MwanaHaki
R I P
- Oct 17, 2006
- 2,401
- 707
Waungwana,
Mpaka sasa, Jimbo la Uchaguzi la Kawe lina wagombea wafuatao wa Ubunge, ambao ndio wanaosikika.
Tetesi zinasema kwamba wakazi wengi jimboni wanamtaka zaidi Halima Mdee, huku nyingine zikisema kwamba huenda James Mbatia akashinda.
Wako watu wengi wanaosema Angela Kizigha hana la kuongea, na akiwa kwenye kampeni anashindwa kuongea, anakwepa kujibu maswali anayotupiwa. Inadaiwa kwamba yeye hayuko mbali na Hawa Ng'umbi, ambaye CCM imetamka kwamba italazimika kutumia nguvu nyingi kurekebisha hali ya hewa aliyoichafua wakati alipopandisha jazba kwenye mdahalo wa TBC1, ambapo Hawa alipandisha jazba na kumjibu mwandishi wa habari aliyemwuliza maswali kuhusu tuhumba mbali mbali dhidi yake.
Ningependa kupata maoni yenu. Nani atashinda?
Asanteni.
-> Mwana wa Haki
Mpaka sasa, Jimbo la Uchaguzi la Kawe lina wagombea wafuatao wa Ubunge, ambao ndio wanaosikika.
- Angela Kizigha (CCM)
- Halima Mdee (CHADEMA)
- James Mbatia (NCCR-Mageuzi)
Tetesi zinasema kwamba wakazi wengi jimboni wanamtaka zaidi Halima Mdee, huku nyingine zikisema kwamba huenda James Mbatia akashinda.
Wako watu wengi wanaosema Angela Kizigha hana la kuongea, na akiwa kwenye kampeni anashindwa kuongea, anakwepa kujibu maswali anayotupiwa. Inadaiwa kwamba yeye hayuko mbali na Hawa Ng'umbi, ambaye CCM imetamka kwamba italazimika kutumia nguvu nyingi kurekebisha hali ya hewa aliyoichafua wakati alipopandisha jazba kwenye mdahalo wa TBC1, ambapo Hawa alipandisha jazba na kumjibu mwandishi wa habari aliyemwuliza maswali kuhusu tuhumba mbali mbali dhidi yake.
Ningependa kupata maoni yenu. Nani atashinda?
Asanteni.
-> Mwana wa Haki