mriringa
JF-Expert Member
- Jan 17, 2017
- 663
- 714
Ujana ni maji ya moto na uzee ni maji ya baridi na ikumbukwe uzee ni usiku.
Wakati natafakari maisha yangu huku nikiwaza kesho yangu imenilazimu niwaze mbali kwaani kuwaza karibu ni sawa na kuchimba shimo ndani ya nyumba.
Uzi huu najua wengi hatuupendi kwavile tunaona leo yetu kama kesho yetu ila ukweli ni kwamba kesho yetu ni ngumu kama leo hujaanda kesho yako.
Wakuu maisha ni fumbo ambalo Mungu pekee analijua na kama binadamu hatujui basi ni mda muafaka wa kuwekeza kwenye kilimo hasa cha mda mrefu ambacho utakula hata uzeeni( ikumbukwe nimesema maisha au uhai ni fumbo hivyo nawe ishi kwa fumbo kwaani hujui utaishi miaka mingapi na ili kuepuka msemo wa MAJUTO NI MJUKUU basi anza kupambana maana mjini kuzuri ukiwa na afya ila ukizeeka mjini kwa mto).
Wakati nawaza vijana kutoka Iringa na Njombe waliopo mjini miaka nenda rudi bila kurudi kuwekeza hata kwenye kilimo cha miti au parachichi huku maeneo ya familia yakiuzwa maana hayana mlimaji. Vijana TURUDI nyumbani tukawekeze ila maisha yawe mjini haina shida.
Miti inalipa sana ila utawala wa mwendazake ulikuwa mgumu kwa hilo zao ila sasa naamini supply na demand ya mbao au nguzo itakuwa kubwa sana.
Narudia kusema wapendwa tuwekeze kwenye ardhi na tulime kwa juhudi mazao ya mda mrefu maana hata uangalizi wake sio kazi ukilinganisha na mazao ya mda mfupi, lakini nisinukuriwe vibaya kwamba mazao ya mda mfupi hayafai hapana maana kuna baadhi ya mikoa hakuna mazao ya mda mrefu kama mikoa mingine.
Tucheze na fulsa zinazopatikana kwenye maeneo yetu. Kila lakheri kwa atakayeona Kuna sababu kuchukua wazo langu au ushauri huu.
Wakati natafakari maisha yangu huku nikiwaza kesho yangu imenilazimu niwaze mbali kwaani kuwaza karibu ni sawa na kuchimba shimo ndani ya nyumba.
Uzi huu najua wengi hatuupendi kwavile tunaona leo yetu kama kesho yetu ila ukweli ni kwamba kesho yetu ni ngumu kama leo hujaanda kesho yako.
Wakuu maisha ni fumbo ambalo Mungu pekee analijua na kama binadamu hatujui basi ni mda muafaka wa kuwekeza kwenye kilimo hasa cha mda mrefu ambacho utakula hata uzeeni( ikumbukwe nimesema maisha au uhai ni fumbo hivyo nawe ishi kwa fumbo kwaani hujui utaishi miaka mingapi na ili kuepuka msemo wa MAJUTO NI MJUKUU basi anza kupambana maana mjini kuzuri ukiwa na afya ila ukizeeka mjini kwa mto).
Wakati nawaza vijana kutoka Iringa na Njombe waliopo mjini miaka nenda rudi bila kurudi kuwekeza hata kwenye kilimo cha miti au parachichi huku maeneo ya familia yakiuzwa maana hayana mlimaji. Vijana TURUDI nyumbani tukawekeze ila maisha yawe mjini haina shida.
Miti inalipa sana ila utawala wa mwendazake ulikuwa mgumu kwa hilo zao ila sasa naamini supply na demand ya mbao au nguzo itakuwa kubwa sana.
Narudia kusema wapendwa tuwekeze kwenye ardhi na tulime kwa juhudi mazao ya mda mrefu maana hata uangalizi wake sio kazi ukilinganisha na mazao ya mda mfupi, lakini nisinukuriwe vibaya kwamba mazao ya mda mfupi hayafai hapana maana kuna baadhi ya mikoa hakuna mazao ya mda mrefu kama mikoa mingine.
Tucheze na fulsa zinazopatikana kwenye maeneo yetu. Kila lakheri kwa atakayeona Kuna sababu kuchukua wazo langu au ushauri huu.