, salender bridge. Pamoja na vivuko mbali mbali kama mv victoria, Mv Kigamboni, Nyasa amepeka kivuko, kigoma na sehemu mbali ya nchi hii. Nani kama Magifuli?
6. SGR. Barabara ya reli ya kisasa kabisa inayotumia umeme inajengwa kwa mara ya kwanza katika nchi yetu. Km 400 from Dar to Moro mradi umefikia 75%. Moro to Dodoma mradi umefikia 35% na kazi inaendelea.
7. Stigler’s Gorge. Ni mradi mkubwa wa umeme unaojengwa katika bonde la rufiji. Huu mradi utasaidia kupinguza gharama za umeme nchi nzima na kuvutia wawekezaji katika nchi yetu kwani gharama ya umeme utakuwa ni mdogo. Nani kama JPM?
8. Elimu Bure. Hapa hakuna shaka watoto wanasoma bure bila malipo yoyote kuanzia darasa la saba adi kidato cha nne. Mikopo ya wanafunzi wa chuo kikuu sasa imebaki historia. Hakuna migomo iliyokuwa inatokea mara kwa mara vyuoni.
9. Maji safi na Salama. Jamani mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni. Kwenye secta ya maji tunaona matokeo chanya ndani ya miaka mitano ya JPM. 5 again JPM.
10. Ndege. Bila ya kupepesa macho tumeona kwa weledi mkubwa jinsi JPM alivyofufua shirika la Ndege Tanzania pamoja na kujenga na kukarabati viwanja vya ndege. Mfano. Terminal three JK Nyerere international, uwanja wa ndege chato, Dodoma, Mwanza, Mbeya, Mtwara na sehemu zingine.
Mwisho ingawa sijataja zote lakini hizi ni baadhi ya miradi ambayo JPM amefanikiwa kwa asilimia mia moja ndani ya miaka 5 tu. Hizi zote ni miradi ya mkakati wenye lengo la kupeleka Tanzania katika uchumi wa kati.
Magufuli 5 again
Samia 5 again
Nawasilisha
Niende moja kwa moja kwenye Hoja.
Kama ilivyokawaida na kanuni na taratibu bila kusahau katiba yetu inavyosema, baada ya miaka 5 ni uchaguzi mkuu nchini kwetu.
Nimekaa na kuwaza na kutafakari kwa kina sana juu ya uchaguzi huu wa October 2020 na kujiuliza kwann tusimrudishe JPM kwa kishindo katika uchaguzi ujao kwasababu JPM ametufanyia mengi makubwa kwa muda mchache. Nitaelezea machache
1. Afya. Serikali imejenga zahanati 1198, vituo vya afya 487, Hospitali za Wilaya 71, Hospitali za Mikoa 10, Hospitali ya kanda 4 pamoja na Hospitali ya Uhuru inayoendelea kujengwa Dodoma.
2. Madawa ya Kulevya. Tunafahamu fika miaka 5 nyuma jinsi nguvu kazi/vijana walivyokuwa wanaaribikiwa na madawa ya kulevya. Sasa ivi madawa ni ndoto katika nchi yetu. Hapa nampa 100% JPM
3. Umeme wa REA. Ni nani asiyejua nini kinaendelea huko vijijini. Umeme unasambazwa kila kijiji aisee kwa hili nampa JPM 100%. Sasa ivi hakuna tofauti kati ya mjini na kijijini. Tumpe 5 tena amalize vijiji vilivyosalia.
4. Miundombinu. Kipindi hiki cha miaka mitano JPM amejenga zaidi ya kilomita 2000.
5. Madaraja na fly over. Ubungo exchange, salender bridge. Pamoja na vivuko mbali mbali kama mv victoria, Mv Kigamboni, Nyasa amepeka kivuko, kigoma na sehemu mbali ya nchi hii. Nani kama Magifuli?
6. SGR. Barabara ya reli ya kisasa kabisa inayotumia umeme inajengwa kwa mara ya kwanza katika nchi yetu. Km 400 from Dar to Moro mradi umefikia 75%. Moro to Dodoma mradi umefikia 35% na kazi inaendelea.
7. Stigler’s Gorge. Ni mradi mkubwa wa umeme unaojengwa katika bonde la rufiji. Huu mradi utasaidia kupinguza gharama za umeme nchi nzima na kuvutia wawekezaji katika nchi yetu kwani gharama ya umeme utakuwa ni mdogo. Nani kama JPM?
8. Elimu Bure. Hapa hakuna shaka watoto wanasoma bure bila malipo yoyote kuanzia darasa la saba adi kidato cha nne. Mikopo ya wanafunzi wa chuo kikuu sasa imebaki historia. Hakuna migomo iliyokuwa inatokea mara kwa mara vyuoni.
9. Maji safi na Salama. Jamani mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni. Kwenye secta ya maji tunaona matokeo chanya ndani ya miaka mitano ya JPM. 5 again JPM.
10. Ndege. Bila ya kupepesa macho tumeona kwa weledi mkubwa jinsi JPM alivyofufua shirika la Ndege Tanzania pamoja na kujenga na kukarabati viwanja vya ndege. Mfano. Terminal three JK Nyerere international, uwanja wa ndege chato, Dodoma, Mwanza, Mbeya, Mtwara na sehemu zingine.
Mwisho ingawa sijataja zote lakini hizi ni baadhi ya miradi ambayo JPM amefanikiwa kwa asilimia mia moja ndani ya miaka 5 tu. Hizi zote ni miradi ya mkakati wenye lengo la kupeleka Tanzania katika uchumi wa kati.
Magufuli 5 again
Samia 5 again
Nawasilisha