Ni namna gani ni jinsi gani tutawini maishani

Status
Not open for further replies.

Airmanula

JF-Expert Member
Joined
Nov 30, 2016
Posts
3,527
Reaction score
5,762
Ilikua jumapili nikamuona rafaeli amekaa ni juu ya nini, ni juu ya baiskeli, namuliza anaenda wapi, kanambia anaenda feli huko feli ni kwanani, ni kwa lile jitu tapeli,,asa utamuona wapi atakua kwenye meli ndio wapi ndio huko huko feli, tena nikamuona huyo huyo rafaeli anacheza na nani, anacheza na yule dada mary,,namuliza rafaeli hapa ndio feli,,anasema sio hivyo mwenzio unajua nimeharibikiwa na ile baiskeli nategemea kwenda kule ostabei nako huko ntamkuta braza Mtei yeye ndie atakayenipunguzia bei ya spea za baiskeli

Kesho yake nikatoka moja kwa moja kwa rafaeli nikamkuta nyumbani anasikiliza CD ya R Keli, nikamuliza rafaeli una CD ya Makaveli akaniambia na makaveli, r keli na maria keli, sisi hatukukaa tukatoka moja kwa moja haooooo mpaka kwenye baa, unaambiwa watu walikua wamejaa nazo baiskeli na motokaa,

basi tukaagiza masafa pale na kitimoto,tulianza kupata moja baridi moja moto, wakati tunaendelea kidogo tu huyooo akatokea Mzee Urassa,,na ile Land Kruza yake new model ya kisasa power engine 2.4 filling system ya kisasa unaambiwa, ni automatic kuanzia kiti hadi vitasa, basi alikua na laki 3 mfukoni, akajishika kiunoni akatuangalia akatudharau akaingiza mkono mfukoni akatoa pesa akaweka pale mezani kisha akaenda chooni, sisi basi tukaanza kulewa, tukalewa tukalewa Yesu wangu , tulilewa tulilewa tulilewa tumelewa wakaanza kuongezeka ndugu zetu kutoka sehemu mbalimbali za kilimanjaro, marangu, machame,uru,,kishimundu, kibosho, mwika vunjo, mpaka kiboroloni unaambiwa tarakea mpaka huko sehemu za rombo wote pale wakawa wamemiminika,masawe alikuepo, mariale alikuepo, shirima alikuepo, mange alikuepo, lema alikuepo, ndossi alikuepo, mtei alikuepo, asei alikuepo, mama priska alikuepo,,mama manka alikuepo, minja alikuepo, kilua alikuepo, na huyu mtoto anakaa mtaa wa pili nani huyu...chuwa, haha eti chuwa nae alikuepo ....

itaendelea...

Weekend njema ...
 
Huyo anaitwa Freddy Saganda.

Dogo alikuwa mtundu sana. Ana flow na "story telling rap"unaona kama movie vile.

Nafikiri alikuwa wa kwanza ku rap kwa lafudhi za kikabila.

Halafu watu wengi wakafikirini Mchaga, wakati hata si Mchaga.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…