Ni nani mnufaika wa Grand Ethiopian Renaissance halts?

Hakuna mtu alikua akipinga SGR SGR yetu kama wewe ulikua unapinga sana tu mpaka ukasema tukitandika reli kilomita moja utatembea uchi, lakini saivi ni aibu tupu imekujaa

JPM is another level
 
Hata mimi nilikua nashangaa kwanini umeme siku hizi haukatiki, yaani napiga kazi tu mbele kwa mbele.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] hupo Kenya hipi wewe!! Ww jamaa huwa una porojo sana au unataka tuingie twitter tukuletee wakenya wanaosema ukweli. Kadoda njoo ufanye yako mzee baba [emoji1]
 
Kupanga bajeti kubwa haina maana yoyote kama hakuna kinachoonekana on the ground, huu ndio ugonjwa wenu kuonyesha kwamba mpo na pesa nyingi wakati 50% ya hizo pesa zinaishia mifukoni mwa politicians, vipi muwe na bajeti kubwa ya elimu lakini mshindwe kutekeleza "Laptop per child?".

Tumekopa na tutaendelea kukopa kwa ajili ya miradi mingi ya maendeleo, lakini tunajitahidi sana kutumia pesa ya ndani hasa katika miradi inayohitaji pesa nyingi ambazo zinaongeza deni la Taifa na kuhatarisha Uhuru wa nchi yetu.

Hiyo pesa uliyosema tumekopa, yote inafanya kazi za maendeleo
1)Upanuzi wa Dar port $350M
2)Upanuzi wa Tanga & Mtwara ports $230M
3) Second phase BRT $160M
4)Uboreshaji wa miundombinu ya Dar $300M
5)Ujenzi wa Ubongo interchange $90M
6)Ujenzi wa Daraja la Salender $400M

Sasa linganisha, tumekopa $1.9B, lakini tumetumia $6.7B pesa yetu ya ndani kujenga SGR, Rufiji hydroelectric dam na ununuzi wa ndege, kama tungekopa jumla ya deni lingekua $7.6B.

Kuhusu pesa kuingia katika county level, hiyo ni miongoni mwa failures ya serikali yenu, research zinaonyesha kwamba pesa nyingi inayopelekwa ktk counties inatumiwa vibaya kuliko iliyopo central government.
 
Green field terminal..
Galana Irrigation project
Mumia sugar company
Crude oil pipeline
BRT
Electrification of old model diesel SGR
Lamu port
5 big stadia
Laptop per child
Mombasa Nairobi super high way

Hongera sana GoK kwa kukamilisha ahadi zenu.
Elezea sisi mkopo wenu wa $2 billion ulikuwa wa kufanyia nini? Passed State. Vile vile weka project yeyote ambayo iko complete and working kama Kweli ipo.
 
Hakuna mtu alikua akipinga SGR SGR yetu kama wewe ulikua unapinga sana tu mpaka ukasema tukitandika reli kilomita moja utatembea uchi, lakini saivi ni aibu tupu imekujaa

JPM is another level
Kweli kabisa mkuu JPM yuko in another level of peddling lies and propaganda... hapo sitabisha.
Nikuulize swali mboga mno, je Tz in drones?
 
Elezea sisi mkopo wenu wa $2 billion ulikuwa wa kufanyia nini? Passed State. Vile vile weka project yeyote ambayo iko complete and working kama Kweli ipo.
Soma post yangu #43. BRT is completed, Nyerere/ Kigamboni bridge is completed, gas pipeline from Mtwara to Dar is complete.

Onyesha ni project gani yenye thamani ya $1B au zaidi ambayo inatekekezwa kwa pesa yenu ya ndani. Onyesha ni project gani kwenu ipo completed. Jibu maswali Tafadhali.
 
Sisi hukopa na kukubali bila kuyumbayumba. Je SGR yenu imefika wapi na inetumia pesa ngapi za ndani na usisahau kuna video ya mbunge wenu ndani ya bunge in National TV.
Joto la Jiwe Wacha nikuulize swali mboga kabisa... Je Tanzania mnaweza afford drones?
 
Nimekuambia niambie ni project gani yenye thamani ya $1B au zaidi inayotekelezwa na GoK, sisi tunatekeleza projects zenye thamani ya $6.7B, naomba ujibu hili swali kwanza, then nitakujibu maswali yako.
 
Nimekuambia niambie ni project gani yenye thamani ya $1B au zaidi inayotekelezwa na GoK, sisi tunatekeleza projects zenye thamani ya $6.7B, naomba ujibu hili swali kwanza, then nitakujibu maswali yako.
Sisi hatuna kubwa kama yenu sis bado maskini. Je Tanzania INA drones?
 
Sisi hatuna kubwa kama yenu sis bado maskini. Je Tanzania INA drones?
Drone ziko za aina nyingi sana, kuanzia civilians, military na for special missions. Wewe unazungumzia Drones zipi?, kumbuka kwamba ni Tanzania na Rwanda pekee zenye kutumia drones kusafirisha dawa na damu vijijini kwa ajili ya kusave lives.
 
Drone ziko za aina nyingi sana, kuanzia civilians, military na for special missions. Wewe unazungumzia Drones zipi?, kumbuka kwamba ni Tanzania na Rwanda pekee zenye kutumia drones kusafirisha dawa na damu vijijini kwa ajili ya kusave lives.
Sawa basi sasa tuwekee drone pictures za 47% SGR. Ni hayo tu all it never happened.
 
Hiyo $1.9B niliyo ongelea ilikua ni external debt, bado hatujaongelea Domestic debt ya serekali.....

