Ni muda muafaka sasa tuwe na Wagombea Binafsi

Ni muda muafaka sasa tuwe na Wagombea Binafsi

jiwe angavu

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2015
Posts
20,419
Reaction score
39,217
Wakuu nawasalimu

Ifike hatua sasa katiba mpya iweke wazi kipengele cha mgombea binafsi katika ngazi zote za uchaguzi kuanzia serikali za mitaa hadi ngazi ya urais.

Vyama vya siasa vingi vimejaa wakanjanja na walaghai na vimeshapoteza mvuto mbele ya jamii..wamebaki wale masikini njaa ambao wanaamini watafaidika na vyo ili hali vyama hivyo vina wenyewe na vingine ni saccoss za familia.

Swali la kujiuliza kwanini serikali ya kijani haitaki uwepo wa wagombea binafasi, shida hasa nini ama wana wivu ama wanajua hawana uwezo wa kusimama dhidi ya mgombea binafsi mwenye uwezo.

Tunahitaji wagombea binafsi waruhusiwe ila mwanachi wachague watu wanao wafahamu sio vyama vyao, imefika wakati nchi hii unashindwa kutofautisha kati ya serikali na chama.

Kwanza watu wengi sio mashabiki wa vyama hivi vilivyo jaa unafiki na ulaghai kwa maslahi ya wachache.

#MaendeleoHayanaChama


FB_IMG_1655450514099.jpg
 
Back
Top Bottom