Ni majanga gani ya kiikolojia ambayo Tanzania imewahi kabili/inakabili?

Ni majanga gani ya kiikolojia ambayo Tanzania imewahi kabili/inakabili?

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Habarini. Kuna hii ishu ya majanga ya kiikolojia ambayo mara nyingi husababishwa na binadamu na shughuli zao. mfano hapa Tanzania kuna janga la Magugu maji katika ziwa Victoria. Inasemekana yaliletwa sijui na watu gani. Pia nasikia kuna Samaki, kati ya Sato au Sangara, waliwekwa humo ziwani na kusababisha kutoweka kwa baadhi ya samaki asili.

Pia kwenye mji wa Dar kuna kunguru wanaoitwa kunguru wa Zanzibar, asili yao ikiwa Bara Hindi, hawa waliletwa Zanzibar ku;la mizoga lakini wamegeuka kuwa janga la kiikolojia. Naomba kujuzwa zaidi juu ya majanga ya kiikolojia yaliyowahi au yanayoipata Tanzania?
 
Hawa kunguru wamekuwa changamoto sana kwakweli!

Hawa kunguru wanakula mpaka kiberiti.
 
Hawa kunguru wamekuwa changamoto sana kwakweli!

Hawa kunguru wanakula mpaka kiberiti.
Halafu wanyama kama hao wanaokula matakataka na mizoga ni hatari sana katika kueneza magonjwa.
 
Kunguru washakwapuaga chapat yangu
Kila nikikumbuka....

Nakumbuka siku moja tulienda Tandika kwenye shughuli fulani.

Muda wa mchana tukaagiza ugali mdogo na samaki mkubwa.

aliyetuletea chakula akatupa tahadhari tuwe makini kuna kunguru.

sisi tukachukulia kawaida.
akakifunika chakula akaondoka.

ndani ya muda huo huo kunguru ameshafunua sahani pale na keshachukua samaki yuko juu kwenye fensi anakula kitu roho inapenda.
 
Hivi hawa wadudu ndio ilishindikana kabisa kapatiwa ufumbuzi? maana ni kero aisee.
 
Hichi kitu hakipo direct sana

Kutokana na aina ya Settlements (Clustered Settlements) tulizo nazo kwenye majiji hasa Dar,
Kupata enough Ventilation within a region ni changamoto and in turns inaleta thick air kwa viumbe hai kwa kulinganisha na huku mikoani

So hapo MADHARA ya kiikolojia yako very minor to individual as he consumes insufficient air regarding mahusiano yake na viumbe wengine
 
Back
Top Bottom