Ni maziwa gani mazuri kwa watoto wachanga wa chini ya mwaka mmoja

SMA Gold , ni mazuri. Ila kopo ni 25,000/=. Maziwa ya ng'ombe hawashauri watoto chini ya mwaka mmoja labda uchanganye na maji.
<br />
<br />
vp maziwa ya soya yanafaa kwa mtoto?je kwa mama mjamzito?
 
Wabongo bana kwa kujifanya wajuajiii..... Mtu ameomba msaada maziwa gani ya kopo mazuri nyie mnajibu maziwa mazuri ya mama tu...... Kwani mmesikia ye hataki kumnyonyesha mwanae...??????? Jamani mkiona mtu anauliza mjue lipo linalomsibu.... Mwingine maziwa hayatoki...... Mwengine mfanyakazi na analazimika kumuacha mtoto masaa mengi nyumbani.... Mwengine muathirika na hapaswi kunyonyesha....... Napendekeza tuwe tunatoa ushauri Kama ulivoombwa
 
Kwani kuna mtu aliyesema maziwa ya mama siyo bara?zipo sabb nyingi zinazoweza kumzuia mama kumnuonyesha mwanae na ndo maana msaada umeombwa hapa tatixo letu kila kitu tunajifanya tunajua
 
Maziwa ya mama ni the best kwa mtoto.

Yanafata maziwa ya ng'ombe. Watoto wengi yatima hulelewa kwa maziwa ya ng'ombe na hakuna madhara wanayapata.

Nchini India baadhi ya watu hawali nyama ya ng'ombe kwasababu ng'ombe kwao ni "mama" kwavile anaweza kutoa maziwa ya kulelea kitoto tangu siku moja hadi utu uzima.

Mimi siamini sana maziwa ya kopo kwani ni gharama sana na cyo natural.
 
Maziwa ya Mama ndio lishe bora kwa mtoto na Mama anapaswa amnyonyeshe motto mpaka miezi sita ipite baada ya hapo kidogo kidogo unanza mpa mtoto maziwa ya ng'ombe,mbuzi,ngamia hii ni kutokana na urahisi wakuyapata huku ukimchanganyia na vyakula vya kumjenga mwili zoezi la kunyonya ni endelevu mpaka afike miaka miwili.Ukitaka mtoto Genious usikosee mwanzoni mwa malezi kuanzia siku ya kwanza ukileta uzungu jiandae kumpeleka mtoto kila aina ya tuition ukubwani.
 


Sio ujuaji ila tunaelekezana na kushare kila mtu alichonacho, sababu wamama wengi wamechukulia kama fashion na sio ubize wa kazi wala upungufu wa maziwa.
 
Ukiacha maziwa ya mama,maziwa mengine yanayoweza kumsaidia mtoto kwa uhakika ni maziwa ya ng'ombe..!!! Maziwa ya viwandani siyo maziwa bora unless hakuna namna nyingine basi unaweza kumpa mwanao..!
 
Hayo maziwa ya kopo ndiyo yanasababisha Dar na Mwanza ziongoze kwa wingi wa mataahira yani 2% na 1.2% respectively.

Hata wamama wa nyumbani hawataki kunyonyesha bila hata sababu za msingi.

Maziwa ya mama ndiyo safi,kina mama na kina dada acheni ubishoo.
 
Nakupa like mwanawane lakini wanawake wa kidijitali waki-google wakakuta uongo wa wafanya biashara wanaubeba kama ulivyo. Fungukeni wandugu wazungu haohao ndo wanaleta maziwa ya kuua vizazi vyetu, baada ya muda wanaleta matokeo eti utafiti unaonesha maziwa ya unga yana sumu, halafu wanaleta brand nyingine. Hapa kanda ya ziwa tunakamua na kunywa bila kuchemsha na tumekuwa watu wazima hatusikii hayo magonjwa yenu. Aki na mama mnaojifanya mmesoma mnagoma kunyonyesha eti nyonyo zisilale mtahangaika kuzunguka hospitalini.
 
Nakubaliana na wewe ila hili la 'mwingine mfanyakazi na analazimika kumwacha mtoto masaa mengi nyumbani' Hivi nyie wasomi kipi bora kati ya kunyonyesha mtoto kumwepusha na magonjwa yaletwayo na wazungu kupitia maziwa ya unga kama kansa, magonjwa ya ini na utahila au kazi inayokufanya umtelekeze mtoto?
 
Tupo pamoja mkuu, mimi mke wangu hunyonyesha watoto kwa maziwa yake mpaka anapomuachisha(zaidi ya mwaka mmoja na nusu).
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…