Nimeitafuta hiyo ripoti ya BoT ili tuongelee hali halisi....






Kwahivyo kuanzia Jan 2017 hadi Jan 2018 serekali kuu ya Tz ilipokea 78.8% of $2.056Billion of external debt ambayo ni approximately $1.5B external debt.
Kati ya Dec 2017 na Jan 2018 mlipokea $67.7 Million dollars, Hatujui zilitumika kufanya nini lakini top of my head najua Bombadier moja inauzwa $32million..... kwahivyo for $67Million unaeza ukapata Q400 mbili + customisation + Pilot training + fuel cost ya kuisafirisha kutoka canada hadi Tz.. ... hilo ni wazo tu... just saying


Ikija Kwa Domestic Debt,





Ukijumuisha monthly Domestic Debt kuanzia Feb 2017 hadi Jan 2018 ambayo inaonyeshwa on top of each bar inakua 7.3 Trillion TZS ambayo kama hesabu zangu ziko sawa 7.3 Trillion TZS ni kama $3.2 Billion USD.



Kwahivyo hapo mkujumuisha external + Internal debt ni kama $4.7B for 2017... Alafu ukumbuke si miradi yote hulipiwa pesa zote kwa mpigo, kwa mfano nakumbuka Ujenzi wa SGR-TZ ulipoanza mlilipa $500m alafu mkangoja next financial year ndo mkalipa $500m...etc,
Project zengine ambazo umetaja hazijaanza na nyengine ambazo zimeanza pia hazijalipiwa zote kwa mpigo kwahivyo hio mikopo imetumika kwa project nyingi zaidi ya hizo ulizotaja......



( Kenya inaongoza kwa WB Logistics Performance Index kwahivyo hakuna vile utaniambia hakuna kinacho onekana on the ground huku Kenya. )
Mimi siko hapa kuwakosoa kuchukua mikopo wala kuingilia/kukagua miradi yenu kwahivyo sitajisumbua kutoa list ya miradi mikubwa inayofanyika kenya. Ninacho jaribu kusema ni kwamba wajinga pekee ndo wanaeza kudanganywa na Propaganda za CCM kua miradi yao yote mikubwa inalipiwa kwa cash na pesa za serekali wakati serekali inapokea mikopo mikubwa kila siku, na hata kama hiyo miradi inalipiwa na cash pesa za walipa kodi watanzania, hiyo mikopo inatumika kujaza pengo lilioachwa na pesa zilizotumika kwa hio miradi kwahivyo nikama serekali inacheza mchezo wa karata wa pata potea ...
 
Wewe unatapatapa baada ya kuona Tanzania inatumia pesa yake katika miradi mikubwa jambo ambalo Kenya imeshindwa, zaidi ya kupiga kelele za GDP
1) Kila mkopo tunaochukua, unaeleweka na bunge linajulishwa kwanini serikali inakopa, wewe unaleta hesabu za Bank kuu, Tafadhali onyesha hizo pesa zilikopwa kwa sababu gani, utapata jibu wapi zilitumika.

2) Nimekuonyesha miradi ambayo tunaitekekeza kwa pesa za mikopo toka nje, kwa ujinga wako bado unauliza hizo pesa zimefanya kazi gani, unadhani BRT, TAZARA flyover, JKNIA Airport, Ubungo interchange, Salender bridge, Uboreshaji wa Dar na Dodoma, yote hiyo tunatumia pesa zipi?.

Deni la ndani kwetu huku zaidi ni local suppliers, malipo ya watumishi na wastaafu mbalimbali, na madeni yaliyoachwa na utawala dhahifu wa Kikwete, yanalipwa taratibu baada ya kufanyiwa verifications.

Tafadhali onyesha miradi inayogharimiwa na GoK, taja mradi mmoja wenye thamani ya $1B unaotimia pesa ya ndani.
 
Rufiji mpende msipende ni 10 to 15 years , hakuna kitu siajabu usiishe, na nakwambia half ya watu humu watakuwa wamekufa, na deni kulipwa na watoto zao
 
Hahhahaha yaani manufacturers wahamishie viwanda tanzania au ethiopia . Kwa incentive gani?
 
joto la jiwe hujajibu swali langu umelikwepa na kuanza visingizio basi muite mwenzako NDINDA akusaidie uone vile hata yeye atatoroka....Njia ya muongo ni fupi. Hamna 47% yeyote ujenzi hata nashuku umesimama mkizingija hela za mkopo.
 
Hahahaa... naona nimekukurupua kutoka kwenya kibanda chako hapo Kibera ata mswaki hujapiga [emoji1] . Ilibidi iwe 10,000 MW by that time Ken Power itakua inunua umeme wa bei chee toka Tz na Ethiopia.

Hakuna shida. Kama bei ya umeme kutoka jirani pamoja na transportation yake kuja Kenya itakuwa chini kuliko umeme wa Kenya, tutanunua tu.
Lakini kama mnataka kuzalisha umeme zaidi ya mnavyohitaji, ili muuzie Kenya, mtapata tabu sana. Kenya pia ina miradi yake ya umeme.
 
Yaani wakenya hawataki Tz iwe na mradi wake wa kufua umeme? Mnatokwa na povu humu nikama JPM amelala na bibi zenu😂😂
Lakini si ajabu...Ndege mlisema ni mitungi ya changa'a, SGR mkasema ni ndoto..Kweli JPM amewafanya mkose usingizi!
Kenya kila kuchao habari ni za mijizi ikiiba billions, hakuna habari za uwekezaji mpya, new projects zimefungwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…