Ni mtazamo wangu...

Ni mtazamo wangu...

Mentor

JF-Expert Member
Joined
Oct 14, 2008
Posts
20,328
Reaction score
23,909
Ni Mtazamo wangu…
Nakumbuka nikiwa sekondari ya Mawezi, Moshi.
Likizo tulikuwa tunakutana na washikaji tuliosoma wote primary halafu wakapangiwa special schools Kibaha, Mzumbe, na Ilboru.
Na wale wa seminary ambapo wanapewa notes na test kila wiki…jamani kuna watu wana raha.
Basi hawa woote tunakutana mtaani tunafundishana weee na kubadilishana knowledge mpaka likizo inaisha…hiyo ndo ilikuwa tuition yetu. Ndiyo si tulisoma wote primary kwahiyo bado ni marafiki.
Na likizo wanakuja nyumbani. Wana interact na sie wa shule za kata tunabadilishana mawazo.
Matokeo form four: Division one (leo hii ningekuwa top ten ya watahiniwa wa CSEE 2012)

A level nikapangiwa Same sekondari. Huko tukawa tunatoroka na kuja kupiga kitabu Moshi sekondari (Old Moshi Sec) wenyewe waliamua kujiita Gold Moshi…dem dayz!
Likizo tena tunakutana na washkaji waliopangiwa Special schools hizo tunabadilishana utirial ma test pepa manini.
Matokeo form six: Division one nzuri tu ya kunipa grades za kusoma Electronic Science & Communication chuo.

Mtazamo wangu:
Ile dhana ya special schools ilisaidia sana kuboresha elimu na kuongeza morali wa wanafunzi kusoma.

  1. Sasa hivi unakuta mwanafunzi anasoma hapo hapo na wale wale aliosoma nao primary hawapati challenges za nje hata kidogo.
  2. Waliofuta special schools hawakukumbuka ule usemi wa, “the world is a book and those who don’t travel read only a book” otherwise walidhani kina Nyerere pamoja na umaskini tuliokuwa nao bado walifanya hivyo. Walipeleka hadi watu kusoma nje kwanini???


My call:

Kawambwa & Co. rudisheni special schools kwa maana ile ile ya special schools….
 
Back
Top Bottom